NJOMBE

NJOMBE

Thursday, February 2, 2012

bil.117/- zahitajika ujenzi wa U/Ndege Msalato

SERIKALI imesema inahitaji sh bilioni 116.95 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege uliopo Msalato mkoani Dodoma.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athman Mfutakamba, alipokuwa akijibu swali na Mbunge wa Bahi, Omary Badwel (CCM) aliyetaka kujua ujenzi wa uwanja huo utaanza lini.
Badwel alihoji kiwanja hicho kinatarajiwa kuwa na ukubwa gani kulingana na mahitaji ya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi.
Mfutakamba alisema serikali inatambua umuhimu wa kuwa na kiwanja kikubwa cha kisasa cha ndege mkoani hapa.
Alisema kutokana na hilo hatua za awali za ujenzi huo zilianza ikiwamo kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Kiwanja cha Ndege cha Msalato kwa gharama ya sh milioni 715.5 kupitia msaada wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo kwa Afrika (BADEA).
Alisema serikali imekamilisha ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaozunguka eneo hilo ambapo wananchi 1,432 wameshalipwa.
“Kazi ya kusafisha maeneo yatakayojengwa miundombinu ya kiwanja kama vile barabara ya kurukia ndege, jengo la abiria na miundombinu mingine ya kiwanja imekamilika,” alisema.
Alisema kwa sasa wanaendeleza majadiliano na washirika wa maendeleo ya taasisi mbalimbali za kifedha kwa ajili ya kukusanya fedha za ujenzi wa uwanja huo.

No comments:

Post a Comment