NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, February 1, 2012

Mil.12/- zawafuta jasho walioharibiwa mashamba

JIBU LA SWALI LA MBUNGE Biharamulo magharibi


KIASI cha sh milioni 12.4 zimetumika kuwafuta machozi wakulima wenye mashamba yaliyoharibiwa na wanyamapori wilayani Karagwe, Kagera.
Fedha hizo zimetolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo jumla ya wakulima 124 walinufaika.
Aidha, wizara hiyo imelipa jumla ya sh mil. 12.4 kwa ajili ya kufuta machozi na jasho kwa wananchi waliopata madhara kutokana na wanyamapori wakali na waharibifu.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Benedict Ole-Nangoro, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Biharamulo Magharibi Dk. Anony Mbassa (CHADEMA) kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.
Mbunge huyo alitaka kujua pamoja na mambo mengine, iwapo wananchi wanaopakana na Hifadhi ya Burigi kama wamelipwa fidia kutokana na uharibifu wa mashamba na madhara kwa binadamu unaofanywa na tembo, nyati na wanyama wengine wakali.
Alitaka kujua kiasi cha fidia kilicholipwa kati ya mwaka 2000 na mwaka 2011.
Akijibu swali hilo Ole-Nangoro alisema jumla ya wananchi saba wamelipwa fedha za kifuta machozi kwa madhara waliyopata kutokana na wanyamapori wakali katika wilaya za Ngara na Karagwe.
“Tangu mwaka 2005 hadi 2006 kiasi cha sh 250,000 kililipwa kwa familia za marehemu wanne waliouawa na tembo na watatu waliojeruhiwa,” alisema naibu waziri huyo.
Alisema wizara hiyo hutoa asilimia 25 ya fedha zinazotokana na mapato ya uwindaji wa kitalii katika pori la Akiba la Burigi kila mwaka ambapo hupelekwa kwenye halmashauri za wilaya husika kwa ajili ya maendeleo ya jamii.

No comments:

Post a Comment