NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, February 1, 2012

Madaktari, serikali zungumzeni - Wahariri

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF), limeshauri serikali na madaktari kukaa katika meza moja ya mazungumzo ili kutafuta muafaka wa mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.
Taarifa ya TEF iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wake, Neville Meena, ilisema majadiliano hayo yatakayofikiwa na pande hizo mbili, yalenge kutatua matatizo ya madaktari, lakini pia yazingatie uwezo wa serikali.
Meena alisema lengo liwe kuwawezesha madaktari kadiri uwezo wa serikali unavyoruhusu sambamba na kuwaokoa wagonjwa wanaokabiliwa na hatari kubwa kwa sababu ya kukosa tiba.
“Madaktari wakubali kurejea kazini haraka iwezekanavyo ili kuokoa maisha ya watu ambao wanapoteza maisha kutokana na kukosa tiba, wakati wagonjwa wakiwa si sehemu ya mgogoro uliopo,” alisema katibu huyo.
Vile vile, Meena aliishauri serikali kufuta amri zake zote dhidi ya madaktari ambao hawakuripoti kazini juzi, ili kuwezesha mazungumzo ya pande zote mbili kufanyika.
“Baada ya maafikiano kuwapo, usiwepo mpango wowote wa wazi au wa kificho wa kuwaadhibu kwa namna yoyote ile viongozi wa madaktari waliogoma kwani tunaamini kwamba madai yao yalikuwa halali,” alisema.

No comments:

Post a Comment