NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, November 27, 2012

Hivi ndivyo alivyosema kamanda wa Polisi juu ya kifo cha Sharoo

Kuhusu kifo cha msanii/mwigizaji Sharo Milionea, namkariri Kamanda wa Polisi Tanga akisema “leo majira ya saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza alipofika eneo hilo gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza” Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei. Kwenye gari alikua mwenyewe

GARI NA MAHALI ALIOPOKATIA ROHO SHARO MILIONEA


Hili ndilo gari aina ya Toyota Harrier lenye namba T278 BVR ilipinduka na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha msanii Sharo milionea USIKU WA JANA MIDA YA SAA MBILI USIKU
VIDIO AMBAZO SHAROO ANAHUSIKA
  
HIVI NDIVYO MWILI WA MAREHEMU SHARO MILIONEA ULIVYO BAADA YA KUPATA AJALI ** TUNAOMBA RADHI KWA PICHA UTAKAYOONA **

Monday, November 26, 2012

BREAKING NEWS ILIYOTUFIKIA SHAROO MILIONEA AFARIKI DUNIA


Sharoo Milionea afariki dunia kwa ajari ya gari iliyopinduka akitokea Dar es salaam akielekea Muheza Tanga habari zaidi.Tutaendelea kukupa 
Bwana alitoa Bwana katwaa ilazwe pema peponi Sharoo Milionea

BOCCO NA NGASSA WAISULUBU SUDANI 2-0

SPORTS/MICHEZO

Mshambuliaji wa timu ya Kilimanjaro Stars, Mrisho Ngassa akikokota
mpira uliozaa goli la pili wakati wa mchezo wa Cecafa Challenge 2012
dhidi ya Sudan uliochezwa katika Uwanja wa Mandela Jijini Kampala

Mashabiki wa timu ya Kilimanjaro Stars waliosafiri kutoka mkoani
Kagera wakishangilia baada ya kufungwa kwa goli la kwanza wakati wa
mchezo wa Cecafa Challenge 2012  dhidi ya Sudan uliochezwa katika
Uwanja wa Mandela Jijini Kampala

Mshambuliaji wa timu ya Kilimajaro Stars, Simon Msuva akimtoka beki wa
timu ya Sudani, Faris Abdallah wakati wa mchezo wa michuano ya
Challenge uliofanyika katika Uwanja wa Mandela Jijini Kampala 

Kilimanjaro Stars wakishangilia goli la kwanza lililofungwa na John
Bocco wakati wa mchezo dhidi ya Sudan katika michuano ya CECAFA
Challenge katika Uwanja wa Mandela Jijini Kampala

Erasto Nyoni wa Kilimanjaro Stars na beki wa timu ya Sudan, Faris
Abdallah wakiwania mpira wakati wa mchezo wa michuano ya Chalenge
uliochezwa katika Uwanja wa Mandela Jijini Kampala jana






Kabila ataka M23 waondoke Goma

Serikali ya Jamhuri ya Demokrasi ya Congo inasema haitazungumza na wapiganaji wa M23 hadi waondoke mji wa Goma ambao waliuteka juma lilopita.
Wanajeshi wa serikali kabla ya mji wa Goma kutekwa
Taarifa hiyo imetolewa siku moja baada ya mkutano wa viongozi wa Maziwa Makuu mjini Kampala, Uganda, kuwasihi wapiganaji waondoke Goma.
Msemaji wa wapiganaji, Kasisi Jean-Marie Runiga, alisema wapiganaji wataondoka Goma baada ya mazungumzo ya amani lakini siyo kabla.
Rais Joseph Kabila wa Congo alikutana na wawakilishi wa wapiganaji mjini Kampala Jumamosi.
Wakuu wa Uganda wanasema yamekuwapo mawasiliano baina ya pande hizo mbili.

Friday, November 23, 2012

Wachezaji 5 watangazwa

Tuzo mchezaji Bora wa BBC 2012
Tuzo mchezaji Bora wa BBC 2012
Majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo la BBC la mchezaji bora zaidi barani Afrika mwaka 2012 yametangazwa.
Yaya Toure, kwa mwaka wa pili mfululizo, yupo kwenye orodha hiyo.
Mwenzake katika timu ya taifa ya Ivory Coast, Didier Drogba pia yumo.
Wachezaji wengine ni pamoja na Demba Ba kutoka Senegal, Younes Belhanda wa Morocco na nahodha wa timu ya Zambia, Christopher Katongo.
Huu umekuwa ni mwaka wa ufanisi kwa wachezaji hao, na timu za wachezaji wanne zikionyesha ustadi kwa kupata vikombe.
Bofya Ukitaka kupiga kura unaweza kufungua anwami hii ya mtandao na kumbuka maagiza yametolewa kwa lugha ya Kiingereza.
Inaelekea Drogba aliondoka Chelsea wakati muwafaka, mara tu baada ya timu yake kukamilisha msimu kwa ushindi wa klabu bingwa barani Ulaya, hii ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya klabu, na vile vile akipata bao la ushindi katika fainali ya Kombe la FA.

Wanaowania tuzo la BBC

Yahya Toure Bofya Yahya Toure.Mcheza kiungo kutoka Ivory Coast, anayeichezea Manchester City ya Uingereza. Toure aliiongoza Manchestert City kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita.
Demba Ba Bofya Demba Ba kwa sasa ni mmoja wa wachezaji nyota wa klabu ya Newcastle na kufikia sasa tayari amefunga jumla ya magoli 6 katika ligi kuu ya premier la England na anatarajiwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Senegal kitakachocheza katika fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika.
Didier Drogba Bofya Didier Drogba ni noadha wa timu ya taifa ya Ivory Coast, amewahi kuongoza Chelsea kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England pamoja na kombe la klabu bingwa barani ulaya.
Chrsitopher Katongo Bofya Christopher Katongo ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo na aliiongoza timu hiyo kushinda fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika
Younes Belhanda Bofya Younes Belhanda ni mchezaji mwenye umri wa miaka 22, na mmoja wa wachezaji waliotia fora na kuisaidia klabu ya Montepellier, kushinda kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya karne moja tangu klabu hiyo ilipobuniwa.
Raia mwenzake wa Ivory Coast, Toure, naye akiichezea Manchester City, aliihakikishia timu yake ubingwa wa ligi kuu ya Premier kwa mara ya kwanza; kombe lao muhimu zaidi katika kipindi cha miaka 44.
Belhanda aliisaidia timu yake ya Ufaransa ya Montpellier kupata ushindi katika ligi ya Ufaransa daraja la kwanza, kwa kufanikiwa kupata magoli 12 katika msimu.
Katika mapambano ya kimataifa, Katongo, kutoka Zambia, naye akiiongoza timu kama nahodha, alifanikiwa kuiwezesha timu yake ya Chipolopolo kuishinda Ivory Coast, na kuibuka mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya kuishinda Ivory Coast katika fainali, kupitia mikwaju ya penalti.
Ba hakung'ara katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya Senegal kuondolewa katika hatua ya makundi, lakini binafsi aliweza kuifanyia timu yake ya Newcastle kazi nzuri, na msimu uliopita alitangazwa kuwa mshambulizi bora zaidi, kwa kufunga jumla ya magoli 17, na kuiwezesha timu kumaliza katika nafasi ya tano.

Baada ya kocha wa Chelsea Roberto Di Matteo sasa Zamu ya Mark Huges

  Mark Huges afutwa kazi
 
Mark Hughes
Mark Hughes
Kocha wa QPR, ambayo kwa sasa iko mkiani kwenye msururu wa ligi kuu ya Premier ya England Mark Hughes amefutwa kazi.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, kocha huyo amefutwa kazi kutokana na matokeo mabaya tangu kuanza kwa msimu huu.
Baada ya mechi 12 kuchezwa QPR haijashinda hata mechi moja.
Taarifa hiyo imesema kuwa, bodi hiyo inajadili mipango ya kutangaza wasimamizi wapya wa klabu hiyo muda mfupi ujao.
Mark Bowen na Eddie Niedzwiecki watasimamia klabu hiyo wakati wa mechi ya ya kesho Jumamosi dhidi ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford.
''Bodi ya wakurugenzi ingependa kutoa shukrani kwa Mark, kutokana na juhudi zake wakati alikuwa kocha wa klabu hiyo kwa muda wa miezi kumi iliyopita'' taarifa hiyo iliongeza.
Wakurugenzi hao wamesema watangaza mipango mipya ya klabu hiyo muda mfupi ujao na aliyekuwa kocha wa Tottenham Harry Redknapp anatarajiwa na wengi kuteuliwa kuwa kocha mpya wa QPR.

Mkuu wa Majeshi DRC afutwa kazi

Generali Amisi
Generali Amisi
Mkuu wa majeshi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amesimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea kufuatia madai kuwa aliwauzia silaha makundi ya waasi yanaopambana na serikali ya nchi hiyo.
Ripoti moja ya Umoja wa Mataifa, imemtuhumu, Generali Gabriel Amisi kwa kuendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa wawindaji haramu na makundi ya waasi, likiwemo kundi la Mai Mai Raia Mutomboki.
Msemaji wa serikali ya nchi hiyo amesema, maafisa kadhaa wa jeshi pia wanachunguzwa.
Serikali ya Rais Kabila imemfuta kazi mkuu huyo wa majeshi, siku chache baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Goma Mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi hao mpia wameutekja mji wa Sake, lakini msemaji wa serikali Lambert Mende, amesema wanajeshi wa serikali wamefanikiwa kuumboa tena mji huo mdogo.
Waasi hao ambao wanaaminika kuungwa mkono na serikali za Rwanda na Uganda, wametishia kuendeleza mapigano hayo hadi mji mkuu wa Kinshasa, ikiwa rais Joseph Kabila hatabuli kuanzisha mazungumzo ya amani.

Mazungumzo ya Amani

Rais wa Uganda
Uganda inaandaa mkutano wa marais wa Rwanda na Uganda hii leo na kuna ripoti kuwa baadhi ya viongozi wa kundi hilo la waasi wa M23 wamesafiri mjini Kampala kushiriki katika mazungumzo hayo.
Ripoti iliyoandikiwa Umoja wa Mataifa na kundi moja wa wataalamu huru, imesema kuwa Generali Amisi, anaendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa makundi ya kihalifu na waasi wanaohudumu Mashariki mwa Congo, eneo ambao bado kuna idadi kubwa ya wapiganaji wa waasi.
Hata hivyo kundi hilo la M23 halikuwa miongoni mwa makundi yaliyotajwa kwenye ripoti hiyo lakini kundi la Raia Mutomboki, moja ya makundi kadhaa yanayojumuisha wapiganaji wa Mai Mai, inaaminika kuwa na uhusiano wa karibu na kundi hilo la M23.
Ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa imenadi kuwa Generali Amisi aliagiza bundi 300, aina ya AK-47 kukabithiwa kundi moja linalohudumu katika eneo hilo la mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lijulikanalo kama Nyatura.
Ripoti hiyo imeongeza kusema kuwa waasi hao wananunua risasi kutoka kwa nchi jirani ya Congo na kusafirisha kupitia Kinshasa hado Mashariki mwa nchi hiyo na mtandao unaoendeshwa na washirika wa Generali Amisi, wakiwemo baadhi ya jamaa ya familia yake.

Tuesday, November 20, 2012

HAYA NDIO MAJIJI MASAFI DUNIANI YALIYOPO KUMI BORA

Hii ni orodha ya majiji kumi bora duniani kwa usafi, kwa mujibu wa jarida la Forbes kwa mwaka 2011.

Dodoso: Je, waafrika ni wachafu? Kwa nini hakuna jiji hata moja la Afrika kwenye Top 10?
Hii ni orodha ya majiji kumi bora duniani kwa usafi, kwa mujibu wa jarida la Forbes kwa mwaka 2011. 

Dodoso: Je, waafrika ni wachafu? Kwa nini hakuna jiji hata moja la Afrika kwenye Top 10?

Monday, November 19, 2012

MIAKA HATARI YA KUVUNJIKA KWA NDOA



Watafiti wa masuala ya uhusiano na ndoa wana kalenda za miaka ya hatari iliyotafsiriwa sambamba na sababu zinazoweza kuvuruga uhusiano na kuwafanya watu waliokuwa wakipendana kuachana.
 Hivyo kwa dondoo tu nimeona ni vyema niwafundishe watu wanaoishi kwenye ndoa sababu zinazotafsiri ukomo wa mapenzi yao kulingana na miaka husika iliyotafsiliwa na watalaamu wa masuala ya ndoa na uhusiano.
 Wanasaikolojia mbalimbali ulimwenguni kupitia tafiti zao walikubali kuuweka UGOMVI kuwa katika sababu zinazoweza kusababisha ndoa kuvunjika ndani ya mwaka 1-2. Wanasema endapo watu waliooana wakianza kugombana kati ya mwezi wa kwanza na kuendelea, basi ujue kuwa wanandoa hao hawawezi kuvuka miaka miwili kabla ya ndoa yao kuvunjika.
 Jambo la kuzingatia katika sababu hiyo ya ugomvi iliyotajwa ni  kwamba watafiti hao hawachukulii hitilafu na migongano ya kawaida kama sababu, bali mikwaruzano mikubwa yenye kuumiza mwili au roho kwa kiasi kikubwa.
  Watafiti hao wanasema wanandoa wapenzi wanaogombana kwa kipindi hicho huwa na kasoro ya ulinganifu wa tabia, mawazo na mwelekeo hivyo kuwafanya wasiweze kuishi pamoja kwa muda mrefu.
 Hivyo ili wanandoa wasiweze kuachana katika miaka miwili ya mwanzo wanashauriwa kuoana baada ya kuchunguzana vema tabia na kulingana katika hali. (Soma TITANIC 1 njia za kutafuta mchumba)
 Mwaka mwingine wa hatari ni wa NNE. Baada ya kuoana mwaka wa nne unatajwa na watafiti kuwa ni wa hatari katika kuwafikisha wapendanao  ukingoni mwa mapenzi yao. Sababu ambayo inapewa uzito katika kizuizi hiki cha ndoa ni kufanikiwa kupata MTOTO.  

Kuwekwa kwa mtoto katika kizingiti hiki kunaonekana na tafiti nyingi kuonesha kuwa wanandoa wanapofanikiwa kupata mtoto hujisahau na kuhamisha mapenzi yao kwa mtoto, huku wakijisahau kuwa wao pia wana jukumu la kupendana.
 Watafiti hao wanasema wapendanao wanapokuwa na mtoto, muda mwingi humfikiria zaidi yeye.  Kama ni suala la kuchukua zawadi za kurudi nazo nyumabani hazitakuwa kwa ajili ya mume/mke bali itakuwa ni kwa mtoto.  Pia msukumo wa kujali, kuhudumia kubembeleza na ukaribu utahamia kwa mtoto, jambo ambalo litawafanya wapendanao hao kujiona kama watu wasiohitajiana sana na hivyo kuleta hatari ya ndoa kufikia ukomo.
 Ili kukwepa ndoa kuvunjika katika mwaka huu, wanandoa wanashauriwa kuwa baada ya kupata mtoto wasisahauliane, wawe na vipindi vya kuwa pamoja na kushirikiana kama mwanzo, kwa lengo la kulinda upendo wao usiharibike.
 Baada ya kuvuka miaka hivyo, mwaka wa saba tangu kuoana unawekwa kuwa ni mwaka wa kizingiti cha mwisho cha wanandoa kuachana.  Kinachosababisha hatari za mwaka huu kuwemo katika fungu hilo ni MAISHA, MAJUKUMU NA MAZOEA.  
Katika kufafanua mwaka huu watafiti hao wameeleza sababu nyingi, lakini za msingi ni hizo ambazo nimezitaja.
 Wanasema katika mapito ya maisha kuishi kwa wanandoa ndani ya ndoa kwa miaka hiyo saba kutakuwa kumewatumbukiza katika kukabili matatizo mengi ya kimaisha na hivyo kuwafanya wazidiwe na harakati za kujikimu.  Kwanza watakuwa wamepata majukumu ya kulea familia, kutunza watoto wao, ambao tayari watakuwa wameanza kusoma n.k.
 Lakini sababu ya kuzoeana inatajwa kuchangia kuondoa msisimko wa kupendana na hivyo kuamsha hisia potofu kuwa mwanandoa anaweza kuishi bila mume au mke wake. Hivyo ili kulinda ndoa katika kipindi hiki cha miaka saba, wanandoa wanashauriwa kutotumia muda wao mwingi kwenye pilika pilika za kimaisha kiasi cha kukosa muda wa kuwa pamoja.
 Hata hivyo wakati watafiti hao wanakubaliana kuwa miaka iliyotajwa ni ya hatari katika kuvunjika kwa ndoa, bado wanarudi katika kapu hilo kwa kusema wanandoa ambao wanaachana baada ya kuishi kwa zaidi ya miaka hiyo iliyotajwa, yaani miaka minane na kuendelea wanaingia katika kundi la wazembe na wavivu wa kufikiria misingi ya ndoa yao.
 Wanasaikolojia wanasema watu walioishi kwa miaka hiyo huwa hawana majibu sahihi yanayoweza kushibisha sababu za kuachana kwao.  Wanachokiamini wataalamu hao ni kuwa, hakuna tabia, mwenendo, migongano mabishano na purukushani mpya za kimaisha zinazoweza kuwatokea wanandoa hao kiasi cha kuonekana kuwa ni sababu za kupiku mazoea na kushindwa kuvumiliana.

Katika kuhitimisha hilo niseme tu kwamba, ili kuepukana na kikwazo cha kwanza watarajiwa wa ndoa wanashauriwa kuchanguana kwa kuzingatia ulinganifu wa tabia. Vijana wengi siku hizi hawazingatii ulinganifu wa kitabia, badala yake wanachagua wenza kwa kufuata uzuri na pesa, huku wakilenga kupata sifa toka kwa rafiki zao

Katika kikwazo cha pili, ushauri uliopo ni kuwa makini juu ya malezi ya watoto na kuepuka kusahauliana.  Watoto wanapaswa kuwa ndani ya upendo wa mume na mke.  Kuhusu kizingiti cha miaka saba, ushauri na kuepuka kuzoeana na daima kujizatiti kukabiliana na changamoto za kimaisha bila kukata tamaa.

Sunday, November 18, 2012

HABARI YA KUSIKITISHA MZEE MAKWETA AFARIKI DUNIA




 


 


WAZIRI wa zamani wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Jackson Makwetta amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam jana.
Taarifa zilizopatikana jana na kuthibitishwa na mtoto wa marehemu, Tumwanuke Makwetta zilisema kuwa marehemu alifariki jana jioni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini ambako alikuwa amelazwa kwa matibabu.
Kabla ya kuhamishiwa Muhimbili, mwanasiasa huyo mkongwe nchini, alifikishwa Hospitali ya Lugalo wiki iliyopita  baada ya hali yake kuwa mbaya kutokana na maradhi ya moyo.
Mtoto wa marehemu, Tumwanuke Makwetta  aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa taarifa zaidi kuhusu msiba wa mzee wao zitatolewa baadaye.
“Kwa sasa siwezi kusema lolote kwa sababu ndiyo tunatoka hospitali kuelekea nyumbani, taarifa zaidi nitakujulisha baadaye,” alisema.
Mtoto wa marehemu alisema kuwa baba yao alifariki  jana jioni walipokwenda kumjulia hali.
Makwetta alianza kuugua akiwa nyumbani kwake Njombe na akapelekwa kutibiwa katika Hospitali ya Consolata ya Ikonda, wilayani Makete na baadaye wiki iliyopita alihamishiwa katika Hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam baada ya kuzidiwa.
Muda mfupi kabla ya kifo chake, Rais Jakaya Kikwete alifika hospitalini hapo kumjulia hali.
Gazeti hili lililokuwa hospitalini hapo lilishuhudia msafara wa Rais ukifika hospitalini hapo na kuingia wodini na baadaye kuondoka.
Rais Kikwete alitumia fursa hiyo pia kuwapa pole wagonjwa wengine waliokuwa wakihudumiwa hospitalini hapo.
Wasifu
Alizaliwa Juni 15, 1943. Alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 1976-1980, mwaka 1982-83 alikuwa Waziri wa Nishati na Madini.
Makwetta pia aliteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo na Chakula mwaka 1983-1987, alibadilishwa wizara na kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa mwaka 1987-1989.
Marehemu alishika wadhifa wa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi mwaka mmoja kuanzia 1989-1990 na baadaye alihamishiwa Wizara ya Kilimo na Chakula mwaka 1991-1992.
Pia amewahi kuwa Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu mwaka 1995-1998.
Makwetta amekuwa Mbunge wa Jimbo la Njombe Kaskazini tangu 1975 hadi 2005, alipoenguliwa katika kura za maoni na aliyekuwa mgombea mpya wa CCM, Deo Sanga.
Pia marehemu ni miongoni mwa mawaziri walioshika nyadhifa za uongozi katika Serikali ya Muungano katika awamu tatu; Awamu ya Kwanza ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Awamu ya Pili ya Ali Hassan Mwinyi na Awamu ya Tatu ya Rais Benjamin Mkapa.CHANZO MWANANCHI

NAWATAKIA JUMAPILI NJEMA NDUGU ZANGUNI.

Mimi kijana mwenzenu na mwanenu nawatakia nyote jumapili njema.Tumshukuru mungu kwa pamoja kwa kupata anagalau neno la kushibisha roho kwa njia ya nyimbo.
Mwambie bwana akutete na kisha akuinue
                      Hapa Upendo Nkone anasema Bwana nitetee

                  Hapa Sarah Kiari anamwambia bwana niinue


Saturday, November 17, 2012

Vuta Hisia Toka Nyerere Hadi Kikwete


Niambie umejifunza nini toka kwa Mwalimu na Jakaya je umeona tofauti yoyote hapo hebu tu saidiane kwa comment yako.

Friday, November 16, 2012

UZAZI WA MPANGO HUPONYESHA NA KUSAIDIA WAGUMBA.

Mama Kataraiya talking to journalists
HUDUMA ya Uzazi wa Mpango ina faida nyingi ikiwa ni pamoja na kuponyesha wanawake wenye matatizo ya maumivu wakati wa hedhi na kusaidia wagumba kupata watoto.
Kutokana na manufaa hayo, akina mama wametakiwa kujiunga na uzazi wa mpango na wanaotumia uzazi huo, kujiepusha na magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende ambayo husababisha madhara kwa wanawake na kuathiri uzazi wa kawaida na wa mpango.
Hayo yamesemwa kwa nyakati tofauti hivi karibuni na Mkufunzi wa Uzazi wa Mpango wilayani Kahama Adventina Kataraiya na mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Kagongwa, iliyopo katika kata ya Asagehe wilayani hapa.
Kataraiya alisema kwamba ugonjwa wa kaswende unaongoza kwa kusababisha madhara ya mimba kwa akina mama wajawazito na kuwa dalili zake hazionekani mapema mpaka anapokuwa mjamzito au anapojifungua.
Aliyataja madhara hayo kuwa ni pamoja na kupata ugumba, kuharibu mimba, kuzaa mtoto mfu, mtoto njiti, mwenye ulemavu, taahira au mtoto kuozea tumboni na kuhatarisha maisha ya mama.
Wataalamu hao walisema kuwa alisema kuwa madhara mengine ya magonjwa hayo kwa baadhi ya wanawake ni kuharibika kwa via vya uzazi na na kuwa si kweli kuwa iwapo wanatumia uzazi wa mpango watapata matatizo ya afya ya uzazi.
Kataraiya alisema, “Madawa ya uzazi wa mpango hayazuii au kutibu magonjwa ya zinaa, ndiyo maana baadhi ya wanawake wanaposhindwa kuzaa au kuharibui mimba, hudhani kuwa ni kwa sababu ya madawa ya uazi wa mpango.”
Alifafanua kuwa “Madawa ya uzazi wa mpango ni salama. Huponyesha wanawake wenye maumivu wakati wa hedhi na kusaidia wagumba, na huweza kuzuia kuanza kwa magonjwa ya kansa kwa wanawake ambao hawajapata ugonjwa huo, na kuwa huweza kusaidia kupata watoto hivyo nawashauri akinamama wenzangu wapimwe na kubaini magonjwa mapema na sio kusingizia dawa za uzazi wa mpango.”
Alidai, kubaini mapema magonjwa na kupata tiba sahihi na ushauri wa matumizi ya uzazi wa mpango na afya ya uzazi, itasaidia kuepuka madhara ya uzazi wa kawaida na uzazi wa mpango.
Alisema njia za uzazi wa mpango zipo za muda mfupi na za muda mrefu zikiwemo za asili na kitaalamu. Njia hizo za kiasili ni unyonyeshaji na kupima ute wa mwanamke ambapo za kitaalamu za muda mfupi ni vidonge vya uzazi wa mpango, sindano na kondomu za kike na kiume.
Njia za muda mrefu ni kitanzi au lupu, vipandikizi na kufunga kabisa uzazi kwa mwanamke na mwanamme ambazo pia hazina madhara yoyote iwapo mtumiaji atafuata masharti na ushauri wa kitaalamu.
“Wanawake wanaotumia njia ya kitanzi wanaweza kupata maambukizi kwa urahisi hivyo wanashauriwa kuzingatiausafi ili kuepuka maambukizi yanayoweza kutokea na kumsababishia kutunga mimba nje ya mfuko wa uzazi.” Alisema mganga mfawidhi Mwaulambo.
Mganga huyo alifafanua kuwa, mama anapofua na kuanika nguo zake anazotumia wakati akiwa hedhi na kuzianika ndani ama chini ya kitanda, ni rahisi kupata maambukizi ya magonjwa kama ya fangas tofauti na yule anayeanika nguo hizo juani na kuzipiga pasi.
“Licha ya kukosa kabisa uzazi, magonjwa hayo ya kaswende au kisonono, humsabisha mwanamke achelewe kubeba mimba na kumuathili kisaikolojia.” Alisema mganga huyo.
Wataalamu hao walitoa wito kwa akina mama kuwahi katika zahanati, vituo vya afya au hospitali ili wachunguzwe maambukizi mbalimbali yakiwemo magonjwa ya zinaa ili kuwaepusha na madhara yatokanayo na maradhi hayo na kuwawezesha kufaidi huduma za uzazi wa kawaida za afya kwa aina mama na uzazi wa mpango.

Thursday, November 15, 2012

Isikilize hii kutoka kwa Rah P.Inasikitisha na inafundisha

Fredinah Peyton a.k.a Rah P


Fredinah Peyton a.k.a Rah P ni msanii wa Hip Hop wa kike kutoka Tanzania.Wengi walijiuliza kuwa dada huyo amepotelea wapi.Rah P yupo Marikani kwa sasa akifanya maisha yake mwenyewe.Je unajuwa ni nini kilimpeleka Marekani,Rah P alienda Marekani kwa lengo la kusoma na alisoma takribani miaka miwili na alikuwa akipata msaada toka Tanzania yani nyumbani na alikuwa akifanyakazi zahapa na pale.Lakini kwa kipindi kifupi hakupata tena hayo mahitaji yake toka nyumbani.Rah P akashindwa kuendelea na shule,Lakini kwa kipindi kifupi alipata mchumba ambaye walikuwa kipendana sana aliyemuahidi kuendelea kumlipia shule na hivyo kabla ya kujuwa mengi zaidi juu ya huyo mpenzi wake alipata ujauzito na kupata mtoto wa kwanza na hivyo jamaa akashindwa na hakutaka kusikia habari ya shule sababu yakuwa na majukumu mengi,Hivyo Rah P akawa ni mama wa nyumbani na akiwa anasoma tu kupitia mtandao (online school) hakuwa anajisikia vizuri kaa tu nyumbani na kuwa mtu wa kulea watoto sababu alijuwa kama kitu chochote kitatokea juu ya huyo mchumba wake atakuwa na kitu cha kumsaidia.Kulingana na maisha livyokuwa jamaa alikwa ni mtu wa kwenda huku na kule akipiga dili zake hivyo Rah P akaendelea na maisha na akapata ujauzito wa pili na wakati huo anapata ujauzito yule jamaa alikamatwa na kuhukumiwa kifungo cha miaka 25 jela.Kwakuwa huyo jamaa alikuwa ni mfanyabiashara ya madawa ya kulevya.Rah P akawa amepatwa na msongamano wa mawazo hivyo akawa ni mlevi mlevi kupindukia iliyompeleka na yeye pia kufungwa jela na mtoto wake wakiume alikuwa na umri wa miezi mitano(5) na wakike umri wa miaka miwili(2) ila alitoka na kugunduwa nijambo gani yampasa afanye kama mungu anavyopendelea awe.Na hivi sasa ameamuwa kuendelea na fani yake ya muziki na kafanya ngoma moja aliyoshirikishwa na mshindi mara mbili wa Tursker Project Fame.Mrwanda Alpha Rwirangira na nyimbo hiyo inakwenda kwa jina la African Swagger
Alpha Rwirangira
 Msikilize hapo wewe mwenyewe umsikie anavyotoa historia yenye kutia majonzi


                            African Swagger-Alpha ft Rah P

JINSI YA KUONDOA HARUFU MBAYA KWENYE MAKWAPA

Najuwa hili janga ni la watu wengi japo kuwa huwa niwaoga kutafuta msaada wa tatizo hili.Si mbaya leo tukipeana pia ushauri na namna tunaweza saidia tatizo hili.
Hakikisha unaoga kila siku ili kupunguza idadi ya bakteria chini ya makwapa, ambayo husababisha kuweka harufu mbaya kwenye mwili. Wakati wa majira ya joto, ambapo ni wakati jasho linakutoka mara kwa mara na husababisha jasho na harufu chini ya kwapa hivyo unahitaji kuoga mara mbili kila siku na sabuni antibacterial na maji moto.
Safisha nguo kat
ika maji ya moto na sabuni ya kuondoa uchafu na mafuta, na kuvaa tu mashati safi na undergarments. Inapendekezwa kuvaa mavazi ya maandishi nyuzi za asili, kama vile pamba na hariri, na nyingine kama hizi ili kusaidia kunyonya unyevu na kuruhusu ngozi yako kupumua.

Wakati unafanya mazoezi tumia nguo zenye vitambaa ambavyo vitanyonya unyevu mbali na makwapa ili kuzuia harufu mbaya.

Vinega, Witch Hazel na Tea Tree Oil
Apple cider siki, vinega nyeupe na witch hazel kupunguza harufu kwenye makwapa kwa kupunguza pH kwenye ngozi. Bakteria wanaisababisha harufu kwenye makwapa hawezi kuishi wakati pH wa ngozi ikiwa ni ndogo. Ili kukabiliana na harufu, loweka pamba katika vinega au witch hazel na kupaka katika makwapa badala ya, au kabla, deodorant. Tea Tree Oil inaweza pia kuwa na manufaa kutokana na tabia yake ya antibacterial.
 

 
 
 
Limau

Kata Limao au ndimu nusu kwa kisu chenye ncha kali.Paka kipande cha limau ulichokata kwenye kwapa lao na kahihisha unalissueeze mpaka litoe maji yake.Weka makwapa yako yapate hewa, ili hiyo juice ya limau uliyopaka ikauke.


Asidi citric katika maji ya limau yataneutralize secretions na kutoka tezi ya jasho, na hivyo kuneutralizing harufu.

Nani kasema uaminifu hakuna siku hizi,Tusikate Tamaa…Uaminifu bado UPO!

Wengi tumekata tamaa ati uaminifu haupo tena. Nikutie moyo kuwa UAMINIFU bado upo. Usipoupata ama kuuona pembeni yako pengine ukisafiri mahali fulani utaukuta.
Kijiji cha mwisho cha mkoa wa Njombe kilichoko kwenye barabara kuu ya kwenda Ruvuma utakuta kijiwe cha mzee mmoja mstaafu wa JWTZ (Jeshi la Wakurya Tangu Zamani!) akiuza miwa, matunda na asali mbichi.
Kilichoshangaza kwangu mimi ni tangazo lilopo hapo kwenye kibao na birika ambalo linatumika kama KIBUBU.
IMG_0782
Kibao kisemacho Angalia Bei-Kama Hatupo Fedha weka kwenye Birika
IMG_0787
Mzee wa Boma.

Wednesday, November 14, 2012

JE WAJUWA VITU VINAVYOWEZA KUMFANYA MTU AKAISHI MIAKA MINGI AU MICHACHE

Jifunze kusamehe na kusahau uishi zaidi


UKITAKA kuwa na maisha marefu na yenye amani, mojawapo ya mambo ambayo unatakiwa kufanya ni kupenda kusamehe na kusahau.
Kama wewe ni mtu wa kuweka moyoni, amini ninachokwambia subiri kuingiwa na magonjwa mabaya kama ya moyo, figo na mengine yanayohusiana na mfumo wa damu kwa ujumla.
Kitaalamu ni hatari zaidi kuweka mambo na kisha kuyarudia, ni kwa sababu unapokuwa na hasira au chuki, mapigo ya moyo yanakwenda kwa kasi au pengine yakaenda kidogo kidogo tofauti na ilivyo kawaida.
Matokeo ya hali hii ni kwamba damu inaweza ikawa inaingia kwa wingi zaidi kwenye moyo au pengine ikawa inaingia kidogo zaidi na hapo huwa ni mwanzo wa matatizo katika mwili.
Ni nzuri ndugu yangu kufahamu kuwa matatizo ni sehemu ya maisha, pekee wasio na shida za dunia hii ni wale ambao wamekufa, lakini kama uko hai, kama si mapenzi, basi mambo ya kibiashara, kazi au hata jirani ama ndugu na wazazi wanaweza kuwa ni kero kwako.
Ni ngumu kufikiri kwamba unaweza kuishi bila kuwa na vikwazo vyovyote; ndio nasema ni suala la msingi kuwa mwangalifu unapokuwa na matatizo kwa kuelewa kwamba shida tumepatiwa wanadamu, kwa hiyo zinapokuwepo ni kuangalia nini cha kufanya ili mambo yaweze kuwa mazuri.
Kufikiria kuachana kwa sababu kuna hali ya kutoelewana, ni ishara kuwa kichwa chako hakina akili nzuri sana tunapolima shamba na kisha tukaona magugu yanaota kwa kasi, tunachokifanya huwa ni kutafuta dawa kwa ajili ya kuua magugu ili mimea ambayo tumepanda iote vizuri, sasa kwanini tunapokuwa na shida kwenye ndoa mnafikiria kuachana? Sio sawa.
Cha msingi kama nilivyosema angalia chanzo hasa cha tatizo ni nini na nini cha kufanya ili muwe wanandoa wenye uhusiano mzuri.
KWA WATU AMBAO SI WANANDOA
Ni ujinga mkubwa kukubali kununua gari ambalo tayari linafuka moshi ndio kusema kwamba kama hamjaoana na tayari mna migogoro, ni vizuri kupata muda wa kutafakari zaidi kama ni lazima kuendelea au la, lakini si jambo zuri sana kuingia kwenye ndoa kama kwenye uchumba tu hakuna amani ya kutosha.
Ni makosa kuamini kwamba leo nanunua gari bovu, halafu ukafikiri kwamba kesho nitapata fundi wa kulitengeneza hatimaye likawa sawasawa. Kama mna hiyo imani ni vizuri basi kuhakikisha kwanza mnaiponya migogoro iliyopo na kupeana muda zaidi, kabla ya kuoana.
KWA WANANDOA TU
Kama nilivyosema, kwa wasio na ndoa, si hekima sana kumsamehe mtu ambaye tabia zake zinaonekana kuwa mbaya; uchumba ni wakati wa kuangaliana, kama unaona mtu hafai, hata kama amefikia hatua gani, mpe nafasi ya kuangaliana zaidi. Usiwe na haraka katika maisha ndugu yangu, utajuta.
Katika ndoa ambacho unatakiwa kufanya ni kujifunza namna ya kuishi pamoja, kusamehe na kusahau pale mnapokoseana.
Hata katika dini tunafundishwa kwamba ni furaha ya Mungu kuona watu wanasameheana, kiasi kwamba baadhi ya vitabu vitakatifu vinaandika kwamba Mungu huwa anakuwa nao wale ambao wanasamehe.
Katika maisha mapya utatakiwa usamehe na kusahau kwa ajili yako mwenyewe, ili kuomba kwako kusizuiliwe na baraka zako zisizuiliwe. Ndio kusema kwamba kama husamehe, ni ngumu nawe Mungu kukusamehe makosa yako.
Kuna wengine katika ndoa unaweza kusikia anakwambia nimekusamehe, halafu siku inayofuata unamsikia tena akisema kwamba aaah nimekusamehe lakini kwa kweli jambo ulilonitendea ni baya sana.
Ndugu yangu jambo moja la msingi sana ambalo ningependa ubaki nalo ni kwamba yuko wapi ambaye hatakukwaza kwa asilimia 100? Hayuko, kwa maana hiyo ni vizuri kujifunza namna ya kuishi na uliyenaye kabla bado hauko kwenye ndoa, pata muda wa kumjua kwa kina kabla ya kuamua. Mkishaingia, mnapaswa kuendelea milele. Mungu awabariki sana.

Heh! Kumbe wasanii wa filamu Wabongo waongo

MWIGIZAJI Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood, Yvonne Cherryl Monalisa amewashutumu wasanii wenzake kwa kusema uongo katika jamii kuhusu maisha yao halisi pamoja na malipo wanayopata.

Binti huyo amedai kwa kufanya hivyo wasanii wengi wemejikuta katika maisha ya kuunga unga kutokana uongo huo.
Baadhi ya wasanii wa filamu wanadanganya sana kuhusu hali halisi ya maisha yao, mtu akipata nafasi ya kuongea na vyombo vya habari kuhusu malipo na maisha yake halisi utakuta akisema kuwa yeye bila kulipwa milioni tano hawezi kushiriki katika filamu, lakini ukweli hakuna msanii wa kawaida anayelipwa fedha kama hizo katika tasnia ya filamu Bongo mimi mwenyewe ni mtayarishaji, anasema Monalisa.
Anaendelea kudai kuwa kutokana na udanganyifu huo Serikali kupitia Bodi ya Filamu iliamua kuongeza gharama za kibali cha kurekodi filamu hadi kufikia Shilingi 500,000 jambo lilofanya wasanii walalamike kama ni fedha kubwa sana kulingana na malipo ya filamu, lakini ilitokana na udanganyifu kutoka kwa baadhi ya wasanii wa filamu kudanganya, mwanadada huyo anasema hali ya soko la filamu ni mbaya kwa sasa.

Tuesday, November 13, 2012

JE WAZIFAHAMU HAKI ZAKO:ZITAMBUE HAKI ZA BINADAMU

Eleanor Roosevelt na Tangazo kilimwengu la haki za binadamu (1949
Najuwa sio kila anayesoma makala hii hajui haki zake bali zipo ambazo yawezekana ulikuwa huzitambui kama ni haki zako.                     Haki za binadamu ni wazo la kuwa kila mtu anastahili haki kadhaa si kwa kutegemea cheo, wala taifa, wala tabaka, wala jinsia, wala dini kwa sababu tu yeye amezaliwa binadamu.

Haki hizi zimeorodheshwa hasa katika Tangazo kilimwengu la haki za binadamu lililotolewa na Umoja wa Mataifa mwaka 1948. Tamko la UM lilikuwa kamilisho la majadiliano kuhusu haki hizi yaliyoendelea kwa karne kadhaa.
Hoja la kimsingi ni kwamba, "Watu wote wamezaliwa huru; hadhi na haki zao ni sawa. Wote wamejaliwa akili na dhamiri, hivyo yawapasa watendeane kindugu". (Kifungu 1 cha tangazo la 1948).
Mizizi ya haki hizo inapatikana katika falsafa na dini mbalimbali ya tangu kale, lakini ilikuwa wakati wa zama za mwangaza tangu karne ya 18 ya kwamba haki hizi zilijadiliwa kwa undani pamoja na swali: ni matokeo gani kuwepo kwa haki hizi yanaleta kwa utaratibu wa siasa, serikali na jamii.

Mfano wa haki za kimsingi

Haki za binadamu za kimsingi ni pamoja na:
  • Kuishi
  • Kuchagua kazi - kutokuwa mtumwa
  • Kuwa na mali
  • Kutoa maoni yake kwa uhuru
  • Kuwa salama, kutotishwa
  • Kuwa na kinga dhidi ya hatua za kisheria, pamoja na nafasi ya kupinga kwa njia halali
  • Kutokamatwa kwa kosa la mtu mwingine
  • Kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya mahakama
  • Kutazamiwa kuwa bila ya hatia kabla mahakama haijatoa hukumu
  • Kuwa na uraia wa nchi fulani
  • Kupiga kura katika uchaguzi huru
  • Kupewa kimbilio kama nchi asilia inazuia uhuru wa msingi
  • Kuchagua dini na kuishi kufuatana na dini
  • Kupinga pamoja na wengine maazimio ya serikali kwa njia ya amani
  • Kupata elimu
  • Kufunga ndoa na mtu mzima yeyote
Hiyo ni kwa kifupi tu Kwa mengine angalia makala juu ya tangazo kilimwengu la haki za binadamu.Zitambue haki zako

HAKI YENYE MFUMO WA USAWA BAINA YA MATAJIRI NA MASIKINI INAWEZEKANA, LICHA YAKUWA WOTE TUNAISHI DUNIANI?

MAANDIKO YA QURAN NA BIBLIA YANASEMAJE?
BIBLIA :
YESU AKASEMA » KWA NINI KUNIITA MWEMA ?
HAKUNA ALIYE MWEMA ILA MMOJA, NDIE MUNGU. WAZIJUA AMRI, USIUE, USIZINI, USIIBE, USISHUHUDIE UONGO, USIDANGANYE, WAHESHIMU BABA YAKO NA MAMA YAKO. AKAMWAMBIA, MWALIMU HAYA YOTE NIMEYASHIKA TANGU UTOTONI MWANGU. YESU AKAMKAZIA MACHO, AKAMPENDA, AKAMWAMBIA, UMEPUNGUKIWA NA NENO MOJA. NENDA , UKAUZE ULIVYO NAVYO VYOTE, UWAPE MASIKINI, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI ; KISHA NJOO UNIFUATE. WALAKINI YEYE AKAKUNJA USO KWA NENO HILO, AKAENDA ZAKE KWA HUZUNI ; KWASABABU ALIKUWA NA MALI NYINGI. »
(MARKO MTAKATIFU 10 :17…..22)


YESU AMEANZA KUTUONESHA KWAMBA MWENYEZI MUNGU NDIE MWENYE UTUKUFU NA MWENYE SIFA ZAIDI YA KIUMBE CHOCHOTE. NA NDIO MAANA KAMWAMBIA TAJIRI HUYU, KWAMBA USINIITE MWEMA ALIYEKUWA MWEMA NI MWENYEZI MUNGU PEKE YAKE. AMBAE UFALME WA MBINGU NA ARDHI VIMO MKONONI MWAKE.
KISHA YESU AMETUNESHA KWAMBA ILI UWE MCHA MUNGU WA KWELI UNATAKIWA USIUE (VIFO VIMEZIDI, RWANDA, KENYA, KONGO, VIFO VYA WALEMAVU WA NGOZI VIMEKUWA CHAMBO CHA MATAJIRI, SUDANI, SOMALIA, AFGHANISTAN, IRAQ, ANGOLA, PHILIPINE……….N.K.),USIZINI (WANAUME KWA WANAUME, WATOTO WA ZINAA KIBAO NA VYOMBO VYENYE KUHAMASISHA ZINAA VINAONGEZEKA KILA KUKICHA, HADI KWA SASA NYUMBA ZA WAGENI NDIO MAKAO MAKUU YA KUSALITI NDOA NA UJIRANI), USIIBE( WIZI WA MABENKI NA MAJUMBANI UMEKUWA KAMA LIGI KUU, ROBA ZIMEZIDI MTAANI HADI WATU WANAOGOPANA NA KUOGOPA KULIZA MWENYEJI NJIA KWA KUKHOFIA KUITWA MWIZI NA KUCHOMWA MOTO KATIKA JINA LA MTU MBAYA), USISHUHUDI UONGO (CHANZO CHA VITA VYA IRAQ AMBAVYO VIMEANGAMIZA MAMILIONI YA WATU MPAKA SASA NI KUWA IRAQ ILIKUWA IKIMILIKI SILAHA ZA MAANGAMIZI, LAKINI SASA TUNAAMBIWA BAADA YAKUNYONGWA ADUI, KWAMBA VIONGOZI WA NCHI ZILIZO VAMIA WALIONGEA UONGO, ILI WAPITISHE AU KUFIKIA LENGO LA MAUWAJI YA WATU WASIOKUWA NA HATIA), USIDANGANYE (KUDANGANYA KUMNEKUWA NJIA MOJAWAPO YAKUTAFUTIA RIZIKI, UTAPELI WA CHENI NA FEDHA BANDIA, UHAKIKA WA KUJUWA CHANZO NA MAANA YA UGAIDI MPAKA SASA NI KIZA KISICHO NA UKWELI WA USHAHIDI KATIKA KILA KUNDI HUSIKA KATIKA VITA VYA UGAIDI ? NA MARANYINGINE TUNASHINDWA KUJUWA TAFAUTI YA UISLAMU NA UGAIDI NI NINI ? AU AU VITA VYA WAISLAMU NA WALE WASIOKUWA WAISLAMU VILIANZA LINI NA NI NINI SABABU ?), MHESHIMU BABA YAKO NA MAMA YAKO(BAADHI YA WAZAZI WALIOWENGI WANAHANGAIKA KILA KUKICHA ILI WAWEZE KUWATULIZA WATOTO WAO KATIKA TABIA NJEMA NA MUELEKEO WA KUJIANDAA NA NDO LAKINI MWISHO WAYOTE VIJANA HUONA WAZAZI WAO NI WATU WAKUWAPOTEZEA MDA, NA MARANYINGINE WATOTO HUWAPA WAZAZI WAO MAJINA YA DINGI AU MZUSHI AU MNENE……………..WAKINA MAMA WAO HUKOSA KAULI YA KUZUIA MATOAKEO KAMA MIMBA NA WIZI).

• YOTE HAYA HUYO JAMAA TAJIRI ALIWEZA KUYAEPUKA NA KUYASHINDA, LAKINI ALISHINDWA KUFAULU, KATIKA MTIHANI WA FEDHA NA MALI.
IKIWA BAADHI YA BINAADAMU, HAWATAKI KUWA SAWA NA WATUMWA WAO AU WAFANYAKAZI WAO AU NDUGU ZAO AU MARAFIKI WAO AU JAMAAZAO, VIPI WAMFANYE MWENYEZI MUNGU SAWA NA WAJA(VIUMBE AU BINAADAMU, MAJINI NA MALAIKA) ?
HUWEZI KUFIKIA WEMA MPAKA UTOE UNACHOKIPENDA ZAIDI, KATIKA NJIA YA HALALI.
QURAN :
MWENYEZI MUNGU ANASEMA » NA MWENYEZI MUNGU AMEWAFADHILISHA BAADHI YENU KULIKO WENGINE KATIKA RIZIKI. NA WALE WALIOFADHILISHWA HAWARUDISHI (HAWAWAGAWII) RIZIKI ZAO KWA WALE ILIOWATAMALAKI MIKONO YAO YA KULIA (WATUMWA), ILI WAWE SAWA KATIKA RIZIKI HII ; (BASI VIPI NINYI MNAMFANYA MWENYEZI MUNGU SAWA NA WAJA WAKE, NA NYINYI HAMKUBALI KUWA SAWA NA WATUMWA WENU) ? BASI JE, WANAZIKATAA NEEMA ZA MWENYEZI MUNGU ? »
(16 :71)
LICHA YA WATU WENGI WENYE UWEZO WA KIFEDHA NA MALI, KUJIFANYA KWAMBA WAO NDIO WENYE KUGOMBANIA HAKI ZA BINAADAMU, NA KUTAKA USAWA WENYE MFUMO WA UADILIFU KATIKA UMILIKAJI, UTENDAJI NA MSINGI WA ELIMU KATIKA JAMII, MARANYINGINE HUSHINDWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MATENDO NA KUSHINDA KATIKA MSINGI WA MANENO YENYE KUTA(WALL) ZA KUTIANA MOYO WA MAFANIKIO.
UTAWAKUTA WATU WENYE ELIMU NA NI MATAJIRI, WAKIJIGAMBA KWAMBA WAO NI WACHA MUNGU AU WANATETEA HAKI ZA WANYONGE AU NI WAADILIFU KATIKA MANENO YAO YA AHADI NA MATENDO YAO, LAKINI MWISHO WASIKU UDHAIFU WAO, UTAJITOKEZA AU UTAUTAMBUA KUPITIA ALAMA ZA MAPITO YAKE (JE ! ALIVYO ZUNGUMZA NDIVYO ATENDAVYO ?).
INAKUWAJE WEWE, UFIKIE CHEO CHA UTAJIRI NA KUITWA TAJIRI, PINDI AMBAPO HUJAFAURU KUARIDHISHA KIMAHITAJI WATU WAKO WA KARIBU.

BIBLIA
YESU AKAWATAZAMA WANAFUNZI WAKE, JINSI ITAKAVYOKUWA SHIDA WENYE MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU !
WANAFUNZI WAKASHANGAA KWA MANENO YAKE. YESU AKAJIBU TENA, AKAWAAMBIA, WATOTO, JINSI ILIVYO SHIDA WENYE KUTEGEMEA MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU! NI RAHISI NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU YA SINDANO KULIKO TAJIRI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU. NAO WAKASHANGAA MNO, WAKIMWAMBIA, NI NANI, BASI, AWEZAYE KUOKOKA? YESU AKAWAKAZIA MACHO AKASEMA, KWA WANADAMU HAIWEZEKANI, BALI KWA MUNGU SIVYO; MAANA YOTE YAWEZEKANA KWA MUNGU.
(MARKO MTAKATIFU 10:23………27)
KUNA WATU WENGI WENYE KUJIGAMBA KWAMBA NI MATAJIRI, LAKINI UKIANGALIA KHALI YA WAZAZI WAKE, MKE AU WAKE, NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI, UTASHANGAA KUHUSU MAANA YAJINA ALILOPEWA MTU HUYO. MTU ANAITWA TAJIRI ( PAPA AU PEDEJE…N.K) LAKINI ANASHINDWA KUDHAMINI CHAKULA CHA WIKI AU MWEZI AU MWAKA KATIKA KITUO FULANI CHA WATOTO YA TIMA AU KUWAPA MITAJI WAJANE AU MASIKINI, HILI NIJAMBO LAKUSHANGAZA KUHUSU UTAJIRI WENYE SIFA YA HEWA MAISHANI.
MARANYINGINE MTU ANAPEWA CHEO CHA UTAJIRI LAKINI KUMLIPA MFANYA KAZI WAKE WA NDANI MSHAHARA WENYE NAFUU YA MAISHA, ANAONA TABU SANA.
NA MARANYINGINE MTU HUSIKA HUITWA TAJIRI, LAKINI UKIANGALIA MAZINGIRA YA KULA NA KUNYWA NYUMBANI KWAKE, NIYENYE WASI WASI NA YENYE HESABU YA HALI YA JUU. UTAKUTA BABA NDIO MWENYE KURUHUSIWA KUNYWA CHAI YA MAZIWA AU KULA NYAMA MARA SABA KWA WIKI, NA WENGINE NI KUNYWA CHAI YA RANGI KATIKA MFUMO WENYE MPANGILIO WA HESABU YA VIJIKO VYA SUKARI NA MARANYINGINE HULA NYAMA KWA MAKADILIO YA VIPANDE.
MAVAZI YA MTUMBA NA UPATIKANAJI WAKE UPO KATIKA MSINGI WA MAOMBI YA HALI YA JUU, WASIWASI KATIKA KUTOA MAONI AU KUOMBA MSAADA, NA MARANYINGINE UTAMKUTA MFANYAKAZI WA NDANI AKIFANYWA WA MWISHO KULA, NA MARANYINGINE AKILISHWA CHAKULA KILICHOBAKI MEZANI. INA MAANA CHAKULA KIKIISHA MFANYA KAZI HUYO, HANA CHAKULA KWA WAKATI HUO, LICHA YA KUWA YEYE NDIE MPISHI.
MARANYINGINE MATAJIRI WA MWILI HUOGOPA KUSALIMIANA NA WATU MASIKINI, KWA KUOGOPA KUOMBWA (KUPIGWA MZINGA), NA MARANYINGINE WATU MATAJIRI HUJIJENGEA NIDHAMU YA KUOGOPWA NA WATU WENYE KHALI YA CHINI.
WATU MATAJIRI MARANYINGI HUJIJENGEA NGOME YA ULINZI KATIKA MFUMO WA DHARAU NA KIBURI, NA MSINGI WAO KATIKA UTENDAJI HUWA NA NJIA NYINGI ZA KUJIEPUSHA KUKAA KARIBU NA WATU WENYE UPUNGUFU WA PESA AU MALI.
MATAJIRI WALIO WENGI HUJIFANYA WAZURI KATIKA JAMII, PINDI WANAPOKUWA KATIKA MAZINGIRA YENYE KUONEKANA(TV NA VIKAO) NA KUSIKIKA(RADIO AU KATIKA MFUMO WA AHADI YENYE KUHITAJI NGUVU YA MASIKINI)SANA.

ASILIMIA KUBWA YA MATAJIRI, NI WATU WENYE KUOGOPA
(GHOFU)KUFIRISIKA, NA NI WENYE KUOGOPA UMASIKINI ZAIDI YA MWENYEZI MUNGU, NA NIWENYE KUOGOPA KUTOA (MALI, PESA, WAKATI AU MDA….N.K.), KUELEKEA KATIKA KAMBI YA MASIKINI NA MAFUKARA NA MAYATIMA NA WAJANE, LICHA YAKUWA NI WATU WENYE KUVAA KOFIA YENYE KIMVURI CHA UCHA MUNGU AU KUTEMBEA NA MBENDERA YA KUTETE HAKI ZA BINAADAMU.
MFANO HAI NI HUU WA SIERRA LEONE:

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KUTETEA HAKI ZA BINAADAMU LA AMNESTY INTERNATIONAL, 23.09.09 LILISEMA MWANAMKE MMOJA KATI YA WANANE NCHINI SIERRA LEONE YUKO KATIKA HATARI YA KUFA WAKATI WA KUJIFUNGUA. HALI HII INAIFANYA SIERRA LEONE KUWA MOJA YA NCHI ZENYE KIWANGO KIKUBWA CHA VIFO VYA KINA MAMA WAJAWAZITO DUNIANI.
AMNESTY INTERNATIONAL ILISEMA MAELFU YA WANAWAKE NCHINI HUMO WANAPOTEZA DAMU NYINGI BAADA YA KUJIFUNGUA KWA SABABU HAWAWEZI KUGHARAMIA MATIBABU KUTOKANA NA UMASIKINI.
MKUU WA SHIRIKA HILO, IRENE KHAN, ALIISHUTUMU SERIKALI NA FAMILIA ZA WANAWAKE HAO KWA KUPUUZIA HALI HIYO.




IKIWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU WALISEMA UONGO, KUHUSU UBAKHIRI WA MATAJIRI, BASI KWELI MATAJIRI WENGI WATAINGIA PEPONI.
NA IKIWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU WANASEMA UKWELI, MOJA WAPO AKIWA NI YESU (NABII ISA KWA WAISLAMU), BASI KUNDI KUBWA LA MATAJIRI LITAANGAMIA SANA SIKU YAKIAMA (SIKU YENYE KUBEBA MALIPO YA KILA KIUMBE NA KUMALIZA UHAI AU MAISHA YA KILA KIUMBE HAI, HAPA DUNIANI).

UBAGUZI WA SALAMU BAINA YA MATAJIRI NA MASIKINI
SIKU ZOTE BAADHI YA MATAJIRI, WANATUMIA KURA YA MAISHA KATIKA MSINGI WENYE MAMLAKA YA PESA NA MALI, ZAIDI KULIKO KUTUMIA MFUMO NA ASILI YA MWANADAMU WA KAWAIDA.
MAMLAKA YA PESA NA MALI INAMFANYA MTU MWENYE MALI, AMUONE YULE MWENYE UPUNGUFU WA MALI NA PESA, KAMA MTU DHAIFU, HATAKAMA MDHARAULIWA (MASIKINI), ANA ELIMU NZURI AU UMRI MKUBWA ZAIDI YAKE(TAJIRI). MAMLAKA HAYO YA PESA NA MALI, YANAMFANYA TAJIRI KUHISI KWAMBA, HANA UPINZANI KATIKA MAONGEZI NA MATENDO.
KWA NJIA HII, THAMANI YA UKUBWA KATIKA NJIA YA UMRI, IMEKUWA DHAIFU NA INAPOTEA KABISA, KWASABABU, MZEE ANAMWITA MTOTO MDOGO BWANA MKUBWA, BABA, MHESHIMIWA, SIFA ZOTE HIZO HUWA NA MSINGI WA KUOMBA KATIKA UNYENYEKEVU WA HALI YA JUU. NA NJIA HII, YA WATOTO KUMILIKI PESA NA KUTOA KATIKA MFUMO WA SIFA, IMEWEZA AU KUFAULU KUVUNJA HESHIMA AU KUSHUSHA HADHI YA NAFSI YA BINAADAMU MWENYE UMRI NA HAKI WA KUHESHIMIWA NA YULE MWENYE UMRI MDOGO, BILA KUJALI MALI NA PESA.
NA ANAPOJITOKEZA MASIKINI KUPINGA MANENO YAKE(TAJIRI) AU VITENDO, HUPEWA (MASIKINI) ADHABU YA KUNYIMWA MSAADA AU KUTAFUTIWA SABABU YA KIFUNGO AU ADHABU NYINGINE YA KUMTIA ADABU (MTU MWENYE UPUNGUFU WA MALI NA PESA LAKINI ANAMKOSOA MTU AMBAE NI TAJIRI WA MALI NA PESA).AU MASIKINI AKINUSURIKA NA ADHABU HIZO, ATAPEWA JINA LA MASIKINI TAJIRI, AMBALO MAANA YAKE NI KUWA NA UTAJIRI NAFSINI
(UTAJIRI WA UADILIFU KATIKA MSINGI WA HAKI) NA KUWA MASIKINI WA MALI NA PESA.

MARANYINGINE, MATAJIRI HAWAPENDI KUWAPA WATU MASIKINI MKONO KATIKA MSINGI WA SALAMU, MATAJIRI HUOGOPA MARADHI KUTOKA KWENYE MIKONO YA WATU MASIKINI NA MAFUKARA NA MARANYINGINE, HUONA(MATAJIRI) KUPEANA MKONO NA MASIKINI, NI KUJISHUSHIA HADHI MBELE YA KUNDI LA MATAJIRI WENZAKE.
MARANYINGINE BAADHI YA WATU MATAJIRI HAWAPENDI KUWAKARIBISHA WATU MASIKINI, KATIKA NYUMBA ZAO AU SEHEMU YA KUKAA ( BARAZANI AU SEATING ROOM) KWASABABU, HUWA(MATAJIRI) NA DHANA YA KWAMBA MTU HUYO MASIKINI, ATAPUNGUZA THAMANI YA BARAZA KWA KUCHAFUA VITI AU KAPETI, AU MARANYINGINE BAADHI YA WATU WENYE UWEZO WANASHINDWA KUWAKARIBISHA WATU MASIKINI BARAZANI MWAO KWA KUGHOFIA KWAMBA MATAJIRI WENZAO WATAWAONA KWAMBA WAO NI MARAFIKI WA WATU WENYE KHALI YA CHINI KIUCHIMI AU KUSHINDWA KUWA KARIBISHA NDANI KWA SABABU BARAZANI MNA WAGENI MATAJIRI AU WATU FULANI MAARUFU.
YOTE HAYO NI MAPAMBANO AMBAYO MASIKINI WANAKABILIANA NAYO KATIKA MSINGI WA KUSAKA RIZIKI. NA NDIO MAANA MAKAO YA MASIKINI, HUITWA USWAHILINI AU USWAZI (YANI SEHEMU YENYE HADHI YA CHINI KATIKA KILA JAMBO)
MARANYINGINE NYUMBA ZA WATU MATAJIRI, ZINA VIKOMBE VYAKUNYWEA WATU WENYE GHADHI YA CHINI NA VIKOMBE NA MASAHANI VYA KUTUMIWA NA WATU WENYE GHADHI YA JUU.
NA MARANYINGINE WATU MATAJIRI WANA TABIA YA KUPEANA TAARIFA ZA SHEREHE KATIKA MSINGI WA UMWINYI NA KUPANGIANA KIASI KIKUBWA CHA MCHANGO. MARANYINGINE MASIKINI MWENYE KUJIPENDEKEZA ILI APEWE KADI YA HARUSI, INAMLAZIMU ACHANGIE HARUSI HUSIKA, KATIKA MFUMO WA KIASI KILICHOPANGIWA WATU WOTE, BILA KUJALI MASIKINI NA TAJIRI.
MCHANGO WA HARUSI HUSIKA UNAWEZA UKAWA KIASI FULANI CHA MTAJI WA MASIKINI.
YOTE HAYO YAMETUZUNGUUKA NA KILA MMOJA ANAUWEZO WA KUYASHUHUDIA AU KUYASIKA KWA WATU AU KWENYE VYOMBO VYA HABARI.
NDIO MAANA TUNAWASIKIA WAHENGA WAKISEMA HIVI « MTAJI WA MASIKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE »
JE ! IKIWA YOTE HAYO, YANATENDWA NA BAADHI YA BINADAMU KUWATENDEA BINADAMU WENZAO.
ITAKUWAJE WATU WAMFANANISHE MTU FULANI AU KIUMBE FULANI NA MWENYEZI MUNGU. MUNGU HANA TABIA YA DHULMA, DHARAU, CHUKI, LAWAMA……JUU YA VIUMBE WAKE. KWASABABU KILA JAMBO MAISHANI LIMEUMBWA KWA REHEMA NA UWEZO WAKE.
UTAKUTA KATIKA WAPINGAJI UBAGUZI WARANGI NA KIKABILA, WAMO MATAJIRI, LAKINI WENGI WETU NI WANAFIKI WENYE MSINGI WA KUHITAJI SIFA KATIKA JAMII. KUNA NDUGU ZETU WENYE ULEMAVU WA NGOZI(ALBINO), KWA SASA WANAWINDWA KAMA SWALA PORINI, JE NINANI WA KUWATETEA KATIKA MSINGI WA AMANI ?
NI MASIKINI WENZAO AU NIMATAJIRI WENYE KUHITAJI NYONGEZA YA MALI NA PESA KATIKA HARAKATI YAO YA KUNUNUA VIUNGO VYA BINAADAMU WENZAO KWA GHARAMA YA JUU KABISA.
KWASASA HATA WACHUNGAJI WAMEANZA KUINGIA KATIKA BIASHARA YA VIUNGO VYA BINADAMU. JE ! WATU WENYE ULEMAVU WATAWEZA KUMTAMBUA MUNGU NA KUHESHIMU AMRI ZAKE, KATIKA KHALI YA KUSAKWA NA WAKUU WAO WA IMANI ?
INAKUWAJE BABA AWEZE KUMUANGAMIZA MKE WAKE AU MWANAE KATIKA JINA LA KUSAKA MOTO WA UTAJIRI WA DUNIA HII ?
MFANO HAI WA MAUAJI YA ALBINO NI HUU :
WATATU KUNYONGWA KWA MAUAJI YA ALBINO ????!!!!!
MAHAKAMA KUU YA TANZANIA, LEO 23.09.09 IMEWAHUKUMU WATUHUMIWA WATATU WA NAUAJI YA ALBINO KUNYONGWA HADI KUFA BAADA YA KUPATIKANA NA HATIA YA KUMUUA MTOTO MATATIZO DUNIA MWENYE UMRI WA MIAKA (13). WALIHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA NA MAHAKAMA HIYO MJINI KAHAMA, MKOANI SHINYANGA NI MASUMBUKO MATATA (32), MKAZI WA ITUNGA, EMANUEL MASANGWA (28), MKAZI WA BUNYIHUNA NA CHARLES KALAMUJI AU CHALES MASANGWA (42) MKAZI WA KIJIJI CHA NANDA WILAYANI BUKOMBE. WOTE WALIPATIKANA NA KOSA LA MAUAJI KINYUME CHA SHERIA YA JINAI YA MAKOSA NAMBA 196 SURA YA 16 ILIYOFANYIWA MAREKEBISHO YA MWAKA 2002.


YOTE HAYO NI MABADILIKO YA KUMUACHA MUNGU KATIKA JINA LA UTANDAWAZI NA UKUTA WENYE MLANGO AMBAO UNA ALAMA ISEMAYO KWAMBA « YA MUNGU YALIISHAPITWA NA WAKATI. »
KWA UPANDE WA MATAJIRI WENYE KUMJUA MUNGU, WAO HUWA NA TABIA MBILI, AMBAZO NI KUTUMIA MFUMO WA ASILI. KUMJALI NA KUMHESHIMU MTU YOYOTE BILA KUJALI MALI, PESA, UMRI…………KATIKA MFUMO WA UADILIFU. NA HUWASAIDIA MASIKINI, MAYATIMA, MAFUKARA, WATUMWA……………..NA HUTOA ZAKA NA SADAKA KWA WAKATI WAKE. NA KATIKA MARAFIKIZAO UTAKUTA MNA MCHANGANYIKO WA MASIKINI NA MATAJIRI, WEUPE NA WEUSI AU WAFUPI NA WANENE AU WEMBAMBA NA WANENE. NA HAO MATAJIRI WENYE TABIA NJEMA KAMA HIZI, NDIO WATAKAORITHI UFALME WA MBINGU, NA MALIZAO ZITALINDWA DUNIANI NA WATAPATA MALIPO YA PEPO SIKU YA KIAMA. INSHALLAH (MUNGU AKIPENDA)

MTAYARISHAJI NI: ISMAIL MUSSA