NJOMBE

NJOMBE

Thursday, February 2, 2012

Mbunge ahoji Bodi ya Mikopo kupewa fedha nyingi


MBUNGE wa Viti Maalumu, Christowaja Mtinda (CHADEMA), amehoji sababu za serikali kutoa fedha nyingi kwa Bodi ya Mikopo ya Vyuo vya Elimu ya Juu wakati wa kipindi cha Uchaguzi Mkuu. Mbunge huyo alisema wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu serikali imetoa fedha nyingi kwa Bodi ya Mikopo, wakati ambao hakuna uchaguzi pesa zinapungua.
Kutokana na hali hiyo, Mtinda alitaka kujua ni kuna uwiano gani wa kimapato na kwanini mikopo ya wanafuzi wa vyuo isipitie moja kwa moja kwenye akauti zao badala ya akauti za vyuo ambazo hutumiwa vibaya na wahasibu kwa kutumia majina feki.
Akijibu swali hilo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema si kweli kuwa mapato ya serikali yanapanda wakati wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha fedha nyingi kupelekwa katika Bodi ya Mikopo.
Kawambwa alisema serikali inapeleka fedha kwenye Bodi ya Mikopo kulingana na mapato yaliyopo na wala si kutegemea kipindi cha uchaguzi kama alivyosema mbunge huyo.
Alidai kuwa serikali haitabadilisha msimamo wake wa kutuma fedha katika vyuo kwani kwa kufanya hivyo kutapunguza hali ya kutuma fedha kwenye akaunti ya mwanafunzi ambaye aliacha masomo muda mrefu.
Hata hivyo Dk.Kawamba alisema kuwa serikali itahakikisha inasimamia vema fedha hizo ili zitumike kwa makusudi tarajali na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment