NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, February 1, 2012

Feza za rada Bil.18/- kununua madawati

Kutoka Bungeni Dodoma

SERIKALI imesema sh 18.4 bilioni kutoka katika fedha zilizorudishwa za rada zitanunua madawati kwa shule za msingi na sekondani nchini.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI-Elimu) Kassim Majaliwa wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum Martha Mlata (CCM).
Mlata alitaka ufafanuzi ni kiasi gani cha fedha kilichotengwa kutokana na fedha za rada kitakachotumika kupunguza tatizo la madawati kwa shule nyingi nchini.
Awali katika swali la msingi, Mbunge wa Musoma Mjini Vicent Nyerere (CHADEMA) alitaka kujua serikali imejipanga vipi kukabiliana na upungufu wa madawati kwa shule zote nchini.
Naibu Waziri alisema mwaka wa fedha 2009/10 serikali ilitoa kiasi cha sh bilioni moja kwenda katika mamlaka za serikali za Mitaa kwa ajili ya ununuzi wa madawati kwa shule za sekondari.
Mwaka 2010/11 serikali ilitoa tena sh bilioni tatu kwa ajili ya kununua madawati kwa shule za msingi kwa utaratibu wa kupeleka fedha kwenye halmshauri.
Hata hivyo alisema walimu wakuu wa shule nchini wamepewa mamlaka ya kutumia fedha zinazotengwa kufanyia ukarabati madawati yanayoharibika.
Kwa upande wake Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Mkuchika alisema kuwa serikali iko mbioni kukamilisha waraka utakaosambazwa na Waziri Mkuu nchi nzima kuelezea kuwa huu ni mwaka wa kumaliza tatizo la madawati kwa shule zote.

No comments:

Post a Comment