NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, February 1, 2012

Mbunge CCM ahoji mshtaki kumhudumia mshtakiwa

MBUNGE wa Viti Maalumu Agnes Hokololo (CCM) jana aliitaka serikali kutoa ufafanuzi kuhusu washtaki kuendelea uwahudumia washtakiwa wao.
Mbunge huyo alitaka kujua hali hiyo kutokana na kile alichokieleza kuwa ni usumbufu na baadhi ya watu wanashindwa kuwapeleka watu mahakamani kuhofia gharama hizo.
“Hivi hii serikali haioni kuwa kumhudumia mshtakiwa kwa kutumia gharama za mshtaki wake unakuwa ni mzigo?’’ alihoji mbunge huyo.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Balozi Khamis Kagasheki alikiri kuwa utaratibu huo upo kwa muda mrefu na kusema serikali inautazama kwa karibu sasa.
Hata hivyo katika hali ya kawadia Kagasheki alisema hata yeye hana majibu ya kama utaratibu huo ni sahihi au si sahihi lakini anachojua ni kwamba ulikuwepo tangu mwanzo.
Kuhusu kuunga mkono juhudi za wananchi katika ujenzi wa vituo vya polisi kila kata, Balozi Kagasheki alisema ni mpango wa serikali katika kuimarisha ulinzi.

No comments:

Post a Comment