NJOMBE

NJOMBE

Thursday, April 12, 2012

Safari ya Simba Es Setif,Licha ya mambo yote Simba hawakukata tamaa


Kwikwi husababishwa na nini?

Baada ya kusoma makala inayohusu kijana mmoja aliyesumbuliwa na kwikwi kwa zaidi ya miaka miwili na nusu, na baadaye kutibiwa tatizo hilo kwa kufanyiwa upasuaji wa ubongo na kutolewa tezi, nimeamua leo nizungumzie kwikwi.
Kwiki ni kitendo kisichozuilika ambacho hutokana na kusinyaa kwa kuta za kiwambo cha moyo au diaphragm. Kwa kawaida kwikwi ni kitendo kinachojirudia rudia mara nyingi. Sauti ya 'hic' inayotokea wakati unapokuwa na kwikwi husababishwa na kidaka tonge (epiglottis) ambacho hufunga haraka wakati hewa inapoingia kwenye koo. Kupiga kwikwi kwa kawaida hakuna maumivu lakini mara nyingine husumbua hasa inapoendelea kwa muda mrefu. Kwikwi ya kawaida huweza kutulizwa kwa kunywa maji, lakini wakati mwingine kufanya hivyo hakusaidii.
Zifutazo ni sababu zinazoweza kukuletea kwikwi
1. Kula kwa haraka.
2. Kula chakula cha moto na kunywa maji baridi baada yake.
3. Kulia au kukasirika.
4. Kula chakula chenye viungo vingi au pilipili.
5. Kula chakula cha moto sana.
6. Kunywa pombe au soda kwa wingi.
7. Kukohoa sana.
8. Kucheka kupita kiasi.
9. Kufurahi sana, kusisimka au kupatwa na msituko.
Kwa ujumla tunaweza kusema kuwa, vitu ambavyo vinakiletea karaha kiwambo cha moyo au diaphragm husababisha kwikwi. Kuna sababu nyingi ambazo husababisha jambo hilo na hizo tulizotaja hapo juu ni miongoni mwazo,ambapo matokeo yake ni humfanya mtu apige kwikwi. Kwikwi kwa kawaida huisha baada ya dakika chache au hata sekunde. Lakini iwapo kwikwi itaendelea kwa masaa au kwa siku, huweza kuwa ni tatizo muhimu la kitiba na pengine hali kama hiyo inaweza ikawa inasababiswa na ugonjwa.
Kuna baadhi ya watu hupata kwikwi sana wakati wa ujauzito, baada ya kufanyiwa operesheni na hata watoto wachanga pia hupatwa na kwikwi mara kwa mara. Wajawazito hupata kwikwi sana mwishoni mwa miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito na mwanzoni mwa miezi mitatu ya pili. Kwikwi hutokea wakati wa ujauzito ni kwa sababu wakati huo uwezo wa kuvuta hewa ndani ya mapafu na kutoa nje huongezeka kwa asilimia 30 hadi 40 ikilinganishwa na hali ya kawaida. Hakuna sababu inayojulikana inayosababisha kwikwi kwa watoto wachanga, na wazazi wanashauriwa wasitiwe hofu na suala hilo. Hii ni katika hali ambayo kwikwi baada ya upasuaji husababishwa na nusu kaputi au anesthesia.

Wednesday, April 11, 2012

Jamani Jamani, "Mafuriko Tena Dar"

Baada ya mvua kunyesha kwa wingu tena siku ya leo jijini Dar es salaam na maeneo mengine kama Morogoro.Imezuwa wawazo tena kwa watu wanaoishi maeneo ya mabondeni.Mvua hii imenyesha kwa takribani masaa matano mapaka hivi sasa ilipotuma habari hii basi mvua hiyo inaendelea.Mvua hii imeanza majira ya saa 12:00 mchana mapaka hivi sasa.Mbali na hilo jingine na hatari ya kuwa na Sunami kubwa katika nchi zote zilizokatika mwambao wa bahari ya hindi ikiwemo Tanzania na eneo kubwa linalo hofiwa ni Dar es salaam.





Mvua kubwa inanyesha na tayari maji yamejaa.Hapa ni Temeke hospitali na sijui ndugu zetu wa mabondeni hali itakuwaje.Mara mjadala utaanza tena wahame wasihame?
Picha na Mjengwa

Safari ya mwisho ya Kanumba

MAELFU WAJITOKEZA KUMZIKA, WATU 600 WAPOTEZA FAHAMU, POLISI WASEMA HAWAKUTARAJIA UMATI MKUBWA HIVYO

MAELFU ya waombolezaji jana walijitokeza katika mazishi ya msanii nguli wa filamu Tanzania Steven Kanumba (28), yaliyofanyika katika Makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumamosi ya Aprili 7, mwaka huu.Kabla ya kuzikwa, mwili wa marehemu Kanumba ulipelekwa katika Viwanja vya Leaders ili kuwawezesha waombolezaji kutoa heshima za mwisho. Hata hivyo, ni wachache waliobahatika kupata fursa hizo baada ya kutokea msongamano mkubwa ulioifanya kamati ya maandalizi ya mazishi hayo kusitisha mchakato huo.

Inakadiriwa kuwa waombolezaji wapatao 600 walianguka kutokana na ama msongamano au majonzi ya kifo hicho cha ghafla cha msanii huyo.

Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Mke wa Rais, Salma Kikwete na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe walikuwa wa kwanza kutoa heshima zao za mwisho na kufuatiwa na viongozi wengine wakiwamo wabunge.

Baada ya viongozi hao kutoa heshima zao za mwisho, Dk Bilal na Mama Kikwete waliondoka na kwa mujibu wa ratiba, ilikuwa zamu ya waombolezaji wengine kuaga.

Hata hivyo, kulitokea msongamano mkubwa wa watu kila mmoja akitaka kulifikia jeneza na kulishika. Ilibidi vyombo usalama na walinzi binafsi kufanya kazi ya ziada kurejesha hali ya utulivu katika eneo hilo.

Kutokana na utaratibu mbovu katika kuendesha shughuli hiyo, ratiba ilikatishwa na mwili kuondolewa saa 6:30 kupelekwa makaburini. Kwa mujibu wa ratiba ya mazishi iliyokuwa imetolewa juzi, muda wa kuaga ulipangwa kuanza saa 6:00 hadi saa 9:00 alasiri.

Badala yake, waombolezaji walitakiwa kujipanga kando ya Barabara ya Tunisia ambako gari lililobeba mwili wa msanii huyo lilipita kuelekea makaburini.

Haikuwa kazi rahisi kwa waombolezaji hao ambao baadhi walifika hapo alfajiri kwa ajili ya kutoa heshima zao mwisho kukubaliana na agizo hilo.

“Hatuwaelewi hawa. Sisi hatukuja kuliona jeneza tunataka kumuona ili tujue kama kweli amekufa. Hawa walioandaa utaratibu huu mbovu ni kina nani jamani au wameshindwa kazi?” alisema mmoja wa waombolezaji na kisha kuangua kilio.

Baada ya hali kutulia umati huo wa waombolezaji ulianza kulisindikiza gari la marehemu kwa nyuma huku wengine wakitaka jeneza hilo lishushwe ili walibebe.

Wakati msafara huo ukielekea makaburini, baadhi ya waombolezaji walikuwa wakianguka na wengine kuzirai baada ya kuona jeneza na kuwafanya watoa huduma wa Msalaba Mwekundu kufanya kazi kubwa ya kuwasaidia na kuwapeleka baadhi yao hospitali.

Licha ya umbali kati ya Viwanja vya Leaders na Makaburi hayo ya Kinondoni kuwa karibu, msafara huo ulichukua takriban saa mbili kufika kutokana na kwenda taratibu ili kutoa fursa kwa waombolezaji ambao baadhi yao walilazimika kupanda juu ya miti, kutoa heshima zao.

Baada ya kufika makaburini, iliwalazimu polisi kuongeza nguvu kudhibiti umati huo na kutoa fursa kwa ibada ya mazishi kuendeshwa kama ilivyopangwa.

Wazirai

Mwenyekiti wa Kamati ya Tiba ya mazishi hayo, Dk Nassoro Ally alisema watu wapatao 600 walizirai katika viwango tofauti kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ya watu kujaa na kubanana na hivyo kukosa hewa.

“Watu wamebanana na kukanyagana. Wemekosa hewa na wengine kati yao wanakabiliwa na matatazo ya kiafya, ugonjwa wa pumu, shinikizo la damu ingawa wapo waliokanyagana na kuanguka kutoka katika miti na kupoteza fahamu,” alisema Dk Ally.

Baadhi ya waombolezaji waliozirai ni pamoja na wasanii Wema Sepetu, Jacqueline Wolper na Irene Uwoya.

Wema alizirai baada ya kufika makaburini na Wolper alifikwa na hali hiyo katika Viwanja vya Leaders.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema watu waliopoteza fahamu hawazidi 30.

Alisema watu waliofika kuaga mwili huo walikuwa ni zaidi ya matarajio yao na kuongeza kwamba kwa mazingira shughuli hiyo, eneo hilo lilikuwa dogo akisema sehemu muafaka ilipaswa kuwa Uwanja wa Taifa.

Kauli za viongozi
Akitoa salamu kwa niaba ya Serikali, Dk Nchimbi alisema huu ni mwaka wa mwisho kwa wasanii kuibiwa kazi zao.
Dk Nchimbi ambaye katika salamu zake pia alitoa ubani wa Sh10milioni kwa niaba ya Serikali, alisema wizara yake ikishirikiana na Wizara ya Fedha, Wizara ya Kazi na Ajira na Shirikisho la Filamu Tanzania (Taff), wameshakutana na kujadiliana namna ya kuzuia wizi katika kazi za wasanii.

“Mwaka huu ndiyo mwisho wa kazi za wasanii kuibiwa na nilipenda sana kuona Kanumba akishuhudia jitihada hizi ambazo tumekuwa tukizifanya naye kama mdau mkubwa wa sekta hii,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:

“Jitihada ambazo amezifanya Kanumba enzi za uhai wake ni dhahiri zimejionyesha leo. Mmejitokeza kwa wingi kuja kumuaga hivyo wasanii mnaobaki mnatakiwa kuiga kile alichokuwa akikifanya.”

Rais wa Taff, Simon Mwakifwamba alisema marehemu Kanumba ameacha pengo kubwa katika tasnia ya filamu kutokana na mchango wake mkubwa aliouonyesha katika kipindi kifupi cha uhai wake.

“Kanumba alikuwa balozi pekee wa filamu nchi za nje. Aliitangaza nchi yetu kupitia tasnia ya filamu hivyo tutamkumba daima kwa kutuonyesha njia,” alisema Mwakifwamba.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amewataka wasanii nchini kufuata nyayo za Kanumba na kumkumbuka msanii huyo milele.

“Watanzania wengi wana majonzi makubwa lakini watambue kwamba ni kazi ya Mungu. Kinachotakiwa sasa hili litumike kama somo kwa wasanii wengine kwani leo tunashuhudia Kanumba akiagwa kama mfalme kutokana na kazi yake nzuri aliyokuwa anaiwasilisha kwa Watanzania,” alisema Nape.

Askofu wa Kanisa la African Inland Church (AIC), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Charles Salala alisema msiba wa Kanumba ni pigo kwa taifa na kuwaasa Watanzania kutenda mambo mema ili kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii.

“Leo tupo katika msiba wa mtu ambaye alikuwa ana mchango mkubwa kwa jamii, ndiyo maana tunashuhudia umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika hapa, lakini jambo ambalo sisi kama binadamu tunatakiwa kufanya ni kuishi maisha mema na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu ,” alisema na kuongeza:

“Marehemu Kanumba aliwahi kuhudumu katika kanisa hili na alikuwa ni mtu mwenye upendo kwa kila mtu ndiyo maana leo maelfu ya Watanzania tupo hapa kumsindikiza ndugu yetu katika safari yake ya mwisho.”
Habari na Mwananchi,Video na Dj Choka.

Alichoeleza Lulu polisi hiki hapa

MSANII Elizabeth Michael (Lulu), ameiambia polisi
kuwa kifo cha Steven Kanumba kimetokana na ugonvi kati yao, huku taarifa nyingine zikieleza kuwa huenda Lulu akafikishwa mahakamani leo.

Habari zilizopatikana jana kutoka Kituo cha Polisi Oysterbay zilieleza kuwa, Lulu alisema kuwa kulitokea ugomvi kati yake na Kanumba baada yeye kuzungumza na simu
kutoka kwa mtu maarufu anayetajwa kuwa mpenzi wake.

"Lulu alisema kuwa ugomvi ulitokana na simu aliyopigiwa na mpenzi wake mwingine, ambaye ni mtu maarufu nchini, ndipo
Kanumba akamfokea na ndiyo ugomvi ukaanzia hapo," chanzo hicho kimesema.

Chanzo hicho kiliongeza kuwa baada ya Kanumba kuanguka, Lulu alitoka nje na kuondoka kwa gari lake hadi maeneo ya Coco Beach, lakini baadaye daktari wa Kanumba alimpigia simu akimtaka arudi ili wampeleke hospitali.

"Alipororudi Sinza ndipo akakamatwa, lakini walikuja Kituo cha Polisi Oysterbay kuchukua PF3," kilisema chanzo hicho.

Chanzo kiliongeza kuwa tangu Lulu alipofikishwa kituoni hapo amekuwa mtulivu asiye na wasiwasi wowote hata katika mahojiano na polisi.

Katika hatua nyingine, Polisi wa kituo hicho jana walipata wakati mgumu baada ya kuibuka kundi la vijana waliotokea makaburi ya Kinondoni kumzika Kanumba, walioandamana wakidai wanamtaka Lulu.

"Tunataka jembe letu", waliimba vijana hao waliofikia 100 wakitokea Barabara ya Ali Hassan Mwinyi huku wakishika majani na kufanya askari waliokuwapo kituoni hapo kuwahi kuchukua silaha na mabomu ya machozi kujiandaa kutuliza ghasia kama zingezuka.

Hata hivyo vijana hao walitawanyika baada ya kuona askari wakiwa tayari kupambana nao na kukimbia maeneo mbalimbali.
Katika hatua nyingine Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa,
Msanii Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu huenda akafikishwa mahakamani leo kujibu tuhuma za kuhusika na kifo cha Steven Kanumba.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela aliliambia gazeti hili jana kuwa Lulu atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni mara baada ya polisi kupata ripoti ya vipimo kutoka Mkemea mkuu wa Serikali.

“Tunasubiri ripoti ya Mkemia Mkuu kubaini chanzo cha kifo hicho kwa sababu wamechukua baadhi ya sampuli za marehemu kwenda kupima na kwamba tutakabidhiwa leo(jana). Kimsingi tukipata tu taarifa hiyo tutamfikisha mahakamani,” alisema Kenyela.

Aliongeza ripoti hiyo itaweza kuwasaidia kuandika mashtaka ili yaweze kufikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kumfikisha mahakamani.

Kamanda Kenyela alisema kuwa, ripoti ya madaktari imewasilishwa juzi na kwamba imeonyesha kuwa Kanumba amefariki kwa ugonjwa wa mtikisiko wa ubongo.

Msanii Stephen Kanumba alifariki usiku wa Ijumaa Kuu
Chanzo Mwananchi.

Tuesday, April 10, 2012

LIVE KUTOKA KINONDONI MAKABURINI KWENYE MAZISHI YA STEVEN KANUMBA

Matukio na Picha Na Dj Choka

Hii ni barabara ya Kinondoni kuingia kwenye makaburi ya Kinondoni ilikuwa ni balaaaa yani dah, kule mbele ndio mwili wa marehemu Steven Kanumba ndio unakuja

 Kwa wingi wa watu ilibidi watu wapande juu ya miti lakini baadae waliamuriwa washuke chini na kamanda Kova

 Ray akiwa aamini kama swaiba wake ndio anakwenda kwenye nyumba yake ya milele

 Charlz Baba akiwa na wenzake kutoka Mashujaa Band, Charz ameniambia walikuwa wanatokea Morogoro so waliweza kuwahi makaburini

Kauli ya Mwisho ya Kanumba Kwa Wasanii wenzake

Hii ya pili ni kauli ya mama yake mzazi baada ya kupata habari za Msiba wa mwanae kipenzi Steven Kanumba

LIVE KUTOKA LEADERS KUMUAGA KANUMBA

 Hawa watoto wanaopita ndio watoto waliokuwa wakicheza movie na marehemu Kanumba enzi ya uhai wake

 Mama yake Kanumba aliyenyoosha mkono juu kuwapungia watu waliokuja uwanjani

 Huyu dada hapa mbele alikuwa akilia kwa uchungu sana hadi nilikuwa namuonea huruma

 Hemed na Yusuph Mlela wakiingia

Makamu wa rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali 

 Mke wa rais Mama Salma Kikwete

Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi akitoa heshima zake za mwisho kwenye mwili wa marehem.
Picha na Matukio na Dj Choka

Daktari aeleza kilichomwua Kanumba

Marehemu Kanumba




NI BAADA YA JOPO LA MADAKTARI MUHIMBILI KUMFANYIA UCHUNGUZI, BABA YAKE AZUNGUMZA, WABUNGE WAMLILIA
Florence Majani na Suzzy Butondo
MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza. Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion,” alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) “Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka” alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo  wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

“Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.”

“Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.”

Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo.

Baba mzazi azungumza Baba mzazi wa mwigizaji huyo, Charles Musekwa Kanumba alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mwanawe Jumamosi saa 10:00 alfajiri baada ya kupigiwa simu na dada wa marehemu, Sara Kanumba.  “Sara aliniuliza: ‘Una taarifa yoyote kuhusu mwanao Kanumba?’ Nikamjibu kuwa sina taarifa yoyote, ndipo aliponieleza habari za kifo hicho. Aliniambia Kanumba hatupo naye tena amefariki kwa kuanguka, amekorofishana na mpenzi wake.”  alisema taarifa hizo zilimsababisha aishiwe nguvu kwa kuwa kilikuwa kifo cha ghafla… “Basi kuanzia hapo, nilianza kupigiwa simu za kupewa pole, ndipo nilipoamini kumbe mwanangu amefariki.”

 Akizungumzia kuchelewa kufika msibani, alisema kumetokana na tatizo la mawasiliano. Awali, alikuwa amepanga mtoto wake Kanumba akazikiwe Mwanza kwa babu yake ndiyo maana hakufika mapema msibani.   “Nilikuwa nimepanga apitishwe hapa kwangu Shinyanga aagwe, halafu tumpeleke Mwanza kwa babu yake kumzika huko lakini alipokuja mama yake alinishauri kuwa huko kutakuwa na nafasi ndogo kwa sababu watu ni wengi pia alikuwa na marafiki wengi, wengine wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo alinishawishi na tukakubaliana kumzika Dar es Salaam,” alisema.

Pia alikanusha uvumi kuwa hajafika msibani kwa kuwa walikuwa na ugomvi na marehemu akisema walishamaliza tofauti zao. Alisema anatarajia kufika leo usiku tayari kushiriki mazishi hayo.

Wabunge  kilio Jana, baadhi ya wabunge waliofika nyumbani kwa marehemu Kanumba waliangua vilio wakati walipotoa salamu zao za rambirambi.
Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata hakuzungumza na badala yake aliimba kipande cha wimbo uliozungumzia kifo na maneno ya wimbo huo yalionekana kuwagusa wafiwa na kusababisha vilio kuanza upya huku baadhi wakipoteza fahamu.
Mbunge mwingine, Neema Mwinyimgaya aliongeza majonzi masibani hapo alipounganisha msiba huo na wa mama yake… “Mama yangu amefariki miezi mitatu iliyopita, huko uliko mama, nakuomba umpokee kijana mwenzetu,” alisema mbunge huyo na kushindwa kuendelea.

Wabunge wengine waliohudhuria msiba huo ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Aboud Juma (Kibaha Vijijini), Mussa Azan Zungu (Ilala), Abbas Mtemvu (Temeke), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Ritha Kabati (Viti Maalumu).
 Kova na mchango wa Kanumba Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema anakumbuka mchango wa Kanumba katika kuzuia uhalifu jijini.

“Tulishirikiana naye pamoja na wasanii wengine kuandaa bonanza maalumu ambalo lilidhamiria kukabiliana na uhalifu hapa jijini na kwa kweli mchakato ule ulifanikiwa kwani uhalifu ulipungua kwa kiasi kikubwa” alisema Kova.
“Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno na nafikiri kujiweka tayari (kiimani) ni jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa makini nalo katika maisha yake,” alisema Kova.

Ratiba ya mazishi
2:30 - Msafara kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club.
3:30 - Misa ya kumuombea na salamu mbalimbali.
6:00 – Kuaga
9:00 - Kuelekea Makaburi ya Kinondoni kupitia Barabara ya Tunisia

SAHIHISHO
Rais Jakaya Kikwete jana alilazimika kubadili ratiba yake ya safari za ndani ya nchi ili kwenda kujumuika na waombolezaji wengine katika msiba wa msanii nguli, Steven Kanumba na hakuwa na safari nje ya nchi kama ilivyoripotiwa na gazeti hili jana. Mhariri
Habari na Mwananchi

LIVE KUTOKA LEADERS CLUB KWENYE MAZISHI YA STEVEN KANUMBA

Kinachosubiriwa kwa sasa ni mwili wa marehemu kuwasili eneo hili la Leaders Club. Nitakuwa najitaidi kuwawekea matukio kila baada ya nusu saa.
Matukio na Choka