NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, February 21, 2012

Maafa Makubwa Bunda kutokana na Mvua


ZAIDI ya watu 80 katika Kijiji cha Serengeti katika Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, hawana mahali pa kuishi, baada ya nyumba zao kuezuliwa kwa upepo mkali, ulioambatana na mvua kubwa.Diwani wa Kata ya Kunzugu inayojumuisha kijiji hicho, Ndovu Chacha, alisema upepo na mvua hiyo ulivuma juzi jioni na kwamba licha ya kuezua nyumba, pia umeharibu mazao ya mashambani.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Serengeti, Yombi Msagasa, alisema nyumba zilizoezuliwa na upepo huo ni         Mnara wa Tigo ulioanguka kutokana na mvua kubwa mkoani Bunda.                                                                                                          na kwamba sita miongoni mwa hizo, ziliezekwa kwa kutumia nyasi.Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa kijiji, nyumba nyingine 25 zilizokuwa zimeezekwa kwa mabati.

Imeelezwa kuwa kwa sasa watu ambao nyumba zao zimeezuliwa, wanahifadhiwa  na ndugu, jamaa na majirani zao.Diwani Ndovu alisema tathimini kuhusu  hasara kamili iliyosababishwa na mvua hiyo inaendelea kufanyika.

“Bado tunafanya tathmini ili kujua hasara kamili iliyosababishwa na mvua hiyo, lakini hali ni mbaya sana maana watu hawana mahali pa kuishi” alisema Diwani huyo, kwa njia simu.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Francis Isack, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya maafa wilayani humo, alisema  bado hajapata taarifa kuhusu tukio hilo.Hata hivyo alisema atalifuatilia
ZAIDI ya watu 80 katika Kijiji cha Serengeti katika Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, hawana mahali pa kuishi, baada ya nyumba zao kuezuliwa kwa upepo mkali, ulioambatana na mvua kubwa.Diwani wa Kata ya Kunzugu inayojumuisha kijiji hicho, Ndovu Chacha, alisema upepo na mvua hiyo ulivuma juzi jioni na kwamba licha ya kuezua nyumba, pia umeharibu mazao ya mashambani.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Serengeti, Yombi Msagasa, alisema nyumba zilizoezuliwa na upepo huo ni 31 na kwamba sita miongoni mwa hizo, ziliezekwa kwa kutumia nyasi.Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa kijiji, nyumba nyingine 25 zilizokuwa zimeezekwa kwa mabati.

Imeelezwa kuwa kwa sasa watu ambao nyumba zao zimeezuliwa, wanahifadhiwa  na ndugu, jamaa na majirani zao.Diwani Ndovu alisema tathimini kuhusu  hasara kamili iliyosababishwa na mvua hiyo inaendelea kufanyika.

“Bado tunafanya tathmini ili kujua hasara kamili iliyosababishwa na mvua hiyo, lakini hali ni mbaya sana maana watu hawana mahali pa kuishi” alisema Diwani huyo, kwa njia simu.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Francis Isack, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya maafa wilayani humo, alisema  bado hajapata taarifa kuhusu tukio hilo.Hata hivyo alisema atalifuatilia
Habari na Mwananchi

Jaji Mkuu awataka majaji kutathimini utendaji haki

JAJI Mkuu, Othman Chande amewataka Majaji Wafawidhi kupanga mikakati mbalimbali ya kuboresha tija, kutathimini majukumu yao pamoja na utendaji haki ulivyo sasa na wanakoelekea.

Alisema hayo juzi Bagamoyo mkoani Pwani wakati akifungua warsha ya siku mbili kwa majaji wafawidhi ya kujadili mambo mbalimbali wanayokabiliana nayo katika utendaji kazi wao wa kila siku ikiwamo utendaji haki na uendeshaji mashauri.

Alisema katika ofisi nyingi tija imepungua na kuwataka nafasi hiyo waliyopata waitumie kupanga mikakati ya kuongeza nguvu kuboresha tija, kuweka malengo nani ana jukumu gani na nani atatoa taarifa za utekelezaji wa majukumu.

“Lengo ni kuboresha utoaji wa haki … ni mara yetu ya kwanza kukutana tangu uteuzi wangu na madhumuni ya kukutana ni kujua tunakokwenda na mchango wa kila mmoja,” alisema Jaji Mkuu.

Alisema katika warsha hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani wataweka vipaumbele vya Mahakama kwa sababu fedha inayopatikana katika bajeti ya muhimili huo wa Dola haitoshelezi.

Jaji Othmani alisema fungu pia lililopatikana kwa kesi za uchaguzi, limechelewa kuwafikia hivyo wataangalia namna ya kuziendesha ziishe kabla ya Mei mwaka huu muda ambao ndio wa kikomo wa kesi za uchaguzi kisheria.
Imeandikwa na Regina Kumba habari leo

Wasomewa mashitaka wakiwa wamejeruhiwa kwa risasi

WAKAZI watano wa jijini Dar es Salaam akiwamo mganga wa jadi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku baadhi yao wakiwa wamejeruhiwa kwa kupigwa risasi, wakishitakiwa kwa kukutwa na bunduki na risasi bila kibali.

Kati ya watuhumiwa hao watano, wanne walikuwa wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili huku nguo zao zikiwa na damu.

Baadhi yao walionekana wamefungwa plasta za jasi na miguuni kuwekewa vyuma vya kurekebisha mifupa na kushindwa kutembea.

Watuhumiwa hao walisomewa mashitaka nje ya mahabusu ya Mahakama. Washitakiwa hao ni Yusuf Matimango (35), Athuman Kibambe (44), Ally Ngingame (42), Said Mangala (40) na mganga wa jadi Asha Ungando (45).

Wakili wa Serikali, Frida Mwela alimuomba Hakimu Bingi Mashabala kuwafuata washitakiwa mahabusu kuwasomea mashitaka kwa sababu hawezi kutembea kutokana na majeraha waliyonayo pamoja na maumivu makali.

Hakimu huyo alikubaliana na ombi hilo na kwenda mahabusu ambapo alisimama nje ya jengo la mahabusu na washitakiwa hao walitolewa nje na kuanza kusomewa mashitaka yao ambayo walikana yote.

Katika mashitaka yao walidaiwa Februari 10 mwaka huu katika mtaa wa Tandika Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam walikutwa na Bunduki aina ya Shot Gun na kukutwa na risasi katika tarehe hiyo hiyo na eneo hilo hilo.

Baada ya kukana mashitaka, walidai kuwa walikamatwa na kupigwa na askari wa kituo cha Polisi Sitakishari na wengine kupigwa risasi miguuni bila kufahamu makosa yao.

“Mheshimiwa hakimu sisi tumekamatwa bila kidhibiti chochote na tulipofika Polisi tulipigwa sana tukalazimishwa kusaini maelezo ambayo hatuyajui na waliokaa wakapigwa risasi na mmoja wetu ameuawa,” alidai Matimango.
                                               Mganga Asha Ungado akiwa chini ya Ulinzi
 Mshitakiwa mwingine alidai kuwa waliwekwa kituoni wiki nzima ndipo walipelekwa Hospitali. Hata hivyo walifungwa majeraha tu bila kupewa dawa yoyote huku mwingine akilalamika kuwa alisikia polisi wakiwaeleza madaktari akatwe mguu tu.

Hakimu Mwashabala alitoa masharti ya dhamana yaliyowataka kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika pamoja na kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni mmoja kila mmoja.
Imeandaliwa na Habari leo

Makamu wa Kwanza wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar azindua kikundi cha wajasiriamali Zanzibar

 


Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akinywa chai iliyotiwa viungo vilivyotengenezwa na wajasiriamali wa kikundi cha Mkuaji, Mtoni, Zanzibar. Maalim Seif alifanya hivyo baada ya kuzindua kikundi cha wajasiriamali hao wanaotengeneza bidhaa mbalimbali. (Picha na Mpigapicha Maalum Habari Leo).

Monday, February 20, 2012

Familia ya JK yamkana aliyetoweka na mamilioni UVCCM

Rais Jakaya Kikwete
Saramba, Arusha
FAMILIA ya Rais Jakaya Kikwete imekana kuwa na nasaba na aliyekuwa Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilayani Simanjiro, Alhaj Omar Yufus Kariaki, anayetuhumiwa kutokomea na zaidi Sh26 milioni, mali ya jumuiya hiyo.

Dada wa Rais Kikwete aliyehudhuria harambee ya kuchangisha fedha hizo kwa mwaliko wa Alhaj Kariaki, Tausi Kikwete aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kitendo cha kijana huyo kujinasibu kuwa na undugu na familia yao, kililenga katika kujinufaisha isivyo halali.

“Ukweli ni kwamba kijana huyo siyo ndugu yetu hata kwa mbali. Kwanza yeye anatoka Kondoa, wapi na wapi na sisi Wakwere wa Bagamoyo, mkoani Pwani, Hatumfahamu kabisa kwenye ukoo wetu zaidi ya kufahamiana naye tulipokutana Hija,” alisema Tausi.

Alisema yeye na ndugu yake Mwanaisha Kikwete, walikutana na mtuhumiwa walipokwenda kuhiji Mecca, Saudi Arabia na baadaye kupeana mawasiliano yaliyowawezesha kuendelea kuwa karibu hata baada ya kurejea nchini.

Alisema baada ya kurejea, yeye na Mwanaisha waliendelea kuwasiliana na Alhaj Kariaki aliyeonyesha kuwa kijana mwenye upendo na busara zilizowavutia wao kutembelea nyumbani kwao, Kondoa kwa mwaliko wake.
“Ukaribu wetu ulifikia hatua ya sisi kutembelea nyumbani kwao Kondoa baada ya yeye kutualika. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kijana huyo si ndugu yetu wala hana nasaba yoyote na kina Kikwete.” alisisitiza Tausi.

Alisema ilipofika wakati wa  harambee ya kutunisha Mfuko wa Mradi wa Maendeleo ya Vijana wa Wilaya ya Simanjiro, kijana huyo akiwa Katibu wa UVCCM wilayani humo, aliwaalika yeye na Mwanaisha kwenda kutoa semina kwa vijana kuhusu mbinu za ujasiriamali na miradi midogo.

Kwa mujibu wa Tausi, semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano ya Hoteli ya Manyara Inn, iliyoko Mererani siku mbili kabla ya harambee iliyoongozwa na aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani katika Serikali ya Muungano.
Hata hivyo kauli hiyo ya Tausi inapinga na kauli yake ya awali kupitia simu mwaka jana, ambapo licha ya kukiri kumfahamu Alhaj Kariaki, pia alisema wana unasaba naye.

“Ni kweli mimi na Mwanaisha ni dada wa mheshimiwa Rais (Kikwete) pia ni ndugu wa karibu wa kijana huyo (Alhaj Kariaki). Lakini binafsi sina mawasiliano naye tangu awe diwani huko kwako Kondoa. Kwa kifupi sijawasiliana naye tangu tuachane Mererani,” alisema Tausi mwaka jana alipoulizwa kuhusu mtuhumiwa huyo.

Katika harambee hiyo iliyohudhuriwa na viongozi na watu kadhaa maarufu kutoka Mikoa ya Manyara na Arusha, Nahodha alichangia Sh2 milioni fedha taslimu  wakati aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Henry Shekifu akichangia 500,000.
Kwa sasa Shekifu ni Mbunge wa Lushoto.

Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Simanjiro, Kiria Laizer, alisema baada ya yeye kukabidhiwa mfuko wenye fedha mara baada ya harambee ambayo mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka naye alichangia Sh1.5 milioni, alikabidhi mfuko huo kwa katibu wake Alhaj Kariaki ambaye hadi juzi alipojitokeza baada ya gazeti hili kuripoti suala hilo.

Mwenyekiti huyo aliwataja wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya UVCCM wilaya walioshuhudia makabidhiano kati yake na katibu wake  kuwa ni Bonny Shongo na Paul Sipitet.

Laizer aliyetoa pongezi na shukrani kwa mwandishi na gazeti la Mwananchi kwa kufanikisha mtuhumiwa kujitokeza, alisema awali walikuwa wakihofia kufuatilia suala hilo kwa karibu kwa hofu kwamba mtuhumiwa ana undugu na familia ya Rais.

Alhaj Kariaki ambaye sasa ni Diwani wa Kata ya Kwa Delo wilayani Kondoa, aliibuka wiki iliyopita baada ya habari zake kuripotiwa katika gazeti hili.

Alikiri kutokabidhi fedha zilizopatikana kwenye harambee hiyo iliyofanyika Mei 9 mwaka juzi akidai sehemu ya fedha hizo amezitunza kwenye akaunti yake, akisubiri kumalizika kwa kile alichodai kuwa mgogoro baina ya viongozi wa CCM mkoani Arusha ili azikabidhi.

SHIRIKA LA MASUALA YA HAKI ZA WATOTO NA SANAA KUFANYA KAMPENI KATA YA USAGARA KUELIMISHA JAMII HAKI ZA WATOTO

MKURUGENZI MTENDAJI WA SHIRIKA LA UNITE TANZANIA CHILDREN LINALOSHUGHULIKA NA MASUALA YA AFYA YA MTOTO NA SANAA BI IRENE RAJAB MHANDO

MKURUGENZI WA SHIRIKA LA UNITE TANZANIA CHILDRENBI IRENE MHANDO

KATIBU WA SHIRIKA HILO BI DORO EZEKEL NTUMBO AKIWA KATIKA MAHOJIANO NA MWANDISHI WA HABARI HIZI KATIKA OFISI YAO ILIYOPO KATIKA JENGO LA READ CROSS

SHIRIKA la Unite Tanzania linalojihusisha na afya ya mtoto na sanaa, limeandaa warsha kwa watendaji na wananchi katika kata ya Usagara Jijijini Tanga yenye lengo la kuijengea uwezo jamii kuhusu masuala yanayohusu haki mbalimbali za watoto ili waweze kuzitekeleza katika familia.

Sanjari na hilo, shirika hilo litaendesha kampeni kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo mabonanza ya watoto kwa kipindi cha miezi sita lengo likiwa kuhakikisha inapambana na vitendo vinavyowakosesha raha na haki watoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Bi Irene Mhando, akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, alisema kuwa lengo la mradi huo uliofadhiliwa na mtandao wa mashirika ya kiraia ya Foundation For Civil Society, alisema kwa kipindi cha miezi sita watajikita katika kata hiyo kuzungumzia kwa undani haki anazostahili kupata mtoto na vile vile kutambua vipaji vyao.

Alitaja makundi ambayo watakutana nayo katika kipindi hicho kuwa ni pamoja na watendaji wa mitaa, madiwani, polisi na wananchi wa kawaida katika mitaa mbalimbali ya kata hiyo ambapo wanatarajia kwamba itawajengea uwezo wa kutambua kwa nini jamii inapaswa kuwalea watoto kwa mtizamo mpana.

"Shirika litaendesha mradi wa kampeni ya haki ya mtoto katika kata ya usagara, kwa kipindi cha miezi sita watazungumza na wananchi, watendaji, polisi na makundi mengine ya jamii ili kuhakikisha malengo ya kuijengea uwezo jamii yanatimia ipasavyo na watoto wanaishi kama watu wengine," alisema Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake, Katibu wa shirika hilo, Bi Doro Ntumbo, akijibu suala la kwanini wamechagua kata ya Usagara na siyo kata nyingine za Jiji hilo, alisema kuwa kata hiyo imekuwa na matukio mengi ya unyanyasaji wa mtoto hivyo kuendesha kampeni katika kipindi hicho kutasaidia kuongeza uelewa kwa jamii na matukio hayo mwisho wa siku kupungua.

"Ukitazama malengo ya mradi huu, kuwaongezea uelewa jamii kuhusu sera ya mtoto ya mwaka 2008, kubadilisha tabia za watu kuhusu namna wanavyotakiwa kuwapa haki watoto...Sasa kata ya Usagara tumeonelea tuanze nayo kwa vile masuala ya unyanyasaji yamekuwa yakikithiri hivyo kufika kwetu tutasaidia maana pia tutaunda mabaraza ya watoto, hii itasaidia kupunguza matukio ya ukiukwaji wa sheria za haki za mtoto," alisema Bi Ntumbo.

MAHARAMIA WACHOMA MOTO BOTI YA UVUVI KIGOMBE


MKUU WA MKOA LUTENI (MSTAAFU) CHIKU GALLAWA (mwenye kilemba) AKIMNYOOSHEA KIDOLE MKUU WA WILAYA YA MUHEZA BW. METHEW NASEI KWAMBA AHAKIKISHE WATU WALIOCHOMA MOTO BOTI YA UVUVI KATIKA MWAMBAO WA KIGOMBE WANAPATIKANA HARAKA.

WANANANCHI WA KIGOMBE WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA. WA KWANZA KULIA NI MSAIDIZI WA MKUU WA MKOA BW. JOSEPH SURA.

BOTI YENYEWE AMBAYO IMECHOMWA MOTO NA MAHARAMIA

MKUU WA MKOA WA TANGA MH GALLAWA AKIWA NA VIONGOZI WA WILAYA YA MUHEZA NA KIJIJI CHA KIGOMBE WALIPOMTEMBEZA KWENYE MWAMBAO WA PWANI KUONA ENEO LILILOHIFADHIWA KWA AJILI YA SAMAKI AINA YA SILIKANTI.


MAHARAMIA wanaoendesha uvuvi haramu katika mwambao wa bahari ya Hindi mkoani Tanga, wameichoma moto boti ya doria inayomilikiwa na Taasisi ya Hifadhi ya bahari ya Silikanti iliyopo katika kijiji cha Kigombe wilayani hapa.

Kuchomwa kwa boti hiyo iliyokuwa ikielea baharini katika eneo hilo la Kigombe, kunatokana na dori ya mara kwa mara inayofanywa na taasisi hiyo kwa ajili ya kuwasaka maharamia wanaoendesha uvuvi haramu wa kutumia mabomu na nyavu ndogo zisizoruhusiwa, kumeelezwa kwamba ndiko kuliwapa hasira maharamia hao, wakachukua maamuzi hayo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kigombe Bew. Mwambi Haji alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni (Mstaafu) Chiku Gallawa aliyefika katika kijiji hicho kupata maelezo ya kuchomwa kwa boti hiyo, alisema tukio hilo lilitokea hivi karibuni na hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Mhifadhi wa bahari ya Silikanti Bw. Sylevester Kazimoto alisema katika kipindi cha mwaka uliopita waliendesha doria 192 za baharini na nchi kavu iliyohusisha vyombo vya dola ambayo iliwezesha kukamatwa kwa wavuvi haramu wapatao sita.

Alisema pamoja na kuwakamata wavuvi hao pia walikamata vifaa vinavyotumika kwa uvuvi huo ikiwemo baruti 29, bunduki 17 za kuulia samaki, mitungi 31 ya kuzamia, makokoro 94, nyavu za utale 11 na samaki wa baruti kilo 124.

Akizungumza katika mkutano na wananchi waliofika katika ofisi ya hifadhi hiyo Mkuu wa Mkoa alisema kuwa kila wananchi analojukumu kubwa la kulinda na kuhifadhi rasilimali za bahari hivyo akawataka wataalamu wa hifadhi hiyo wakishirikiana na serikali ya kijiji kuandaa mpango wa kuorodhesha wavuvi wote na boti zao kisha kuziandika namba.

Alisema suala la uvuvi haramu hivi sasa linatakiwa kupigwa vita baada ya muda mrefu nchi yetu kuliacha bila kuwachukulia hatua watu wanaoendesha uvuvi haramu ambao licha ya kuharibu mazingira pia wanaleta matatiz ya kiafya kwa kuvua samaki wa aina hiyo.

Hata hivyo, mjumbe wa serikali ya kijiji hicho Bw. Hassain Bakari almtaka mkuu huyo wa mkoa kuingilia kati suala la wavuvi haramu kukamatwa kisha kesi zao kuishia hewani kwa maana ya polisi na mahakamani hatua ambayo inasababisha wavuvi hao kutawala mwambao wa bahari kwa kuendesha vitendo hivyo wakiamini kwamba, wakikamatwa kesi zao watazimaliza.

Sunday, February 19, 2012

KATIBU TAWALA MKOA SINGIDA AASA PROGRAMU ZA MAJI KUSIMAMIWA NA WATU WALIOFUNZWA VYEMA.


Katibu tawala mkoa wa Singida Liana Hassan akifungua mafunzo ya siku moja yaliyohudhuriwa na kamati ya seketarieti ya mkoa wa Singida na za halmashauri za wilaya ya Manyoni na Singida.
Mshauri mwandamizi wa Mrogramu ya usambazaji wa maji vijijini RUWASA-CAD Kazuyuki Suenaga akitoa taarifa yake mbele ya mkutano wa mafunzo yaliyohudhuriwa na kamati za maji na usafi wa mazingira ya seketarieti mkoa wa Singida na za halmashauri za wilaya ya Singida na Manyoni.
Baadhi ya wanakamati za maji na usafi wa mazingira za seketarieti ya mkoa wa Singida na halmashauri za Manyoni na Singida.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Katibu tawala mkoa wa Singida Liana Hassan amesema programu za maji zinazofadhiliwa na wafadhili mbali mbali, zitakuwa endelevu tu iwapo zitasimamiwa na watu waliofunzwa vema mbinu bora za uendeshaji wa miradi ya maji.
Akifungua mkutano wa siku moja wa kwanza uliohusu mafunzo ya kuzijengea uwezo timu za maji na usafi wa mazingira za sekretarieti ya mkoa na zile za halmashauri za wilaya ya Manyoni na Singida, Hassan amesema mafunzo hayo yanalenga kuzijengea uwezo timu hizo ili ziweze kusimamia vizuri utekelezaji wa usambazaji wa maji vijijini awamu ya pili (Rural water supply and sanitation capacity development -RUWASA – CAD).
 AKifafanua amesema watu/viongozi hao waliofunzwa vema juu ya uendeshaji bora wa miradi ya maji, watasaidia kuwafunza na kuwahamasisha  watumiaji wa maji, mbinu sahihi zitakazosaidia miradi yao ya  maji, kuwa endelevu.
Aidha, Katibu huyo wa mkoa amesema lengo letu sote ni kuhakikisha kuwa asilimia 48 ya wakazi wa mkoa wa Singida wanapata maji safi na salama kwa umbali mfupi kutoka wanakoishi.
Lengo hilo litafikiwa tu iwapo jamii itakuwa imeelimishwa mbinu ya kutunza miradi hiyo.
Katika hauta nyingine, Katibu tawala huyo amesema utekelezaji wa mradi wa usambazaji wa maji vijijini utakapoanza, uangalie uwezekano wa kusaidia kugharamia masomo ya ufundi wa pampu za maji na injini kwa vijana waishio vijijini, ili kuondoa uhaba mkubwa wa mafundi wa aina hiyo ngazi ya vijiji.
 Kwa upande wake mshauri mwandamizi wa mradi wa RUWASA – CAD awamu ya pili Kazuyuki Suenaga, amesema kwa sasa wanaendelea kuzijengea uwezo timu za maji na usafi wa mazingira za sekretarieti ya mikoa na za halmashauri za wilaya.
Suenaga asema timu hizo za mikoa ya Singida, Tabora na Mwanza, zitajengewa uwezo kwa kupatiwa mafunzo yanayohusu uendeshaji na utunzaji bora wa miradi ya maji.
Amesema wanayo imani kwamba baada ya kuzifunza timu hizo na zenyewe, zitafunza jamii ili miradi iliyopo kwenye maeneo yao iwe endelevu.
Aidha, Suenaga amesema kutokana na hitaji la Tanzania la uboreshaji wa sekta ya maji, serikali ya Japan imeamua kuiunga mkono kwa kusaidia kupatikanaji wa maji safi na salama na usambazaji wake, maeneo ya vijijini chini ya ushirikiano na program ya Japan International Co-operation Asency (JICA).

Mwakyembe Asikitishwa na Taarifa ya Jeshi la Polisi

SIKU moja baada ya Jeshi la Polisi kudai Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe hajalishwa sumu, kiongozi huyo ameibuka na kusema amekerwa na  jeshi hilo kutoa taarifa za uongo kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuingilia utaratibu wa matibabu bila ya idhini yake. 
Mwakyembe alifafanua kuwa sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, bali  inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa na kusisitiza kuwa, aliwahi kulieleza jeshi hilo kwamba kuna kundi limejipanga kumdhuru, lakini lilifanya mzaha.  Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kyela, alisema tangu alipoanza kutumiwa ujumbe wa vitisho na wabaya wake aliowaita ni mafisadi mwanzoni mwa mwaka jana, alikuwa akitoa taarifa kwa jeshi hilo, lakini mpaka sasa limeshindwa kuwachukua hatua zozote. 
Kauli hiyo ya Dk Mwakyembe inafuatia Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai(DCI), Robert Manumba kuwaeleza waandishi wa habari juzi kwamba wananchi wanatakiwa kupuuza madai yaliyotolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta kuwa Waziri Mwakyembe amelishwa sumu.
  DCI Manumba alieleza kuwa waliwasiliana na Wizara ya Afya ili kubaini chanzo cha ugonjwa wa Naibu Waziri huyo, lakini taarifa iliyowasilishwa na wizara hiyo kwa Jeshi la Polisi imeonyesha kuwa, hajalishwa sumu.  Katika taarifa yake aliyoitoa jana, Mwakyembe alisema anapata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yake, au walisoma taarifa nyingine na kama waliisoma, taarifa hiyo wenyewe ama walisomewa.
Katika taarifa hiyo, alisema alichokisema DCI  Manumba kwa waandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Hospitali ya Apollo ya nchini India anakotibiwa.  “Ripoti inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow (ndani ya ute wa mifupa) kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua,”  “Lakini vyombo vyetu vya dola vinapelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu kwamba ‘sikulishwa sumu’, sikulishwa sumu,” alisema Mwakyembe katika taarifa hiyo. 
Aliongeza kuwa,“Nimelazimika leo Jumamosi (jana) kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari uliofanyika jana (juzi) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa, “sikunyweshwa sumu”.  Mwakyembe alisema taarifa hiyo ya DCI Manumba imeshindwa kufafanua ugonjwa wake wa ngozi umesababishwa na nini.  Waziri huyo alisema msimamo huo wa Jeshi la Polisi umemkera katika hali aliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yake  na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea Hospitali ya Apollo ambako bado anatibiwa.
Alisema kuna ufinyu wa uelewa uliojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi uliosisitiza kuwa ’hakunyweshwa sumu’  wakati sumu si lazima unyweshwe ili imdhuru mtu, bali inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa.  Waziri huyo alisema kuwa ni hatari kwa Jeshi hilo kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Alifafanua kwamba Februari 9, mwaka jana, alimwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi(IGP) Said Mwema, kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yake na ya viongozi wengine.  Alisema kuwa kwa kutambua kuwa Polisi wa Tanzania husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo wafanye kazi, alihakikisha ameainisha katika barua hiyo kila ushahidi alioupata au kupewa.
  Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema anashangazwa na utaratibu unaotumiwa na Jeshi hilo wa kusubiri ushahidi mezani bila ya kuchunguza na kuwafananisha na mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani.  Alisema utaratibu huo haupo popote duniani ila ni  Tanzania peke yake, kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi.  “ Polisi duniani kote wanachohitaji ni kupata clue  au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika,” Mwakyembe alisema katika taarifa hiyo.  Naibu waziri huyo alisema pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi aliokuwa nao, yapo mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo. 
Mambo manne  Akifafanua mambo hayo katika taarifa hiyo, alisema siku chache baada ya kumkabidhi IGP Mwema  barua hiyo, alitumiwa timu ya wapelelezi ofisini kwake ili kuchukua maelezo yake ya ziada.  Alifafanua kuwa timu hiyo ilikuwa inaongozwa na Ofisa wa polisi ambaye wiki chache zilizopita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia dawa za kulevya mtoto wa mmoja wa wafanyabiashara maarufu nchini, suala alilodai kuwa mpaka sasa uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha.
  Alisema kwa msingi huo, aliona ameletewa mtuhumiwa wa rushwa na ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi jambo ambalo haliwezekani na kwamba suala lake limefanyiwa mzaha.  Mwakyembe alisema wiki chache baada ya barua yake kuwasilishwa kwa IGP na timu ya polisi kuanza kazi, Jeshi hilo likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari aliowatuhumu kushirikiana na majambazi.  “Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza,”ilibainisha taarifa hiyo. 
Alisema tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari, wale aliowatuhumu kwenye barua yake, walihamishiwa mikoa mingine.  Mwakyembea alisema ili kumkatisha tamaa kabisa, barua yake ya ‘siri’ kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari iliyokebehi na kukanusha taarifa nzima aliyoitoa   “Sijui kwa faida ya nani,” alihoji katika taarifa hiyo na kuongeza, “ Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa Jeshi la Polisi.  Akitoa mfano wa Waziri Sitta, kuwa hivi karibuni, kiongozi huyo alihojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, lakini  taarifa ya mahojiano  ikaonekana  kwenye moja ya magazeti, ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta na kubainisha kuwa uadilifu wa uongozi wa Jeshi la Polisi, umefikia pabaya.

  Mwakyembe alisema, katika barua yake kwa IGP alieleza kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kumuua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wao.   Waziri huyo alieleza kushangazwa na msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama alipewa sumu au la na kuamua kutoa tamko hata kabla ya kumchunguza alivyo.
Alisema polisi hawajawahi kumhoji yeye wala wasaidizi wake ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaomfanyia uchunguzi nchini India.  Waziri huyo aliwashangaa polisi badala ya kumshukuru,  Waziri Sitta kwa sababu amekuwa akiwapa tahadhari kuhusu afya yake ili suala hilo lichunguzwe kwa kina, badala yake sasa anaonekana adui wao.  “Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Mlimani na DCI Manumba. 
Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa Sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua,” alilalamika katika taarifa yake hiyo.  Alisema viongozi hao wanajua kuwa hawezi kukaa kimya au kumung’unya maneno pale anapoona haki inakanyagwa bila ya kujali matokeo ya uamuazi huo.  Katika taarifa hiyo, Dk Mwakyembe aliwataka Watanzania kuombeana afya na uhai ili waweze kutenda haki na waendelee kuitetea nchi yao ikiwemo kumalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA na Kagoda kwa maslahi mapana ya Taifa.   Historia ya ugonjwa wa Mwakyembe  Dk Mwakymbe alianza kuumwa Oktoba 9 mwaka jana na baadaye kupelekwa nchini India na kulazwa katika Hospitali ya Apollo kwa matatibu. Alirejea nchini Desemba 11, mwaka jana baada ya kulazwa hospitalini  humo kwa takribani miezi miwili.

Msemaji wa familia ya Dk Mwekyembe na Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa, alisema baada ya mbunge huyo  kurejea nchini, afya yake ni njema ndio maana ameruhusiwa kutoka hospitali.
 Kauli za Waziri Sitta   Mara kadhaa Waziri Sitta amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari akisisitiza kuwa ugonjwa wa Dk Mwakyembe, umetokana na kulishwa sumu.  Akiwa kwenye uzinduzi wa Programu ya Neno la Hekima kutoka kwa Kiongozi iliyoanzishwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima la Kawe, jijini Dar es Salaam Januari 28 mwaka huu, Sitta alisema:

“ Nasema Dk Mwakyembe kapewa sumu, kama vyombo vya uchunguzi vinasema siyo, basi watueleze ukweli, tena haraka,” alisisitiza Waziri Sitta katika hafla hiyo.
Sitta alihoji “ Ni vipi uone binadamu ambaye ukimshika katika ngozi unga unamwagika chini, mhudumu anakuja kuufagia, lakini baada ya saa moja unarudia tena, kitu hicho si cha kawaida.”   Sitta alisema wamejaribu wameshindwa kwa kuwa Dk Mwakyembe analindwa kwa jina la Yesu ambalo ni kubwa kuliko yote.

 Waziri Nahodha  Akijibu moja ya kauli hizo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nohodha alimtaka Waziri Sitta awasilishe ushahidi wake ili ufanyiwe kazi badala ya kuzungumza nje ya vyombo vya sheria.  Hata hivyo, Sitta alisema hatapeleka ushahidi wa madai aliyotoa kuwa Dk Mwakyembe alilishwa sumu kwa kuwa polisi tayari wanao ushahidi.

Alisema wanachotakiwa kufanya Polisi ni kufanya uchunguzi kuhusu madai hayo ya Dk Mwakyembe kulishwa sumu kwa kuwa ushahidi wanao na wasianze kurushiana mpira.
“Waziri Nahodha anataka ushahidi gani ikiwa taarifa za madaktari zinazomhusu Dk Mwakyembe kuhusu sumu aliyopewa  zilishapelekwa polisi, anataka mimi nitoe ushahidi gani?” Alisema Waziri Sitta.  

MKAZI WA SINGIDA AHUKUMIWA KUPELEKWA TAASISI YA MAGONJWA YA AKILI KWA KIPINDI CHOTE CHA MAISHA YAKE KWA KOSA LA MAUAJI.

Jaji Mwanahamisi Kwariko.
Nathanel Limu.
Mahakama kuu kanda ya Dodoma inayoendelea na vikao vyake mjini Singida imemwamuru mshitakiwa Simon Andrew mkazi wa kijiji cha Kidaru wilayani Iramba, kupelekwa kwenye taasisi inayojishughulisha na magonjwa ya akili kwa kipindi chote cha maisha yake yaliyobakia hapa duniani.
Akitoa amri hiyo, Jaji Mwanahamisi Kwariko amesema mahakama yake imekubaliana na upande wa mashitaka kwamba mshitakiwa Simon alimuua bibi kizee Tiale Mbogo kwa kukusudia.
Aidha, Jaji Kwariko amesema mahakama pia inakubaliana na upande wa mashitaka kwamba wakati mshitakiwa Simon akitenda kosa hilo hakuwa na akili timamu.
“Mahakama hii imepokea ripoti kutoka kwa daktari kuwa mshitakiwa ni mgonjwa sugu wa afya ya akili, Kwa hali hiyo, mahakama imefiakia uamuzi kuwa mshitakiwa Simon apelekwe kwenye taasisi inayojishughulikia  watu wenye magonjwa ya akili”,amesema.
Awali mwanasheria mkuu wa serikali Neema Mwanda, alidai mbele ya Jaji Kwariko kuwa mnamo Desemba 18 mwaka 2000 katika muda usiofahamika, mshitakiwa alimuuwa kwa makusudi kikongwe Tiale Mbogo.
Neema amesema kuwa mshitakiwa Simon alikutwa na majirani wa bibi kikongwe Tiale akiwa amesimama jirani na mwili wa Tiale.
Watu hao waliweza kumkamata mshitakiwa na kumfikisha mbele ya vyombo vya dola.
Imedaiwa bibi Tiale kabla ya kufikwa na mauti hayo, alikuwa akiota jua. Mshitakiwa alimpiga na kitu ambacho hakijafahamika na kisha kufariki dunia papo hapo.

MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAATUA MKOA WA KATAVI LEO KUANZA ZIARA YAKE.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Katavi Mkoa wa katavi kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku tatu ya mkoa huo jana Februari 18, 2012. Kushoto ni Mkewe Mama Asha Bilal, na (kulia) ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Eng. Stella Manyanya. (Picha na Muhidin Sufiani-OMR).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakifurahia ngoma ya asili ya Mkoa wa Rukwa, wakati walipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Katavi mkoani humo jana Februari 18, kwa ajili ya kuanza ziara ya siku tatu.(Picha na Muhidin Sufiani-OMR).

JK,Dr SLAA WAONGOZA MATEMBEZI YA HISANI KUSAIDIA UJENZI WA HOSPITALI YA KINAMAMA YA CCBRT JIJINI DAR.


Rais Kikwete akiongoza matembezi ya Hisani kuchangia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya Baobab iliyo chini ya CCBRT jijini Dar es salaam. Katika picha kutoka kulia Meya wa Ilala Mh. Jerry Silaa, Meya wa Kinondoni Mh. Mwenda, Bw. Erwin Telemans Mkurugenzi mtendaji wa CCBRT, Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya CCBRT Bw. Wilbroad Slaa na kulia kwa Rais ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hadji Mponda na Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Bw. Andrew Dunnet pamoja na Mwamvita Makamba wa Vodacom Tanzania katika matembezi hayo jana asubuhi.
Rais Jakaya Kikwete akishiriki katika mazoezi ya viungo kabla ya kuongoza matembezi ya hisani kuchangia   ujenzi wa hospitali ya kinamama matatizo mbalimbali ya uzazi katika hospitali ya CCBRT jana asubuhi jijini Dar es salaam. Matembezi hayo yameanzia katika hoteli ya Golden Tulip na kumalizika katika Hospitali ya CCBRT Mikocheni, matembezi hayo yameandaliwa kwa pamoja na kampuni ya Vodacom Tanzania, Vodafone pamoja na hospitali ya CCBRT Kampeni hiyo inaitwa Find your Moyo.(Picha na IKULU).

Saturday, February 18, 2012

Dk Slaa: Sina mpango wa kuwania Ubunge Arumeru

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema hana mpango wa kugombea ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki.Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alikaririwa akisema kama Dk Slaa ataamua kuwania ubunge katika jimbo hilo, chama kitaheshimu uamuzi wake akisema: “Katika suala la kugombea, utashi binafsi ni jambo la msingi... kama Dk Slaa ataamua kugombea ubunge Arumeru Mashariki, tutaheshimu uamuzi wake.”

Mbowe alisema Dk Slaa amekuwa akiombwa kugombea ubunge katika maeneo mengi ikiwemo Igunga na chama hakikuwahi kumlazimisha kwani jambo la kwanza ilibidi mwenyewe aonyeshe utashi binafsi wa kutaka kuwania kiti hicho.“Dk Slaa aliwahi kuombwa akagombee Igunga lakini hakwenda. Hii ni kwa sababu anakubalika karibu kote nchini, hivyo kama atakuwa na utashi binafsi kwanza, nadhani taratibu za chama zitatumika tu kufikia uamuzi,” alifafanua.

Lakini akizungumza katika mahojiano maalumu na Kituo cha Televisheni cha Mlimani jana, Dk Slaa alisema hafikirii kuwania ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa kuwa kazi yake ni kukijenga chama kitaifa ili kiweze kupata wabunge wengi.

Alisema hawezi kujifunga kwenye jimbo moja wakati alishasema kuwa kazi yake ni kutetea wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwa kukijenga chama chake.“Siwezi kujifungia kwenye jimbo moja, nilishasema kazi yangu ni kukijenga chama ili kiweze kupata wabunge wengi,” alisema Dk Slaa.

Wakati Dk Slaa akitoa msimamo wake huo, baadhi ya makada waliokwishajitokeza na kuonyesha nia ya kugombea jimbo hilo wamesema kama ataamua wako tayari kumpisha.

Mmoja wa makada hao ni aliyepeperusha bendera ya Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010 jimboni humo, Joshua Nasari ambaye alitoa upinzani mkali kwa mgombea wa CCM, marehemu Jeremiah Sumari.

Tangu juzi kumekuwa na mjadala katika mitandao ya kijamii huku baadhi wakimtaka Dk Slaa akagombee ubunge Arumeru Mashariki kuziba pengo la marehemu Sumari lakini, wengine wanapinga na kumtaka aendelee kubaki na nafasi yake ya katibu mkuu wa chama kwa lengo la kukijenga.

Joshua Nasari

Kwa upande wake, Nasari (26) ambaye ana mtaji mkubwa wa kura alioupata katika uchaguzi wa mwaka 2010, alisema yupo tayari kufanya mazungumzo na viongozi wa juu ya chama chake juu ya kumpisha Dk Slaa kuwania ubunge katika jimbo hilo kama akihitaji.

Nasari ambaye amerejea hivi karibuni mjini Arusha akitokea Marekani, leo anatarajiwa kuchukua fomu rasmi ili kuwania nafasi hiyo kupitia Chadema.“Nimesikia maoni kupitia mitandao na wadau wakimuomba Dk Slaa kugombea, hili ni jambo jema kwetu kwani wananchi wanajua jimbo hili tunashinda Chadema na kama Dk (Slaa) akitaka kugombea demokrasia ya chama chetu itafanya kazi, kwani kikubwa tunataka ushindi,” alisema Nasari.

CCM walalamika
Baadhi ya wanachama wa CCM, wamelalamikia gharama kubwa za fomu za chama hicho zinazotolewa kwa makada wake wanaotaka kuwania ubunge katika jimbo hilo.Wanachama Julias Nangisa na Lameck Kanangira walisema jana kwamba gharama ya Sh300,000 wanayotakiwa kulipa ni kubwa mno kwa mwanachama wa masikini wa CCM.

“Gharama hizi kubwa zinaonyesha kama mtu huna kipato cha kutosha huwezi kuwa kiongozi ndani ya CCM kwani fomu tunatakiwa kulipa 100,000 na mchango wa chama 200,000 kabla ya kukabidhiwa fomu,” alisema Nangisa na kuungwa mkono na mwenzake.

Alipoulizwa kuhusu malalamiko hayo, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Arumeru, Edson Lihweuli alisema: “Kwanza hao wanaolalamika walipaswa kuja kwangu na siyo kwenye vyombo vya habari, gharama ya fomu ni Sh100,000 na mchango ni Sh200,000 na malipo haya ni halali.”

Kwa upande wake Chadema kinatoa fomu zake kwa wagombea kwa Sh50,000 bila ya gharama nyingine za ziada.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema Mkoa wa Arusha, Ephata Nanyaro alisema japokuwa chama hicho ni kichanga na bado kinahitaji michango ya wanachama, wameona gharama ya fomu ikiwa ni Sh50,000 inawafanya wanachama wengi hasa wa hali ya chini kujitokeza kugombea.

Hadi sasa wanachama tisa wa vyama vya CCM na Chadema wamejitokeza kuchukua fomu kupitia vyama vyao hadi jana mchana. Wagombea wa CCM ni sita na Chadema watatu.

Takukuru waweka CCM
Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Arusha, wameweka kambi katika Ofisi za CCM Wilaya ya Arumeru ili kuchunguza mwenendo wa utoaji fomu na pia vitendo vya rushwa.

Liyumba kusimama kizimbani tena Machi 15

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imeshindwa kumsomea maelezo ya awali aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, anayekabiliwa na kesi ya kukutwa na simu kwenye gereza la Ukonga, kutokana na wakili wake anayemtetea Majura Magafu kutokuwapo mahakamani.

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda, jana alidai mbele ya Hakimu Mkazi Stuart Sanga, kuwa kesi imekuja kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa maelezo ya awali yanayohusiana na mashtaka yanayomkabili.

Baada ya kutoa maelezo hayo, Liyumba aliieleza mahakama kuwa wakili wake hayupo amekwenda mkoani Arusha kuhudhuria mkutano.Hivyo, Hakimu Sanga aliiahirisha kesi hiyo hadi Machi 15, mwaka huu itakapopelekwa tena kwa ajili ya Liyumba kusomewa maelezo ya awali.

Hatua hiyo ilikuja baada ya Mahakama ya Kisutu kulitupilia mbali ombi la Liyumba kutaka afutiwe kesi hiyo kwa sababu, haina mamlaka ya kuisikiliza.

Liyumba kupitia kwa Wakili Magufu aliwasilisha pingamizi hilo la awali akidai mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza, kwa sababu taratibu za awali za sheria ya Magereza ya mwaka 2002 hazikufuatwa.

Wakili Magafu alidai kwa mujibu wa Sheria ya Magereza ya mwaka 2002, inataka mshtakiwa anayeishi mahabusu kabla hajaletwa mahakamani asomewe mashtaka na ofisa wa magereza gerezani, iwapo atapatikana na hatia atapewa adhabu.
Alidai kuwa iwapo mshtakiwa huyo ataonekana amekuwa mtendaji sugu wa makosa akiwa gerezani,  italazimika afunguliwe mashtaka katika mahakama za uraiani.

Akipangua hoja za upande wa utetezi, Wakili wa Serikali Eliezabeth Kaganda, alidai kuwa kesi ya aina hiyo inayomkabili Liyumba siyo ya kwanza kufunguliwa mahakama nchini.

Kaganda alitaja kesi ya jinai Na. 472/2009 iliyokuwa ikimkabili Juma Matonya katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke na Hakimu Mzava alimhukumu kifungo cha miezi sita jela baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kukutwa na simu gerezani.Kesi nyingine mbili za aina hiyohiyo, ambazo washtakiwa walitiwa hatiani moja akitakiwa kulipa faini ya Sh20,000 na nyingine kwenda jela miezi sita.

 Wakili Kaganda alieleza kuwa kabla hawajamfikisha Liyumba mahakamani hapo Jeshi la Magereza lilikuwa na mamlaka ya kushughulikia tuhuma zilizokuwa zikimkabili mshtakiwa na kwamba, mkurugenzi wa mashtaka na maofisa wa magereza walikuwa wameishaamua kuifungua kesi hiyo mahakamani hapo.

Lakini kwa sababu hiyo haikuwa mara ya kwanza kukutwa na simu gerezani na alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu, hivyo haikuwa rahisi kumpa adhabu akiwa gerezani.

Awali, Septemba 8, mwaka jana Liyumba alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza akikabiliwa na shtaka la kukutwa na kitu kilichokatazwa gerezani chini ya kifungu cha 86 (1,2) cha sheria ya Magereza kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Liyumba ambaye wakati huo alikuwa mfungwa mwenye Na.303/2010, Julai  mwaka jana, aliyokuwa akitumia kufanyia mawasiliano binafsi wakati ni kinyume cha sheria.

HAKAMA NCHINI ZATAKIWA KUTOAHIRISHA BILA SABABU ZA MSINGI

Na.Ashura Mohamed - arusha
Mahakama nchini zimetakiwa kutoahirisha kesi mara kwa mara ikiwa hakuna sababu za msingi za kufanya hivyo kwa kuwa inachelewesha wahusika kupata haki zao kwa wakati.
Hali inatokana na mahakama nyngi hapa nchini kuahirisha kesi mara kwa mara bila sababu za msingi hali ambayo haileti tija kwa wenye kudai haki.
Hayo yamesemwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Othman Chande wakati akifungua mkutano mkuu wa chama cha wanasheria Tanzania bara uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa(AICC) mkoani Arusha.
Jaji chande amesema kuwa kesi zinaweza kuahirishwa ikiwa kuna sababu za msingi kama msiba au wakili ambaye yupo katika kesi hiyo ana kesi nyingine lakini sababu nyingine ambazo si za msingi zisisababishe kesi kuahirishwa ili kesi hizo zimalizike kwa wakati.
Pia Jaji chande amesema kuwa kuna changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na wananchi wenye uwezo wa kawaida kupata haki yao ya msingi ya wakili pindi wanapokuwa wanakabiliwa na kesi kubwa kama ubakaji ambazo adhabu zake ni kubwa kama vile kifungo cha maisha ambapo walitakiwa kupata mtetezi lakini kutokana na mawakili wa serikali kuwa wachache wanakosa huduma hizo.
Kwa upande wake rais wa chama hicho Francis Stola amesema kuwa mkutano huo ni wa kutathimini utoaji haki na majukumu ya mahakama ambapo ameiomba serikali upande wa mahakama kutenga fungu la fedha za kutosha ili mahakimu na majaji waweze kufanya kazi zao kwa umakini zaidi.
Hata hivyo amesema kutokana na kukosekana kwa fungu la fedha la kutosha hali hiyo inapelekea wanasheria wengi kupokea rushwa na kupelekea haki kupotea kwa wananchi ambao waniotegemea mahakama.
Aidha stola ameeleza kuwa kukosekana kwa vitendea kazi kama maktaba na kukosekana kwa vitabu vya sheria ni tatizo pindi mahakama inapotaka kutoa maamuzi.
Stola amesema mada ambazo zitakazotolewa kuwa ni pamoja na mfumo wa uendeshaji wa kesi za madai,njia gani iweze kutumika ili bunge liweze kutunga sheria ambazo zitakuwa bora,mfumo wa uwendeshaji wa kesi a jinai na nyingine nyingi.
Mkutano huo wa wanasheria kutoka Tanzania bara wameshiriki ili kuhakikisha kuwa wanakuwa na mchango wao ili wananchi wenye uwezo wa chini wanapatiwa haki zao

BASI LA ABOOD LAPATA AJALI ASUBUHI YA LEO MAENEO YA MBEZI


Wananchi wakitazama jinsi basi la abood lilivyopinduka huku wengine wakiokoa abiria waliopo kwenye basi hilo asubuhi ya jana.Picha Na Lukaza
Basi la kampuni ya Abood likiwa limepinduka maeneo ya Mbezi likiwa linatoka Mkoani Morogoro kuelekea Dar es salaam asubuhi ya leo.Chanzo cha ajali hii hakikujulikana ila inasemekana ni kutokana na dereve kuovertake gari mbele na hatimaye kumshinda na kupinduka.

Wanafuzi 3303 wafutiwa mitihani yao, hawataruhusiwa kurudia mpaka baada ya miaka mitatu


Na Fatma A Mzee Habari Maelezo
Katibu mtendaji wa baraza la Taifa la mitihani Tanzania (NECTA), Dkt Joyce L. Ndalichako ameeleza kuwa jumla ya wanafuzi 3303 wamefutiwa mitihani yao kutokana na kuthibitika kufanya udanganyifu.
DK. Joyce liyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Bwawani mjini zanzibar.
Aliongeza kuwa kati ya hao kuna baadhi ya watahiniwa wameandika matusi katika karatasi zao kamitihani na wengine kuwacha maswali na kutokujibu kabis maswali ya majibu hayo. Hata hivyo Dkt Joyce alishindwa kujibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari kutokana na kutokufanya majumuisho yote ya mitihani hiyo iliyofanyika nchini.
Aidha alieleza kuwa suwala hilo la udanganyifu linafanyika katika makundi yote matatu ambao ni walimu wazazi pamoja na wanafunzi wenyewe.
Dkt Jooyce ameongeza kuwa waliofutiwa mitihani kulitokana na kikao cha 86 nambari 6 B kilichofanyika tarehe 7-2-2012. Kanuni za baraza la mitihani zinazoeleza kuwa watahiniwa hao hawataruhusiwa kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.
Hata hivyo amesema kuwa baraza limewaonea huruma kwa kuwapa hukumu hiyo kwani katika kanuni za NECTA wanafunzi wanaofutiwa mitihani hawaruhusiwi kufanya mitihani tena.
Pia katibu mtendaji huyo aliwataka wasimamizi kuwa makini katika kazi zao na kusimamia kwa uwangali mitihani kwani udanganyifu huwa unamadhara makubwa katika taifa ambapo kutazalishwa wataalamu wasio na viwango hasa katika kipindi hiki ambapo tunaingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Wakati huo huo chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kimewasimamisha wanafunzi watatu wa chuo hicho baada ya kubainika walitumia vyeti vya kughushi wakati walipojiunga na chuo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari katika chuo hicho, Vuga mjini Zanzibar, mwanasheria wa SUZA Mtaibu Abdalla Othman amewataja wanafunzi hao kuwa ni Mahfoudhat Hassan Khamis anaesoma digrii ya sanaa, Shafii Suleiman Mringo anaesoma cheti cha teknolojia ya habari na Yussuf Khamis anaesoma cheti cha sayansi ya komputa.

TATHIMIN YA MBIO ZA MWENGE- MOROGORO


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Msham Abdulla Khamis aliesimama katikati akifunga mkutano wa Tathimin ya mbio za Mwenge wa Uhuru na wiki ya Vijana katika Ukumbi wa Edema Mkoano Morogoro jana .
Baadhi ya viongozi waandamizi wa Kitaifa na waandaaji wa sherehe za Mwenge wakiwa kwenye tathimin ya mbio za Mwenge na wiki ya vijana wakati wa mkutano wao uliofanyika kwenye Ukumbi wa Edema Mkoani Morogoro leo wakiwa kwenye majadiliani ya kina .
Kamisaa wa Tume ya Sensa ya Taifa Mhe. Paul Kimiti akiongea na Viongozi na Waandaji wa Mbio za Mwenge Kitaifa kwenye mkutano wao wa kutathimin mbio za Mwenge uliofanyika kwenye Ukumbi wa Edema Mkoani Morogoro jana.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Msham Abdulla Khamis wa pili kulia , akiwatambulisha Wanajeshi wawili wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ndugu Tanu Mlowezi kushoto na Mary Shayo Kulia waliofikisha Mwenge wa Uhuru kwenye Mlima Kilimanjaro, Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari ,Vijana ,Utamaduni na Michezo mama Sihaba Nkinga wa tatu kulia wengine ni Kaimu Mkurugenzi wa Vijana ndugu James Kajugusi wa nne kulia na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Vijana Dkt. Steven Kissui kwenye mkutano wa Tathimin ya mbio za Mwenge uliofanyika kwenye Ukumbi wa Edema Mkoani Morogoro jana.

Friday, February 17, 2012

Nauli za Ndege za Shushwa Songea

WAKAZI wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wamempongeza Mkuu wa Mkoa huo, Said Mwambungu kwa jitihada mbalimbali za kuhamasisha maendeleo ambazo amekuwa akizichukua.

Jitihada hizo ni kuwasaidia wananachi kupata huduma za usafiri wa ndege baada ya kufanikiwa kuzungumza na uongozi wa kampuni ya ndege ya AURIC Airline na kukubaliana kushusha gharama za usafiri wa ndege kutoka Sh400,000 hadi 325,000 kwa safari za kutoka Songea hadi Dar es salaam  .
 Habari zaidi katika habari za Kibiashara                                                                                                                       

Dk.Slaa anaruhusiwa kugombea Arumeru


    Mwenyekiti wa Chadema, Freeman    Mbowe




















 WAKATI Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akianza kugusa hisia za watu wanaomtaka agombee ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki, mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe amesema iwapo mtendaji mkuu huyo wa chama ataamua kuwania kiti hicho, wataheshimu uamuzi wake.

Wakati Mbowe akitoa kauli hiyo, aliyepeperusha bendera ya Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010, Joshua Nasari na kutoa upinzani mkali kwa mgombea wa CCM, marehemu Jeremiah Sumari, naye amesema kama katibu mkuu wake ataamua kuwania kiti hicho, hatakuwa na pingamizi ikiwa chama kitaamua kwani lengo ni kutwaa jimbo hilo.

Akizungumza na Mwananchi jana baada ya kuibuka mjadala kuhusu uwezekano wa Dk Slaa kuwania jimbo hilo, Mbowe alisema, "Katika suala la kugombea, utashi binafsi ni jambo la msingi...,kama Dk Slaa ataamua kugombea ubunge  Arumeru Mashariki, tutaheshimu uamuzi wake."

Mbowe alisema katika uteuzi wa chama, kuna vigezo vinavyoangaliwa ikiwa ni pamoja na jinsi mtu anavyokubalika kwa wananchi anakogombea, sifa zake na utashi wake binafsi na kuongeza, "Hatuna uteule katika chama."

Hata hivyo, Mbowe alisema Chadema hakiwezi kumlazimisha Dk Slaa akagombee jimbo hilo kama mwenyewe utashi haumtumi kufanya hivyo, na kwamba hana shaka na kukubalika kwa katibu mkuu huyo kutokana na imani aliyojijengea kwa umma wa Watanzania.

Mbowe alisema Dk Slaa amekuwa akiombwa kugombea ubunge katika maeneo mengi likiwamo Jimbo la Igunga, lakini chama kisingeweza kumlazimisha kwani jambo la kwanza ilibidi mwenyewe aonyeshe utashi binafsi wa kutaka kuwania kiti hicho.

"Dk Slaa aliwahi kuombwa akagombee Igunga, lakini hakwenda. Hii ni kwasababu anakubalika nchini karibu kote, hivyo kama atakuwa na utashi binafsi kwanza, nadhani taratibu za chama zitatumika tu kufikia uamuzi," alifafanua.

Mwenyekiti huyo wa Chadema pia alitoa angalizo kwamba, wakati mwingine uamuzi wa chama kupata mgombea unaangalia jinsi mgombea alivyo na mtandao katika jimbo analotaka kugombea ili hata kama akichaguliwa aonekane ni mbunge wa eneo hilo.

"Ndiyo maana nasema kuna vigezo vingi tu, kwa mfano mtu anaweza kuwa mbunge mzuri bungeni, lakini je, ana connectivity (kinachomuunganisha) jimboni, kuangalia kama ana makazi na mtandao mwingine kwani asije akawa mbunge mzuri bungeni, lakini jimboni akiwa kama mgeni hivyo watu wakaona kama kimewapelekea pandikizi tu,"alifafanua Mbowe.

Tangu juzi kumekuwa na mjadala katika mitandao ya kijamii huku baadhi wakimtaka Dk Slaa akagombee ubunge Arumeru Mashariki kuziba pengo la aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Marehebu Sumari, lakini wengine wanapinga na kumtaka aendelee kubaki na nafasi yake ya katibu mkuu wa chama kwa lengo la kukijenga.

Hata hivyo, Dk Slaa ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 alishika nafasi ya pili akiwa nyuma ya Rais ya Jakaya Kikwete, juzi alinukuliwa na gazeti moja la kila siku (siyo Mwananchi) akisema, "Siwezi kulizungumzia jambo hilo, maana nilikwisha kusema muda mrefu kuwa sitaki tena ubunge na isitoshe mimi si mwenyeji wa Arumeru,"
                                                 Katibu Mkuu Chadema Dr.Willibrod  Slaa              
 Joshua Nasari                  
Kwa upande wake Nasari (26) ambaye ana mtaji mkubwa wa kura kufuatia matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010 alitoa msimamo wake akisema  yupo tayari kufanya mazungumzo na viongozi wa juu ya chama chake juu ya kumpisha Dk Slaa kuwania ubunge katika jimbo hilo kama akihitaji.

Nasari ambaye amerejea hivi karibuni mjini Arusha akitokea nchini Marekani, leo anatarajiwa kuchukua fomu rasmi ili kuwania nafasi hiyo kupitia Chadema.

"Nimesikia maoni kupitia mitandao na wadau wakimuomba Dk Slaa kugombea, hili ni jambo jema kwetu kwani wananchi wanajua jimbo hili tunashinda Chadema na kama Dk (Slaa) akitaka kugombea dekomrasia ya chama chetu itafanya kazi, kwani kikubwa tunataka ushindi,"alisema Nasari.

Nasari aliyewahi kuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) kati ya 2008 na 2009 alipohitimu shahada ya Sayansi ya Jamii katika masuala ya utengenezaji Sera na Utawala, alisema ana imani Chadema kitashinda Arumeru.

"Nilikuwa Marekani kikazi na sasa nimerejea kama ulivyoshuhudia watu wengi wananiunga mkono na tayari wamenichangia Sh 11milioni za kampeni na magari manane," alisema Nasari.

Mgombea huyo ambaye tayari ametangaza kuacha kazi katika shirika la Kimarekani la Foundation For Tomorrow  ili kujikita kwenye uchaguzi huo, alisema wakazi wa Arumeru Mashariki wanahitaji mwakilishi sahihi ambaye anaweza kuwatetea katika kuinua uchumi wao.

Hata hivyo, alisema tayari amepata taarifa za Dk Slaa kutoa tamko kuwa hawezi kushiriki katika uchaguzi huo, kwa kuzingatia kuwa sio mkazi wa Meru na pia hana nia ya kugombea kiti hicho.

"Nategemea Dk Slaa na viongozi wengine wa kitaifa, wakiwapo wabunge, marafiki zangu wa vyuo vikuu na wengine wengi tutakuwa nao Arumeru kuhakikisha Chadema inashinda,"alisema Nasari.

Hadi  kufikia jana, kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema Mkoa wa Arusha (Bavicha),  Ephata Nanyaro,  wanachama waliokuwa wamechukua fomu ni Yohane Kimuto, Samweli Chami na Rebecca Mwingisha na leo Nasari atakuwa mwanachama wa tatu.

"Tunatarajia wanachadema wengi zaidi watajitokeza katika siku hizi zilizobaki ili kuchukuwa fomu na kurejesha mapema,"alisema Nanyaro.

Mgombea CCM alalamikia rushwa
Katika hatua nyingine, Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM katika Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Elirehema Kaaya ambaye pia ni afisa wa mifugo mkoani Mwanza, amekitaka chama hicho kukemea kampeni za fedha ndani ya chama katika uchaguzi huo.

Kaaya ambaye pia aligombea jimbo hilo katika uchaguzi uliopita na kushindwa katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema wakazi wa Arumeru hawahitaji mgombea wa CCM ambaye anapata nafasi hiyo kwa kutumia fedha.

"Arumeru wanataka mtu wa kuwasemea matatizo yao mjengoni (bungeni) na sio mtu anayetumia fedha kupata ubunge na mimi naomba chama kikemee na kukomesha matumizi ya fedha,"alisema Kaaya.

Akizungumzia maombi hayo, Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru Edson  Lihweuli alionya mgombea yoyote ambaye atabainika kujihusisha na vitendo vya rushwa au kukiuka taratibu atachukuliwa hatua.

Lihweuli alisema wagombea wote ambao wamechukua fomu, wamekuwa wakipewa taratibu hizo ili kuhakikisha uchaguzi ndani ya chama hicho unakwenda vizuri.                     

Wakati huohuo, Mkuu wa shule ya Sekondari ya Leguruki inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Mwalimu  Athony Msami jana alijitokeza kuchukua fomu na kufanya wagombea wa chama hicho wanaomba ridhaa ya chama kufikia  sita.Wengine  waliokuwa wamechukuwa fomu  ni Sioi Sumari, mtoto wa aliyekuwa mbunge Jeremiah Sumari, William Ndeoya Sarakikya, Elipokea Urio, Elishiria Kaaya na Elirehema Kaaya.
 Wakati kada huyo wa CCM akichukua fomu, juzi jioni Mkurugenzi wa kituo cha Mikutano cha Arusha(AICC), Elishiria Kaaya alirejesha fomu na kueleza kuwa anagombea ili kutekeleza ilani kwa kushughulikia matatizo ya wananchi wa Meru.

Kaaya ambaye pia aligombea uchaguzi uliopita na kuangushwa katika kura za maoni na Marehemu Sumari, alisema miongoni mwa mambo ambayo atayasimamia ni kuhakikisha anashirikiana na wananchi kukabiliana na matatizo ya upatikanaji maji, barabara, huduma za afya na masuala ya elimu.

Takukuru yaanza kazi
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Arusha imekutana na wagombea waliojitokeza kuchukua fomu katika uchaguzi huo na kuwaonya kutojihusisha na rushwa pia kuwataka waheshimu sheria za gharama za uchaguzi.

 Takukuru pia imetamka kwamba tayari imeshashaanza kupokea malalamiko mbalimbali ya makada wa vyama tofauti vya siasa wilayani humo, kujihusisha na vitendo vya kutoa na kupokea rushwa na kwamba madai hayo yameanza kufanyiwa kazi.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Takukuru mkoani Arusha, Mbengwa Kasumambuto imesema katika kujipanga kukabiliana na rushwa katika uchaguzi huo taasisi hiyo imekutana na wagombea wote wa vyama hivyo kwa lengo la kuwatahadharisha.

“Katika kujipanga na uchaguzi wa Arumeru kwanza tumewaita wagombea ambao wameshajitokeza hadi sasa pamoja na viongozi wa vyama vyao, lengo ni kuwatahadharisha na kuwataka waheshimu sheria ya uchaguzi,”alisema Kasumambuto.

Wanafunzi wanane wadaiwa kumbaka mwalimu kwa zamu

Mwandishi Wetu, Bagamoyo
 WANAFUNZI wanane wa Shule ya Sekondari Bagamoyo wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bagamoyo kujibu tuhuma za kumbaka mwalimu wao kwa zamu.

Katika kesi hiyo iliyojaza umati mkubwa wa wakazi wa eneo hilo, imedaiwa kuwa wanafunzi hao walimbaka mwalimu huyo kwa zamu na kumsababishia maumivu makali.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, William Mwantela alimwambia Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Said Mkasiwa kuwa wanafunzi hao walitenda kosa hilo Januari 16 mwaka huu katika mazingira ya shule hiyo.

Aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Emmanuel Antoni, Fadhili Nassoro, Nassa Yohana, Benjamini Mhina, Yusuph Timothy, Frank Jackson, Frank Kanya na Hamisi Timbwa.
 
Mwendesha mashtaka huyo alidai mahakamani hapo kuwa tukio hilo lilitokea shuleni hapo Januari 16 mwaka huu majira ya saa 9:00 jioni.

Hata hivyo, watuhumiwa hao wote walikana shtaka na kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 29 mwaka huu baada ya mwendesha mashtaka huyo kudai kuwa ushahidi haujakamilika.

Awali kabla ya kuahirisha kesi hiyo upande wa utetezi ulimwomba hakimu kuruhusu dhamana na hakimu aliruhusu akitaka kila mmoja adhaminiwe na mtu mmoja mwenye hati na kitambulisho ambaye atasaini hati ya dhamana ya Sh2milioni.

Washitakiwa watatu walifanikiwa kutimiza masharti hayo ya dhamana na wako nje, lakini wengine watatano wameshindwa na kupelekwa rumande hadi kesi hiyo itakapotajwa tena siku iliyopangwa.