NJOMBE

NJOMBE

Thursday, February 2, 2012

CCM waweka kambi karibu na CHADEMA

WAKATI kampeni za vyama mbalimbali zikiwa zinaendelea katika Jimbo la Uzini, Visiwani Zanzibar za kumsaka mwakilishi wa jimbo hilo, Chama cha Mapinduzi (CCM), nacho kilihamishia ngome yake hatua chache kutoka ilipo ngome ya CHADEMA.
Mwandishi wetu alishuhudia makada wa chama hicho wengine wakiwa wamevalia sare za CCM majira ya saa moja jioni wakiwa wanashusha vyombo na vyakula mbalimbali kutoka katika gari.
Mmoja wa wakazi wa Uzini, aliliambia Tanzania Daima kuwa kutokana na ukaribu wa kambi hizo mbili kuna hatari kubwa ya kuwapo kwa vurugu baina ya wafuasi wa vyama hivyo.
“Hawa jamaa ni sawa na Simba na Yanga, naliomba Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi eneo hili kwani wakati wowote mambo yanaweza kubadilika,” alisema.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare, alisema uamuzi wa CCM kukaa karibu na kambi ya chama hicho si mzuri na unaonyesha walivyo wachokozi.
Lwakatare alisema chama chao kimejipanga vilivyo kwa lolote litakalotokea na kuwaonya CCM kuwa wasithubutu kuanzisha fujo na Jeshi la Polisi kuwa macho kwa kuwapo dalili za uchokozi za CCM.

No comments:

Post a Comment