NJOMBE

NJOMBE

Friday, August 31, 2012

Kivumbi Uefa Champion League 2012/2013

Champions League

 Group A


Position Team Played Goal Difference Points

Group B


Position Team Played Goal Difference Points

Group C


Position Team Played Goal Difference Points
1 AC Milan 0 0 0
2 Anderlecht 0 0 0
3 Malaga 0 0 0
4 Zenit St P'sbg 0 0 0

Group D


Position Team Played Goal Difference Points

Group E


Position Team Played Goal Difference Points

Group F


Position Team Played Goal Difference Points

Group G


Position Team Played Goal Difference Points

Group H


Position Team Played Goal Difference Points
1 Braga 0 0 0
2 CFR Cluj-Napoca 0 0 0
3 Galatasaray 0 0 0
4 Man Utd 0 0 0
1 Barcelona 0 0 0
2 Benfica 0 0 0
3 Celtic 0 0 0
4 Spartak Moscow 0 0 0
1 BATE Borisov 0 0 0
2 Bayern Munich 0 0 0
3 Lille 0 0 0
4 Valencia 0 0 0
1 Chelsea 0 0 0
2 FC Nordsjaelland 0 0 0
3 Juventus 0 0 0
4 Shakhtar Donetsk 0 0 0
1 Real Madrid 0 0 0
2 Ajax 0 0 0
3 Borussia Dortmund 0 0 0
4 Man City 0 0 0
1 Arsenal 0 0 0
2 Montpellier 0 0 0
3 Olympiakos 0 0 0
4 Schalke 04 0 0 0
1 Din Zagreb 0 0 0
2 Dynamo Kiev 0 0 0
3 FC Porto 0 0 0
4 Paris SG 0 0 0

Thursday, August 30, 2012

Ngoma nzito Polisi


•  Wadaiwa kumfanyia mtoto unyama wa kutisha Manyara

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kutokana na kujirudiarudia kwa mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola, Rais Jakaya Kikwete, anapaswa kuingilia kati kuunda tume huru ili kuwezesha uchunguzi wa kina.
Hata hivyo, wakati CHADEMA ikitaka tume huru ya kuchunguza matukio hayo likiwemo lile la kuuawa kwa kijana Ally Hassan Singano maarufu kama Zona katika maadamano yao juzi, Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, limejivua lawama za mauaji hayo.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, alisema wanapinga kauli za serikali, Jeshi la Polisi na CCM zenye kulipotosha taifa kuhusu mashambulizi na mauaji yanayoelezwa kufanywa na askari mkoani Morogoro.
Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, alisema kuwa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani juzi, Dk. Emmanuel Nchimbi zina mwelekeo wa kulilinda Jeshi la Polisi, ambalo askari na maofisa wake ni sehemu ya watuhumiwa wa mauaji badala ya kuwezesha ukweli kuthibitika na hatua kuchukuliwa kwa wahusika.
“Ikumbukwe kuwa Agosti 27 mwaka huu, polisi mkoani Morogoro walifyatua risasi za moto na kupiga mabomu ya machozi wananchi na wanachama wa CHADEMA waliokuwa wamejikusanya kwa ajili ya kuelekea kwenye mkutano halali, na kusababisha kifo cha raia mmoja asiye na hatia na kujeruhi wengine wawili,” alisema.
Alisema kwa mauaji hayo na mengine katika maeneo mbalimbali nchini, Serikali ya CCM kupitia vyombo vya dola inaendelea kukiuka ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatambua kwamba uhai ni haki ya msingi wa raia wote.
Mnyika alibainisha kuwa, hawakubaliani na hatua zilizochukuliwa na serikali mpaka sasa kuhusu tukio husika pamoja na maelezo yaliyotolewa na Waziri Nchimbi juzi, ambayo alidai kwa sehemu kubwa yametokana na taarifa zisizo za kweli kutoka polisi.
“CHADEMA haina imani na timu iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi kuchunguza tuhuma za askari kufyatua risasi na mabomu ya machozi na kusababisha mauaji kwa kuwa tayari serikali na jeshi hilo wametoa maelezo yenye kutofautiana kwa kiwango kikubwa,” alisema.
Kwamba wakati serikali na polisi wakisema kuwa marehemu alikutwa umbali wa mita 300 na kupelekwa hospitali na wasamaria wema, mashuhuda wameeleza wazi kuwa askari walifika jirani na eneo lake na ofisa mmoja akaonesha ishara, na ndipo mabomu ya machozi na risasi za moto zikafyatuliwa na mojawapo kumpata na kudondoka.
Mnyika alidai kuwa mashahidi wote waliohojiwa wanaeleza kwamba bunduki ya polisi ndiyo ilielekezwa na kufyatuliwa kwa marehemu, maelezo pekee yanayotofautiana ni kuwa baadhi wameeleza kuwa ni bunduki ya risasi za moto na wengine wameeleza kuwa ni bunduki ya kufyatulia mabomu ya machozi.
Aliongeza kuwa sababu zilizotolewa na serikali kuwa polisi walizuia maandamano ya CHADEMA mkoani Morogoro kwa sababu ya sensa ya watu na makazi si za kweli kwa vile sababu pekee zilizotolewa ni ufinyu wa barabara na kuwa yalipangwa siku ya kazi.
Kwa mujibu wa Mnyika, ushahidi wa suala hili ni barua ya Jeshi la Polisi ya Agosti 23, 2012 yenye Kumb. Na. MOR/A.25/1/VOL.II/202 na kwamba polisi mkoani Morogoro ndio waliacha kuheshimu utawala wa sheria na makubaliano yaliyofikiwa baada ya mazungumzo ya pande zote.
“Kwa kuzingatia utofauti mkubwa baina ya maelezo yanayotolewa na serikali na Jeshi la Polisi kuhusu matukio husika na ukweli halisi ulivyotokea, CHADEMA kinasisitiza kuwa uchunguzi huru ufanyike kwa mujibu wa sheria ya uchunguzi wa vifo sura ya 24 ya sheria za Tanzania,” alisisitiza.
Wajitetea Moro
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alisema kuwa matokeo ya uchunguzi wa tukio hilo, yalionesha kwamba jeraha lililokuwa kichwani kwa marehemu lilitokana na kugongwa na kitu kizito kilichorushwa na si risasi.
Alisema kuwa uchunguzi huo ulifanywa na madaktari wawili wa mkoani humo pamoja na Dk. Ahmed Makata kutoka jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwanasheria wa CHADEMA, Aman Mwaipaya na baadhi ya askari.
Kamanda Shilogile alisema kuwa baada ya matokeo hayo ya daktari, polisi sasa wanaendelea na uchunguzi wa kubaini kitu hicho kilichorushwa na kusababisha kifo cha kijana huyo.
Alisema kuwa baadaye Jeshi la Polisi litachukua hatua za kisheria kwa askari ama mtu mwingine atakayebainika kuwa alirusha kitu hicho, ikiwa ni pamoja na kumkamata kiongozi wa CHADEMA aliyechochea maandamano hayo yaliyozua vurugu.
Kamanda Shilogile alisema kuwa ili kubaini hayo yote, serikali imeunda tume ya kuchunguza na kwamba inayoundwa na askari polisi na watu wengine ambao watasaidia kukamilisha uchunguzi huo.
Aliongeza kuwa tume hiyo ambayo tayari imeshafika mkoani Morogoro itatafuta maelezo na ushahidi kutoka kwa watu mbalimbali walioshuhudia tukio hilo, wakiwemo wanahabari na hivyo kuwaomba wote watakaohitajika kutoa ushirikiano.
Kuhusu majeruhi Hashimu Seif aliyejeruhiwa mguu katika vurugu hizo, Shilogile alisema kuwa uchunguzi umebaini kuwa alijeruhiwa na bomu lililomuangukia mguuni na kwamba anaendelea vizuri ikiwa bado yuko hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi.
Wadaiwa kumtesa mtoto
Katika hatua nyingine jeshi hilo Mkoa wa Manyara, limeingia katika kashfa nzito likidaiwa kumpiga na kumuumiza vibaya mtoto wa kiume, Kadogoo Kalanga (16), ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Selina kwenye chumba cha uangaliazi maalumu (ICU) akiwa hajitambui.
Mtoto huyo ambaye taarifa za polisi juu ya kilichompata zinatofautiana, yuko mahututi akiwa amevimba sehemu za siri na nyuma ya kichwa (kichogoni).
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Akili Mpwapwa alisema kuwa mtoto huyo alipatwa na hali hiyo baada ya kufikishwa kwenye kituo cha polisi cha Orkasumeti wilayani Simanjiro kwa tuhuma za wizi wa mbuzi wawili na kupandisha mori, na hivyo kujipigapiga chini hali iliyomsababishia kupoteza fahamu.
Hata hivyo, maelezo yake yanapingana na polisi waliompeleka mtoto huyo kwenye kituo cha afya Orkasumeti, ambao waliwaeleza madaktari kuwa alipata ajali ya pikipiki.
Daktari aliyempokea mtoto huyo kituoni hapo, aliyejitambilisha kwa jina moja la Ester, alimweleza mwandishi wa habari juzi kwa njia ya simu kuwa, mtoto huyo alifikishwa hapo Jumatatu wiki hii na askari ambao walimweleza kuwa alipata ajali ya pikipiki.
Alisema kuwa walimpa huduma ya kwanza, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo ya kutojitambua, walishindwa kubaini anaumwa wapi, hivyo siku iliyofuata akashaurina na madaktari wenzake wakaamua kumpa rufaa kwenda hospitali yenye vifaa kwa ajili ya vipimo zaidi.
Kamanda Mpwapwa alipoelezwa kuwa taarifa yake inatofautiana na ile ya askari wake kwenye kituo cha afya, aliendelea kusisitiza kuwa taarifa anazotoa ni zile alizopewa na Mkuu wa Polisi (OCD) wa Wilaya ya Simanjiro, na kwamba kama inatofautiana na nyingine hilo halimuhusu.
“Maelezo ninayokupa mimi ni yale niliyopewa na OCD wangu, kama kuna “contradiction” (mkanganyiko) kati ya taarifa niliyopewa na ambayo imetolewa mahali pengine hilo si tatizo langu,” alisema.
Naye mama wa mtoto huyo, Paulina Kalanga, aliwaeleza waandishi wakati akisubiri mtoto wake apatiwe matibabu kwenye hospitali ya Selian kuwa, alipata taarifa kwamba Kadogoo yuko kituo cha afya saa tano asubuhi ya Jumatatu na alipofuatilia alimkuta akiwa hajitambui.
Alisema madaktari walimweleza kuwa mtoto huyo alipelekwa hapo na askari polisi watatu na alipomkagua akishirikiana na ndugu zake, walibaini kuwa ameumizwa vibaya sehemu za siri ambazo  zimechubuka na kuvimba, huku kaptula aliyokuwa ameivaa ikiwa imelowa mkojo na kuchanika eneo la katikati.
Paulina aliongeza kuwa, tangu wakati huo hadi jana asubuhi mtoto huyo hajaongea zaidi ya kuzungusha kichwa sana wakati fulani, hali inayomlazimu amsaidie kukishikilia kuepuka asijiumize.
Alisema kuwa mtoto huyo anaonekana kuumia kila anapoguswa maeneo ya nyuma ya kichwa, kwenye mbavu na kwamba anahisi mfumo wake wa haja ndogo huenda umepata tatizo kwani tangu Jumatatu hapati choo kidogo licha ya kuwekewa chupa kadhaa za maji ya kumwongeza nguvu mwilini.
Kadogoo alilazimika kuhamishiwa katika Hospitali ya Agha Khan ya mjini Arusha kwa kutumia gari la wagonjwa la Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro lenye namba za usajili SM 5004 ili kufanyiwa kipimo cha kichwa, CIT SCAN.
Mama mzazi wa mtoto huyo pamoja na ndugu wengine waliokusanyika hospitalini hapo, walieleza masikitiko yao juu ya kitendo hicho cha kinyama wakidai mpaka sasa polisi imeshindwa kuwapa namba ya taarifa iliyofunguliwa kwao (RB) kuhusu kosa linalomkabili Kadodoo.
Chanzo Mtanzania daima

Ngoma nzito Polisi
•  Wadaiwa kumfanyia mtoto unyama wa kutisha Manyara

na Waandishi wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kutokana na kujirudiarudia kwa mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola, Rais Jakaya Kikwete, anapaswa kuingilia kati kuunda tume huru ili kuwezesha uchunguzi wa kina.
Hata hivyo, wakati CHADEMA ikitaka tume huru ya kuchunguza matukio hayo likiwemo lile la kuuawa kwa kijana Ally Hassan Singano maarufu kama Zona katika maadamano yao juzi, Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, limejivua lawama za mauaji hayo.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, alisema wanapinga kauli za serikali, Jeshi la Polisi na CCM zenye kulipotosha taifa kuhusu mashambulizi na mauaji yanayoelezwa kufanywa na askari mkoani Morogoro.
Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, alisema kuwa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani juzi, Dk. Emmanuel Nchimbi zina mwelekeo wa kulilinda Jeshi la Polisi, ambalo askari na maofisa wake ni sehemu ya watuhumiwa wa mauaji badala ya kuwezesha ukweli kuthibitika na hatua kuchukuliwa kwa wahusika.
“Ikumbukwe kuwa Agosti 27 mwaka huu, polisi mkoani Morogoro walifyatua risasi za moto na kupiga mabomu ya machozi wananchi na wanachama wa CHADEMA waliokuwa wamejikusanya kwa ajili ya kuelekea kwenye mkutano halali, na kusababisha kifo cha raia mmoja asiye na hatia na kujeruhi wengine wawili,” alisema.
Alisema kwa mauaji hayo na mengine katika maeneo mbalimbali nchini, Serikali ya CCM kupitia vyombo vya dola inaendelea kukiuka ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatambua kwamba uhai ni haki ya msingi wa raia wote.
Mnyika alibainisha kuwa, hawakubaliani na hatua zilizochukuliwa na serikali mpaka sasa kuhusu tukio husika pamoja na maelezo yaliyotolewa na Waziri Nchimbi juzi, ambayo alidai kwa sehemu kubwa yametokana na taarifa zisizo za kweli kutoka polisi.
“CHADEMA haina imani na timu iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi kuchunguza tuhuma za askari kufyatua risasi na mabomu ya machozi na kusababisha mauaji kwa kuwa tayari serikali na jeshi hilo wametoa maelezo yenye kutofautiana kwa kiwango kikubwa,” alisema.
Kwamba wakati serikali na polisi wakisema kuwa marehemu alikutwa umbali wa mita 300 na kupelekwa hospitali na wasamaria wema, mashuhuda wameeleza wazi kuwa askari walifika jirani na eneo lake na ofisa mmoja akaonesha ishara, na ndipo mabomu ya machozi na risasi za moto zikafyatuliwa na mojawapo kumpata na kudondoka.
Mnyika alidai kuwa mashahidi wote waliohojiwa wanaeleza kwamba bunduki ya polisi ndiyo ilielekezwa na kufyatuliwa kwa marehemu, maelezo pekee yanayotofautiana ni kuwa baadhi wameeleza kuwa ni bunduki ya risasi za moto na wengine wameeleza kuwa ni bunduki ya kufyatulia mabomu ya machozi.
Aliongeza kuwa sababu zilizotolewa na serikali kuwa polisi walizuia maandamano ya CHADEMA mkoani Morogoro kwa sababu ya sensa ya watu na makazi si za kweli kwa vile sababu pekee zilizotolewa ni ufinyu wa barabara na kuwa yalipangwa siku ya kazi.
Kwa mujibu wa Mnyika, ushahidi wa suala hili ni barua ya Jeshi la Polisi ya Agosti 23, 2012 yenye Kumb. Na. MOR/A.25/1/VOL.II/202 na kwamba polisi mkoani Morogoro ndio waliacha kuheshimu utawala wa sheria na makubaliano yaliyofikiwa baada ya mazungumzo ya pande zote.
“Kwa kuzingatia utofauti mkubwa baina ya maelezo yanayotolewa na serikali na Jeshi la Polisi kuhusu matukio husika na ukweli halisi ulivyotokea, CHADEMA kinasisitiza kuwa uchunguzi huru ufanyike kwa mujibu wa sheria ya uchunguzi wa vifo sura ya 24 ya sheria za Tanzania,” alisisitiza.
Wajitetea Moro
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alisema kuwa matokeo ya uchunguzi wa tukio hilo, yalionesha kwamba jeraha lililokuwa kichwani kwa marehemu lilitokana na kugongwa na kitu kizito kilichorushwa na si risasi.
Alisema kuwa uchunguzi huo ulifanywa na madaktari wawili wa mkoani humo pamoja na Dk. Ahmed Makata kutoka jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwanasheria wa CHADEMA, Aman Mwaipaya na baadhi ya askari.
Kamanda Shilogile alisema kuwa baada ya matokeo hayo ya daktari, polisi sasa wanaendelea na uchunguzi wa kubaini kitu hicho kilichorushwa na kusababisha kifo cha kijana huyo.
Alisema kuwa baadaye Jeshi la Polisi litachukua hatua za kisheria kwa askari ama mtu mwingine atakayebainika kuwa alirusha kitu hicho, ikiwa ni pamoja na kumkamata kiongozi wa CHADEMA aliyechochea maandamano hayo yaliyozua vurugu.
Kamanda Shilogile alisema kuwa ili kubaini hayo yote, serikali imeunda tume ya kuchunguza na kwamba inayoundwa na askari polisi na watu wengine ambao watasaidia kukamilisha uchunguzi huo.
Aliongeza kuwa tume hiyo ambayo tayari imeshafika mkoani Morogoro itatafuta maelezo na ushahidi kutoka kwa watu mbalimbali walioshuhudia tukio hilo, wakiwemo wanahabari na hivyo kuwaomba wote watakaohitajika kutoa ushirikiano.
Kuhusu majeruhi Hashimu Seif aliyejeruhiwa mguu katika vurugu hizo, Shilogile alisema kuwa uchunguzi umebaini kuwa alijeruhiwa na bomu lililomuangukia mguuni na kwamba anaendelea vizuri ikiwa bado yuko hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi.
Wadaiwa kumtesa mtoto
Katika hatua nyingine jeshi hilo Mkoa wa Manyara, limeingia katika kashfa nzito likidaiwa kumpiga na kumuumiza vibaya mtoto wa kiume, Kadogoo Kalanga (16), ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Selina kwenye chumba cha uangaliazi maalumu (ICU) akiwa hajitambui.
Mtoto huyo ambaye taarifa za polisi juu ya kilichompata zinatofautiana, yuko mahututi akiwa amevimba sehemu za siri na nyuma ya kichwa (kichogoni).
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Akili Mpwapwa alisema kuwa mtoto huyo alipatwa na hali hiyo baada ya kufikishwa kwenye kituo cha polisi cha Orkasumeti wilayani Simanjiro kwa tuhuma za wizi wa mbuzi wawili na kupandisha mori, na hivyo kujipigapiga chini hali iliyomsababishia kupoteza fahamu.
Hata hivyo, maelezo yake yanapingana na polisi waliompeleka mtoto huyo kwenye kituo cha afya Orkasumeti, ambao waliwaeleza madaktari kuwa alipata ajali ya pikipiki.
Daktari aliyempokea mtoto huyo kituoni hapo, aliyejitambilisha kwa jina moja la Ester, alimweleza mwandishi wa habari juzi kwa njia ya simu kuwa, mtoto huyo alifikishwa hapo Jumatatu wiki hii na askari ambao walimweleza kuwa alipata ajali ya pikipiki.
Alisema kuwa walimpa huduma ya kwanza, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo ya kutojitambua, walishindwa kubaini anaumwa wapi, hivyo siku iliyofuata akashaurina na madaktari wenzake wakaamua kumpa rufaa kwenda hospitali yenye vifaa kwa ajili ya vipimo zaidi.
Kamanda Mpwapwa alipoelezwa kuwa taarifa yake inatofautiana na ile ya askari wake kwenye kituo cha afya, aliendelea kusisitiza kuwa taarifa anazotoa ni zile alizopewa na Mkuu wa Polisi (OCD) wa Wilaya ya Simanjiro, na kwamba kama inatofautiana na nyingine hilo halimuhusu.
“Maelezo ninayokupa mimi ni yale niliyopewa na OCD wangu, kama kuna “contradiction” (mkanganyiko) kati ya taarifa niliyopewa na ambayo imetolewa mahali pengine hilo si tatizo langu,” alisema.
Naye mama wa mtoto huyo, Paulina Kalanga, aliwaeleza waandishi wakati akisubiri mtoto wake apatiwe matibabu kwenye hospitali ya Selian kuwa, alipata taarifa kwamba Kadogoo yuko kituo cha afya saa tano asubuhi ya Jumatatu na alipofuatilia alimkuta akiwa hajitambui.
Alisema madaktari walimweleza kuwa mtoto huyo alipelekwa hapo na askari polisi watatu na alipomkagua akishirikiana na ndugu zake, walibaini kuwa ameumizwa vibaya sehemu za siri ambazo  zimechubuka na kuvimba, huku kaptula aliyokuwa ameivaa ikiwa imelowa mkojo na kuchanika eneo la katikati.
Paulina aliongeza kuwa, tangu wakati huo hadi jana asubuhi mtoto huyo hajaongea zaidi ya kuzungusha kichwa sana wakati fulani, hali inayomlazimu amsaidie kukishikilia kuepuka asijiumize.
Alisema kuwa mtoto huyo anaonekana kuumia kila anapoguswa maeneo ya nyuma ya kichwa, kwenye mbavu na kwamba anahisi mfumo wake wa haja ndogo huenda umepata tatizo kwani tangu Jumatatu hapati choo kidogo licha ya kuwekewa chupa kadhaa za maji ya kumwongeza nguvu mwilini.
Kadogoo alilazimika kuhamishiwa katika Hospitali ya Agha Khan ya mjini Arusha kwa kutumia gari la wagonjwa la Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro lenye namba za usajili SM 5004 ili kufanyiwa kipimo cha kichwa, CIT SCAN.
Mama mzazi wa mtoto huyo pamoja na ndugu wengine waliokusanyika hospitalini hapo, walieleza masikitiko yao juu ya kitendo hicho cha kinyama wakidai mpaka sasa polisi imeshindwa kuwapa namba ya taarifa iliyofunguliwa kwao (RB) kuhusu kosa linalomkabili Kadodoo.

Waziri wa kawi Nigeria ajiuzulu

 
Waziri wa kawi Barth Nnaji
Waziri wa kawi nchini Nigeria, Barth Nnaji amejiuzulu baada ya kuhusishwa na kashfa ya kandarasi ya uzalishaji umeme.
Serikali ya Nigeria iko katika harakati za kubinafsisha makampuni yake katika juhudi za kumaliza tatizo kubwa la upungufu wa umeme.
Msemaji wa bwana Nnaji alisema kuwa waziri huyo amelimbikiziwa makosa hayo visivyo.
Ni nadra kwa wanasiasa nchini Nigeria ambako ufisadi ni tatizo kubwa kujiuzulu baada ya kuhusishwa na kashfa yoyote kwa mujibu wa wadadisi wa siasa za nchi hiyo.
Rais Goodluck Jonathan,aliyeahidi kupambana na tatizo la upungufu wa umeme alipoingia madarakani mwaka 2010, alisema kuwa anakubali kujiuzulu kwa bwana Nnaji.
'Maslahi ya kibinafsi'
Sekta ya kawi Nigeria
Hakuna yeyote aliyetoa maelezo kuhusu hatau ya bwana Nnaji kujiuzulu, sio rais Goodluck wala Nnaji mwenyewe, lakini inakuja baada ya magazeti ya Nigeria kuripoti kuwa waziri huyo alikuwa na uhusiano na kampuni ambayo ilitaka kununua mali ya serikali ambayo ilikua inauzwa.
Msemaji wa Nnaji alithibitisha kuwa alikuwa na maslahi katika mojawapo ya makampuni yaliyotoa maombi yao ya kununua mali hizo.
Aliongeza kuwa bwana Nnaji hakufurahia hata kidogo kuhusu tuhuma hizo na kwamba alionelea ni bora kwake kuendelea na shughuli zake za binafsi.
Mwandisi wa BBC Fidelis Mbah anasema kuwa tangu kuingia ofisini mwezi Julai mwaka 2011,bwana Nnaji amekabiliwa na changamoto kubwa kwa sababu ya mageuzi anayojaribu kuleta.
Amekuwa akijaribu kukabiliana na ufisadi na utenda kazi duni wa sekta ya kawi , hatua ambayo imeghadhabisha wafanyakazi wa umma ambao huenda wakapoteza kazi zao.
Kisima cha mafuta nchini Nigeria

Wenye biashara za kifahari ambazo huingiza nchini humo majenereta kutoka nje pia yamemshtumu mipango yake ya kutaka kuuza makampuni sita ya kuuza jenereta hizo kama mpango wa kubinafsisha sekta ya kawi.
Nigeria ndio nchi inayozalisha pakubwa mafuta pamoja na kuwa na visima vingi vya gesi.

Assad ahitaji muda zaidi kushinda vita

Rais Bashr Al Assad
Rais wa Syria Bashar al-Assad amesema kuwa serikali yake inahitaji muda wa ziada kuweza kushinda vita dhidi ya waasi nchini humo.
Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni kinachounga mkono serikali ya Assad,
rais huyo pia alipuuza tamko kuwa haiwezekani kutenga maeneo ya kutolea misaada katika maeneo ya mipaka nchini humo,
Wanaharakati wa upinzani wanadai kuwa jeshi limefanya mashambulizi katika maeneo mengi ya nchi hiyo kutaka kudhibiti maeneo yaliyotekwa na waasi.
Mapambano makali yaliripotiwa kutokea siku ya Jumanne katika mji mkuu Damascus, Aleppo na mkoa wa kaskazini masharibi wa Idlib.
Bwana Assad amesema kuwa serikali yake iko kwenye vita ndani na nje ya nchi.
"bila shaka tunahitaji muda zaidi kuweza kumaliza vita hivi katika njia inayofaa. Lakini ninachoweza kusema ka neno moja tu ni tunapiga hatua''. Bwana Assad alisema.
"hali kwa sasa angalau ni nzuri, lakini bado hatujafika mwisho. Hilo bila shaka linahitaji muda zaidi'' alisema Assad
''Maafisa wa ulinzi wanafanya kitendo ha ushujaa kwa kila hali. Lakini waasi hawataruhusiwa kueleza hofu wala hawataruhusiwa kiufanya hivyo.'' aliongeza rais Assad.
Kila mtu hapa nchini ana wasiwasi kuhusu hali ya nchi yetu, hilo ni jambo la kawaida.Ninawaambia wananchi wa Syria, mustakabali a nchi hii uko mikononi mwenu, wala sio mikononi mwa watu wengine''.
Rais aliwakejeli maafisa wakuu wa serikali na jeshi ambao wameasi serikali katika miezi ya hivi karibuni akisema kuwa hatua hiyo iliweza kuisafi serikali mwanzo na kisha nchi kwa ujumla.

Desmond Tutu asusia mkutano kwa sababu ya Blair


Desmond Tutu

Askofu mkuu Desmond Tutu amesusia warsha moja baada ya kukataa kushiriki warsha hiyo pamoja na waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.
Tutu ambaye ni mwanaharakati mkongwe wa amani, alisema kuwa hatua ya Blair kuunga mkono vita vya Iraq, haikubaliki kimaadili, na kuwa hapaswi kuwa na ushirikiano wowote na yeye.
Wawili hao walistahili kushiriki katika warsha ya siku moja kuhusu uongozi mjini Johannesburg, Afrika Kusini hapo kesho.
Waakilishi wa Blair walielezea masikitiko yao kwa hatua ya askofu kuamua kujioandoa kwenye mkutano wao.
Tutu, aliyepata tuzo la amani la Nobel mwaka 1984 kwa sababu ya kampeini yake ya amani wakati wa enzi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini alistahili kushirki mkutano kuhusu uongozi pamoja na bwana Blair.
Majeshi ya Marekani Iraq
Washiriki wengine ni pamoja na bingwa wa mchezo wa chess duniani ambaye pia ni mwanasiasa wa upinzani nchini Urusi, Garry Kasparov pamoja na afisaa mkuu mtendaji wa maduka ya Tesco Uingereza Sir Terry Leahy.
Katika taarifa iliyotolewa kutoka kwa ofisi ya bwana Tutu, " Askfo Tutu anaonelea kuwa hatua ya Blair kuunga mkono uvamizi wa Marekani nchini Iraq,kwa misingi hafifu na madai ambayo hayakuwahi kuthibitishwa sio jambo linalokubalika kimaadili.
"Kauli mbiu ya warsha hiyo ya uongozi ni maadili na uongozi. Na kwa muktadha huu, itakuwa si vizuri kwa Askofu mkuu kushiriki na Tony Blair kwenye warsha hiyo.'' ilisema taarifa hiyo.
Hata hivyo taarifa kutoka ofisi ya Blair iliyotolewa kujibu hatua ya Askofu, ilisema kuwa wawili wao hawakupangiwa kushiriki pamoja.
Taarifa hiyo iliongeza kuwa '' kuhusu swala la Iraq, wawili hao daima hawajawahi kukubaliana kuhusu kung'olewa mamlakani kwa Saddam hussein kwa nguvu , tofauti kama hizi ni nzuri katika mazingira ya demokrasia''
''Na ikiwa ni swala la maadili, hivi maajuzi kumeadhimishwa mauaji ya halaiki ya Halabja ambako maelfu ya watu waliuawa kwa siku moja kwa kumutumia silaha za sumu na kwamba kuhusu vita kati ya Iran na Iraq takriban watu milioni moja walifariki ikiwemo wale waliouawa kwa kemikali hizo za sumu. Kwa hivyo maamuzi haya daima hayawezi kuwa rahisi ukizingatia maadili na siasa.'' iliongeza taarifa hiyo.
Hatua ya Tutu kujiondoa kwa warsha hiyo inajiri huku chama kimoja cha kiisilamu nchini Afrika Kusini kikitangaza kupanga maandamano kupinga uwepo wa Balir kwenye warsha hiyo kwa sababu aliunga mkono vita vya Iraq.

Wednesday, August 29, 2012

USHER THE DRAMA BOY


Three Kings/WENN.com
Hivi karibuni Usher alikua na migogoro na mpenzi wake wa zamani tameka foster waliojaaliwa kupata watoto wawili, migogoro huo ulikua nani akae na watoto? maana kila mmoja alitoa sababu ya kutaka kuishi na watoto. usher alidai kuwa tameka is uncapable of raising the kids while tameka alisema usher hutumia drugs  mbele za watoto na yupo busy sana with clubbin hivyo hatwaangalia watoto kwa makini. baada ya court kuangalia malalamishi ya pande zote mbele imekubali usher akae na watoto muda mrefu na watashinda kwa tameka for few hours

Bangi inaathiri akili kwa vijana

Utafiti uliodumu muda mrefu umethibitisha kuwa vijana wanaovuta bangi wanadhuru akili zao, na huenda wakapoteza ufahamu na uwezo wa kukumbuka.
Vijana walioanza kutumia bangi hiyo wakiwa na chini ya miaka ishirini walionyesha matokeo mabaya zaidi katika mitihani na kuonyesha upungufu mkubwa katika akili zao.
Utafiti huu umefanyiwa takriban watu 1,000 nchini New Zealand.
Kikundi kimoja cha kimataifa, kilichofanya utafiti huo, kiligundua kuwa vijana walioanza kutumia bangi wakiwa chini ya umri wa miaka 18 wakati akili zao zikiwa bado zinakomaa, walipoteza uwezo wao wa kufahamu mambo haraka.
Mtaalamu wa maswala hayo nchini Uingereza, alisema kuwa huenda utafiti huo, ukafafanua kwa nini watu wanoatumia bangi hawana uelewa mzuri wa mambo.
Kwa zaidi ya miaka 20 , watafiti wameweza kuwafuatilia watu wanaotumia bangi kutoka eneo la
Dunedin nchini New Zealand.
Waliwachunguza walipokuwa watoto kabla ya hata kuanza kutumia bangi na kisha kuwachunguza mara kwa mara hadi walipofika miaka 38.
Kikundi hicho hata hivyo kilizingatia mambo kama utumiaji wa pombe na sigara pamoja na madawa mengine ya kulevya pamoja na maisha yao wakiwa wanafunzi.
Waligundua kuwa wale waliokuwa wanatumia bangi kwa muda mrefu, angalau mara nne kwa wiki kila mwaka na katika umri wao wa ujana, waliathrika kutokana na kupungukiwa akili.

Tuesday, August 28, 2012

Wanawake Togo wasusia ngono kudai Mageuzi


Isabelle Ameganvi anasema kususia ngono kutasaidia wanawake kusikika
Wanawake nchini Togo, wametakiwa kususia kitendo cha ndoa kuanzia Jumatatu wiki hii kama njia ya kushinikiza serikali kuleta mageuzi.
Kampeini hiyo yenye kauli mbiu ''Juhudi za kuokoa Togo'' imeanzishwa kwa ushirikiano na mashirika tisa ya kijamii pamoja na vyama saba vya upinzani pamoja na vyama vingine vya kijamii.
Kiongozi wa upinzani, Isabelle Ameganvi alisema kuwa kususia ngono huenda ndio itakuwa silaha inayofaa kuweza kuleta mageuzi ya kisiasa.
Muungano wa vyama hivyo pamoja na mashirika yasiyo ya kijamii unataka rais Faure Gnassingbe, ambaye familia yake imeshikilia madaraka kwa miaka mingi waweze kuondoka mamlakani.
"tuna njia nyingi za kuwashinikiza wanaume kuelewa tunachotaka sisi wanawake'' alisema bi Ameganvi, kiongozi wa tawi la wanawake la muungano huo.
Vurugu Togo
Alisema kuwa yeye ameweza kushawishiwa na mgomo sawa na huo nchini Liberia mwaka 2003,ambao walitumia njia ya kususia ngono kushinikiza amani.
"ikiwa wanaume watakataa kusikia kilio chetu, tutalazimika kufanya maandamano ambayo yatakuwa makali zaidi kuliko mbinu hii ya kususia ngono.'' aliongeza bi Ameganvi
Togo imekuwa ikiongozwa na familia moja kwa zaidi ya miaka arobaini.
Rais President Faure Gnassingbe alichukua mamlaka mnamo mwaka 2005 kufuatia kifo cha babake Gnassingbe Eyadema, aliyetawala Togo kwa miaka 38. Rais alichaguliwa kwa muhula mwingine mnamo mwaka 2010.
Mgomo huo ulitangazwa katika mkutano wa hadhara mnamo siku ya Jumamosi mjini Lome, na ambao ulihudhuriwa na maelfu ya watu.
Vurugu nchini Togo
Mkutano huo ulifanyika kupinga mabadiliko ya hivi karibuni yaliyofanywa ambayo wakereketwa wanasema kuwa yatarahisisha ushindi wa chama tawala cha Gnassingbe kuweza kwenye uchaguzi wa bunge utakaofanyika mwezi Oktoba.
Wanaharakati wanasema kuwa mgomo huo utashinikiza wanaume ambao hawajihusishi na mchakato wa kisiasa kuweza kuhakikisha malengo yake yanatimizwa ambayo ni pamoja na kukomeshwa kwa utawala wa rais usio na kikomo.
Mapema mwezi huu, waandamanaji wanaopinga utawala wa rais Gnassingbe walitawanywa na polisi kwa kutumia gesi ya kutoa machozi na wengine zaidi ya miamoja wakakamatwa.

Wakamatwa Mombasa sababu ya Rogo


Fojo zaendelea Mombasa kwa siku ya pili mfululizo
Watu 12 wamekamatwa na polisi kufuatia makabiliano kati ya polisi na vijana wanaofanya vurugu kufuatia kuuwawa kwa kiongozi wa kidini Sheikh Aboud Rogo siku ya jumatatu.
Katika siku ya pili ya vurugu hizo, wengi ya vijana hao wamekamatwa nje ya Msikiti Musa iliyo eneo la Majengo visiwani Mombasa.
Hata hivyo katika eneo moja polisi walilazimika kutumia risasi za mpira kuwatawanya vijana waliokuwa wakiwasha matairi barabarini na kufanya uporaji.
Bwana mmoja alichomwa kisu katika karakana yake na kulazimika kupewa huduma ya kwanza na wafuasi wa dhehebu la Jeshi la wokovu.
Na wakati Mombasa ikiwaka moto, wapiganaji wa Al shabaab wametuma ujumbe katika mtandao wao wakiwasihi waislamu wa kenya "wachukuwe kila hatua zinazostahili kulinda dini yao"
" Waislamu lazima wachukue sheria mikononi mwao, na wasimame kidete dhidi ya makafiri na kuchukua kila hatua kuilinda dini yao, heshima yao ,mali yao na maisha yao kutoka kwa maadui wa waislamu" , Al shabaab wamenukuliwa wakisema hayo katika taarifa yao.
Kiongozi huyo wa kidini Sheikh Aboud Rogo ,aliyepigwa risasi na kuuwa siku ya jumatatu alikuwa ametajwa na Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa kama mtua anayewasajili baadhi ya vijana wa Kenya wkenda kujiunga na wapiganaji wa Al Shabaab.
Sheikh Aboud Rogo pia anadaiwa kuwa alikuwa mfadhili wa kundi hilo la Al shabaab.

Wafungwa tisa wauawa nchini Gambia

Rais wa Gambia Yahya Jammeh
Wafungwa tisa wameuawa nchini Gambia licha ya wito kutoka kwa jamii ya kimataifa dhidi ya sera rasmi nchini humo ya kutekeleza hukumu zote za kunyongwa kwa wafungwa mwezi ujao.
Wafungwa hao, waliuawa kwa kupigwa risasi siku ya jumapili , kwa mujibu wa waziri wa mambo ya ndani.
Rais wa nchi hiyo, Yahya Jammeh aliahidi kuwauwa wafungwa wote arobaini na saba waliohukumiwa kunyongwa ifikapo katikati ya mwezi Septemba.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa ushirikiano na jamii ya kimataifa yameelezea wasiwai na kutoa wito kwa rais Jammeh kutotekeleza adhabu hiyo.
Shirika la kimataifa la Amnesty International, lilikemea sera hiyo wiki jana wakati lilipofichua kuwa vifo hivyo vilitekelezwa siku tatu zilizopita.
Wengi wa wafungwa wa Gambia ambao wamehukumiwa kunyongwa ni maafisa wakuu wa zamani pamoja na maafisa wa ngazi za juu wa kijeshi ambao wamekuwa wakifungwa kwa madai ya uhaini tangu mwaka
1994, wakati rais Jammeh alipoingia mamlakani kwa njia ya mapinduzi.
Mkuu wa sera ya kigeni katika muungano wa Ulaya, Catherine Ashton, ameitaka serikali ya Gambia kukoma kutekeleza hukumu ya kuwanyonga wafungwa mara moja.
Hotuba ya siku ya Eid
Mwanamke mmoja ni miongoni mwa wale walionyongwa kulingana na taarifa ya wizara ya mambo ya ndani. Baadhi ya makosa aliyopatikana na hatia nayo ni, mauaji, uhaini, biashara haramu ya madawa ya kulevya, ulanguzi wa watu na mengineyo. Yote hayo hukumu yake ikiwa kunyongwa.
Hukumu ya kunyongwa ilifutiliwa mbali na rais wa zamani, Dawda Jawara lakini ikarejeshwa mwaka 1995 pindi rais Jammeh alipochukua mamlaka.
"ifikapo kati kati ya mwezi ujao, wafungwa wote waliohukumiwa kunyongwa, hukumu zao zitakuwa zimetekelezwa. Hakuna namna ambavyo serikali yangu itaruhusu asilimia 99 ya watu wa nchi hii kuishi katika hofu ya wahalifu." alisema rais Jammeh katika hotuba ambayo ilipeperushwa moja kwa moja kuliptia runinga ya taifa tarehe kumi na tisa mwezi Agosti wakati wa sherehe ya siku ya Idd.
Kwa upande wake, rais wa Benin Benin, Thomas Boni Yayi, ambaye ndiye mwenyekiti wa muungano wa Afrika alituma waziri wake wa mambo ya nje nchini Gambai kutoa onyo kwa rais Jammeh dhidi ya kuendelea kutekeleza hukumu ya kunyongwa.

Hali ya hatari katika jimbo la Louisiana


Athari za kimbunga Isaac
Rais barack Obama ametangaza hali ya hatari katika jimbo la Louisiana nchini Marekani linalotishiwa na kimbunga Isaac. Kimbunga hicho kinatarajiwa kufika ardhini jioni ya leo ikiwa miaka saba tangu kutokea gharika la Katrina katika eneo la New Orleans.
Kwa sasa kimbunga Isaac kimetajwa kuwa bado ni tufani japo kinatarajiwa kushika kasi zaidi na kuwa kimbunga kamili la uharibifu mkubwa inapoelekea kuvuka ghuba ya Mexico.
Kimbunga kama hicho kwa jina Katrina, kiliwaua zaidi ya watu elfu moja mia nane mjini New Orleans mnamo agosti mwaka wa elfu mbili na tano.
Tangazo hilo la hali ya hatari litawezesha afisi za serikali kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya misaada baada ya kimbunga kupita.
Kimbunga hicho kinapiga miaka saba baada ya kimbunga kibaya zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Marekani cha Katrina kugonga Marekani.
Chama cha Republican kimelazimika kuchelewesha kongamano lake la kitaifa , mjini Tampa, Florida kumchagua rasmi mgombea wa urais kwa chama hicho atakayepambana na rais Barack Obama.
Kimbunga saac kiliwaua watu 24 nchini Haiti na katika Jamuhuri ya Dominica na pia kusababisha uharibifu mkubwa katika visiwa vya Caribbea.
Hapo jana, kituo cha kitaifa cha kutabiri vimbunga, kilionya kuwa huenda kimbunga hicho kikafikia daraja ya pili kikiambatana na mawimbi makali yenye kasi ya kilomita 160, kwa saa.
Rais Obama aliitikia wito wa jimbo la Louisiana kuitaja hali kuwa ya hatari, na kuwezesha jimbo hilo kupokea msaada wa kitaifa kupambana na hali.

Sunday, August 26, 2012

Mwana anga mkongwe wa Marekani afariki

Rais Obama ameongoza katika sifa na rambi-rambi zilizotolewa baada ya kifo cha Neil Armstrong, mwana anga wa kwanza kutua kwenye mwezi, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 82 kutokana na matatizo aliyopata baada ya upasuaji aliofanyiwa kwenye moyo.
Neil Armstrong
Mwenzake Armstrong katika safari ya kihistoria ya kwenda mwezini mwaka wa 1969 alikuwa Buzz Aldrin, ambaye alisema Armstrong alikuwa rubani na kamanda mahiri.
Familia ya Neil Armstrong imetoa wito kwa Wamarekani kuonesha heshima zao kwa kufuata mfano wake wa kutumika, kufanikiwa na bila ya majivuno.
Taarifa ya familia iliwaambia wale washabiki wake: "ukitembea nje usiku ukaona mwezi unakuchekea, mfikirie Neil na umkonyeze."

Wachimba migodi waanza kurudi kazini

Kampuni ya migodi iliyokuwa chanzo cha mgomo wa ghasia Afrika Kusini, Lonmin, inasema kuwa wafanyakazi wake zaidi wamerudi kwenye mgodi wa Marikana, karibu na Rustenberg.
Polisi nje ya mgodi wa Marikana wakati wa mgomo
Serikali ya Afrika Kusini imeteua tume ya majaji kuchunguza kilichotokea.
Lonmin inasema kuwa katika mgodi wa Eastern Shafts, huko Marikana, 57% ya wachimba migodi wako kazini Jumamosi.
Sehemu nyengine ya machimbo imefungwa kwa sababu ya mapumziko ya mwisho wa juma.
Kampuni inasema hali ni ya amani, na kwamba mazungumzo yanaendelea ili kushawishi wafanyakazi wote warudi kazini.
Lakini uchimbaji wa madini ya dhahabu nyeupe, platinum, ulisimamishwa kwenye mgodi huo zaidi ya majuma mawili yaliyopita kwa sababu ya mgomo, na bado kazi haikuanza.
Mazishi ya baadhi ya wachimba migodi waliokufa yamefanywa na mawaziri walihudhuria na kuahidi kuzisaidia familia za wachimba migodi hao.
Wakuu sasa wamethibitisha kuwa kati ya waliokufa, watano walikuwa wageni kutoka nchi za nje.

Gambia yaanza tena kunyonga wafungwa

Shirika la kimataifa la kutetea haki za kibinaadamu, Amnesty International, linasema limeambiwa kwamba Gambia imewanyonga wafungwa tisa kati ya 47 ambao wamehukumiwa kifo.
Rais wa Gambia, Yahya Jamme
Msemaji wa Amnesty, Lisa Sherman Nichols, aliiambia BBC kwamba wafungwa hao ni wa mwanzo kunyongwa nchini Gambia kwa miaka 29, na inasemekana alikuwako mwanamke kati yao, na wananchi watatu wa Senegal.
"Tumepata taarifa za kuaminika kuwa watu 9 walinyongwa jana usiku.
Nimezungumza na baadhi ya jamaa zao, ambao bila ya shaka wako kwenye majonzi, na wametuomba tuchukue hatua.
Wamegusia kuwa kuna wengine watanyongwa leo usiku.
Tunajaribu kuzitawanya habari hizi ulimwenguni na serikali ya Gambia inafaa kujua kuwa macho ya ulimwengu na serikali za nchi za nje yameelekezwa juu ya nchi hiyo."
Hapo awali, shirika la raia la nchi hiyo lilimlaumu rais wa Gambia, Yahya Jammeh, na lilisema kwamba wengi waliohukumiwa kifo ni wafungwa wa kisiasa.

Saturday, August 25, 2012

Risasi zafyatuliwa katikati ya New York

Watu kadha wamepigwa risasi nje ya jengo maarufu la skyscraper mjini New York, Empire State Building, ambalo linavutia watalii.
Empire State Building mjini New York
Meya wa New York, Michael Blomberg, alisema baadhi ya wale waliojeruhiwa pengine walipigwa risasi za polisi, lakini alisema majeruhi siyo mahtuti.
Mshambuliaji huyo ametajwa kuwa John Jeffrey Johnson - mpambi wa maduka ya nguo, ambaye alitolewa kazini mwaka jana.
Mtu aliyemuuwa ni mfanyakazi mwenzake wa zamani.
Eneo hilo la misafara mingi ya magari katika mtaa wa Manhattan, limefungwa na magari hayaruhusiwi kupita.

Sierra Leone yabanwa na kipindupindu

Serikali ya Uingereza inatayarisha msaada wa dharura kwa ajili ya Sierra Leone, ambako kipindu-pindu kimeuwa watu zaidi ya 200.
Sierra Leone

Uingereza inataraji kuwapatia watu maji masafi na kujenga mitaro kwa watu kama milioni mbili.
Uingereza imeanza kusafirisha kwa ndege zana za matibabu na wafanyakazi hadi Sierra Leone.
Watu zaidi ya 12,000 wameambukizwa ugonjwa huo mwaka huu.

Friday, August 24, 2012

Breivik siyo mwendawazimu

Mahakama ya Norway yameamua kuwa Anders Behring Breivik ana akili zake timamu, na imemhukumu kifungo cha miaka 21 kwa kuuwa watu 77 mwezi wa Julai mwaka jana.
Breivik anatabasamu
Upande wa mashtaka ukitaka kupata uamuzi juu ya akili ya Breivik, na angekutikana punguani angewekwa kwenye jela ya wendawazimu kwa muda usiojulikana.
Breivik siku zote amekiri kufanya mashambulio ya mabomu na bunduki, bila ya kuonesha majuto.
Amekuwa akishikilia kuwa ana akili yake, na kwamba aliyofanya ni vitendo vya kisiasa.
Alitabasamu hukumu ilipotolewa.
Wakili wa Breivik amethibitisha kuwa mteja wake hataomba rufaa.

Israili na Afrikan Kusini yazozana


Rais jacob Zuma
Rais jacob Zuma
Israili imekasirishwa na uwamuzi wa serikali ya Afrika ya Kusini wa kupiga marufuku nembo zinazowekwa kwenye bidhaa ambazo zina nembo isemayo ''made in Israel'' il hali zimetengenezwa Ufuko wa magharibi.
Badala yake Afrika ya Kusini inataka bidhaa hizo zibainishwe kwa kuandikwa kuwa zimetengezwa katika ''maeneo yanayokaliwa''
Wizara ya mashauri ya nje ya Israil itaja hatua hiyo kama ya ubaguzi.
Makaazi, miji ya Israili iliyojengwa katika maeneo yanayozozaniwa ya wa Palestina ni kinyume cha sheria ya Kimataifa ingawa Israili inapinga hilo.
Afrika ya Kusini inaaminika kuwa nchi ya kwanza kujaribu kutimiza uamuzi huu kisheria ingawa serikali nyingine kama Uingereza, zimewahi kuyashauri maduka makubwa yabainishe bidhaa zitokazo kwenye makaazi ya walowezi wa Israili.
Lakini kuanzia leo nchini Afrika ya Kusini, bidhaa kutoka makaazi hayo ya Israili, hazitokubalika kuwa na nembo "made in Israel".
Wizara ya mashauri ya nje ya Israili, imeutaja uwamuzi huo kama wa Ubaguzi wa rangi na usiokubalika.
Wizara hiyo imemtaka Balozi wa Afrika ya kusini nchini Israili aeleze hatua ya serikali yake.
Kuna kampeni inayofanywa miongoni mwa wa Palestina na waungaji mkono wao ya kususia bidhaa zinazotengenezwa ndani ya maeneo yanayokaliwa na walowezi wa Kiyahudi pamoja na Israili kwa ujumla.
Msemaji wa vuguvugu la Afrika ya Kusini ameutaja uamuzi wa Afrika ya Kusini kama ishara tu lakini akaonyesha matumaini utakua chachu kwa wengine.
Raia wa Palestina wanaopendelea vikwazo mara kwa mara hutumia mfano wa juhudi za uhuru huko Afrika ya Kusini kama changamoto na kuishutumu Israili kuwa inaendesha sera ya ubaguzi na kuongoza dola la kiimla, Israili inapinga tuhuma hizo.

Uingereza yaibembeleza Ecuador

Uingereza imeandika barua kwa ubalozi wa Ecuador mjini London ikitaka kurejelea mazungumzo kuhusu hatma ya Julian Assange, mwanzilishi wa mtandao wa kufichua siri wa Wikileaks, aliyetorokea katika majengo ya ubalozi huo kuepuka kurejeshwa nchini Sweden kwa lazima.
Julian Assange katika ubalozi wa Ecuador
Uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ulivurugika baada ya uamuzi wa Ecuador kumpa bwana Assange hifadhi ya kisiasa na Uingereza kutishia kuvamia ubalozi huo na kumkamata.
Afisi inayoshughulika na masuala ya kigeni haijasema chochote kuhusu ujumbe uliokop kwenye barua hiyo lakini afisa mmoja ameelezea kuwa inanuia kutuliza hali kati ya mataifa hayo mawili.
Rais Rafael Correa ameiambia BBC kuwa Uingereza ilifanya makosa makubwa kwa kutishia kuingia kwa nguvu kwenye ubalozi wa Equador,''Huu ni mvutano ambao ungeisha iwapo Uingereza ingetoa hakikisho ya kupita kwa usalama kwa Bwana Assange au unaweza kuendelea kwa miezi na hata miaka iwapo hataweza kutoka kwenye ubalozi wetu hapa London kuelekea Equador.''
Huenda mataifa ya Amerika Kusini yakamuunga mkono rais Rafael Correa.
Huku Uingereza ikisema kuwa inataka kurejelea mashauriano kuhusu hatma ya Julian Assange, Equador haikubaliani na msimamo huo na inataka kuhakikishiwa kuwa Assange hatakamatwa iwapo atatolewa kwenye ubalozi wao nchini Uingereza kuelekea Equador.
Equador inataka pia kuhakikishiwa kuwa mwanzilishi huyo wa mtandao wa Wiki Leaks hatawahi kupelekwa Marekani anakokabiliwa na tuhuma za kutoa taarifa muhimu na za siri kwenye mtandao wake.
Hata hivyo hakuna matumaini kwamba Marekani itakubali hilo.
Kwa hiyo ubalozi wa Equador umekiri kuwa huenda ukampa bwana Assange hifadhi kwa miaka mingi.

Thursday, August 23, 2012

Watu 48 wauawa Kenya

Ramani ya Kenya
Ramani ya Kenya
Polisi nchini Kenya, wanasema kuwa watu 48, waliuawa siku ya Jumanne usiku wa kuamkia , Jumatano, kufuatia mapigano makali kati ya jamii za Pokomo na Orma katika eneo la Mto Tana Kusini Mashariki mwa Kenya.
Mauaji hayo yilitokea wakati watu wenye silaha kutoka jamii ya Pokomo waliposhambulia kijiji kimoja katika eneo la Reketa huku wakiteketeza makaazi ya watu.
Naibu kamanda wa polisi mjini Mombasa, Joseph Kitur, amethibitisha kuwa watu 48 waliuawa, 31 kati yao ni wanawake, watoto 11 na wanaume sita.
Ng'ombe wapatao 60 vile vile walikatakatwa na wavamizi hao.
Kitur amesema shambulio hilo ni la kushangaza kwa kuwa watu 34 waliuawa kwa kukatakatwa mapanga, wengine 14 nao waliteketea hadi kufa katika nyumba zao.
Amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa shambulio hilo lilifanywa na watu kutoka jamii ya Pokomo.
Tangu mwezi uliopita, jamii hizo mbili zimekuwa zikipigana kuhusu umiliki wa ardhi inayotumiwa kama eneo la malisho ya mifugo, lakini shambulio hilo la Jumatano ndilo baya zaidi kuwahi kutokea katika historia yao.
Ripoti zinasema polisi wanawasaka wale waliofanya mashambulio hayo.
Kuna taarifa kuwa watu kadhaa wamekamatwa na polisi lakini mkuu huyo wa polisi hakuthibitisha ripoti hizo.
Idara ya polisi imesema uhasama kati ya jamii hizo mbili umekuwa ukitokota kwa muda, lakini hapakuwa na ishara ya fununu yoyote kuwa shambulio hilo la Jumatano lingetokea.
Mwaka wa 2001, takriban watu 130, waliuawa kwenye mapigano katika maeneo ya mipakani kati ya jamii hizo mbili.
Mbunge wa Eneo hilo, Danson Mungatana, amesema shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi mashambulio mengine yaliyofanywa na jamii ya Orma ambapo mamia ya mifugo iliibwa.

Dk. Ulimboka azimwa azidiwa kete

•  Vigogo serikalini wamzidi nguvu, abaki njia panda
 DHAMIRA ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka ya kutaka kuwafichua polisi na watu wengine wanaodaiwa kuhusika katika tukio la kumteka, kumpiga, kumtesa na kumtupa katika Msitu wa Mabwepande, imezimwa na vigogo wa serikali, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Uchunguzi ambao gazeti hili limekuwa likiufanya tangu Dk. Ulimboka awasili nchini, umebaini kuwa kinara huyo wa mgomo wa madaktari uliotikisa nchini, amekuwa na vikao na vigogo wa idara za ulinzi na usalama na kumshawishi awe mtulivu katika kipindi hiki ambapo serikali inafanya uchunguzi wa kina kubaini waliohusika kumteka nyara.
Watu wa karibu na daktari huyo, walilieleza gazeti hili kuwa, katika kipindi kifupi amekutana na vigogo kadhaa wa serikali wakimtaka asiseme chochote kwa hofu ya kuvuruga uchunguzi.
Wakati vigogo wa serikali wakifanikiwa kumzima Dk. Ulimboka, upande wa pili wa wanaharakati, ndugu na madaktari wenzake, wamekuwa wakimbana kumtaka awe jasiri kueleza umma ukweli, na hata kuwataja kwa majina waliohusika kumteka.
Hata hivyo, Joshua Mulundi aliyetajwa kuwa raia wa Kenya amefikishwa mahakama akituhumiwa kuhusika na tukio hilo.
Habari kutoka ndani ya uongozi wa Chama cha Madaktari (MAT), zilidai kuwa, hali ya ushawishi kutoka kwa vigogo wa serikali na mbinyo anaoupata kutoka kwa wanaharakati na madaktari wenzake, umemweka njia panda Dk. Ulimboka kiasi cha kushindwa kuamua kama atoke hadharani kueleza ukweli au atulie ili kulinda maisha yake.
Mara baada ya kurejea nchini akiwa na afya njema, Dk. Ulimboka amekuwa akikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari, kwamba anajiandaa kueleza ukweli wa tukio nzima na hata kuwataja waliohusika na unyama aliofanyiwa.
“Kwa jinsi hali ilivyo, Dk. Ulimboka atabaki na siri moyoni maana amekutana na watu wazito, wamezungumza nae na kumshawishi anyamaze, ndiyo maana hadi sasa hayuko tayari kuueleza umma kile alichopania kusema. Lakini pia wanaharakati na hata wanasiasa kila siku wanajaribu kumshawishi atoke hadharani kusema ukweli kabla tukio hilo halijaanza kusahaulika masikioni mwa watu,” alisema daktari mmoja ambaye ni mtu wa karibu na Dk. Ulimboka.
Katika kuthibitisha kwamba Dk. Ulimboka hayuko tayari kusema chochote, juzi gazeti hili lilikutana nae katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Ubungo ambapo alisema kuwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa, anamwachia Mungu.
Dk. Ulimboka ambaye aliongozana na familia yake kanisani hapo kwa nia ya kutoa sadaka na kumshukuru Mungu, alipobanwa hakuwa tayari kusema chochote zaidi ya kusema muda ukifika ataweka ukweli hadharani na kukanusha tuhuma za kunyamazishwa na vigogo.
Duru za kiintelijensia zililieleza gazeti hili kuwa, katika hali ya kawaida Dk. Ulimboka hawezi kusema chochote kama ilivyotokea kwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe aliporejea kutoka kwenye matibabu.
Dk. Mwakyembe ambaye aliugua ugonjwa ambao hata mwenyewe aliamini ulitokana na sumu, uliosababisha aoze kucha, kutoka unga mwilini na miguu kupasuka, alipata kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba atakuja kueleza ukweli jinsi alivyopewa sumu iliyomsababishia ugonjwa huo.
Hata hivyo, Dk. Mwakyembe tangu aliporejea hadi kuteuliwa kuwa Waziri wa Uchukuzi, hajawahi kueleza chochote kama alivyoahidi na kumweka mahali pabaya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Samuel Sitta ambaye ndiye aliyeshikia bango kwamba Dk. Mwakyembe alipewa sumu.
Dk. Ulimboka ambaye alipelekwa Afrika Kusini akiwa hawezi kutembea wala kula mwenyewe baada ya Juni 27 mwaka huu kutekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika Msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, amekuwa akiwakwepa wanahabari na anaishi kwa kujificha.
Kiongozi huyo wa madaktari amerejea nchini huku serikali na madaktari wakiwa hawajafikia mwafaka kuhusu madai yao.
Madai ya madaktari hao ni hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.
Safari ya Dk. Ulimboka kwenda kwenye matibabu nchini Afrika Kusini ilitawaliwa na usiri mkubwa alipoondoka nchini Juni 31 mwaka huu, akisindikizwa na Dk. Pascal Lugajo, kaka yake, Dk. Hobakile Ulimboka na mke wake, Dk. Judith Mzovela.
Kutekwa
Dk. Ulimboka alitekwa na kufanyiwa vitendo vya ukatili wakati akiratibu mgomo wa madaktari uliokuwa ukiendelea na aliokotwa na msamaria mwema akiwa amefungwa mikono na miguu akiwa katika hali mbaya.
Kutokana na tukio hilo, wanaharakati wa haki za binadamu waliituhumu serikali kuhusika na tukio hilo, huku yenyewe ikikana na kuliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka waliohusika.
Wakati Dk. Ulimboka alipokuwa akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete alisema serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya serikali na madaktari.
Rais Kikwete alisema hayo katika hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
“Dk. Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na serikali,” alisema Rais Kikwete.
Alisema alichofanyiwa Dk. Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.
Kauli ya Rais Kikwete kuhusu mgomo wa madaktari inafanana na ile iliyokuwa imetolewa awali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisema wanatambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk. Ulimboka, lakini ameshangazwa na hisia hizo akisema haoni sababu ya serikali kufanya hivyo.
Chanzo Mtanzania daima