NJOMBE

NJOMBE

Thursday, March 15, 2012

"Tujaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri"

Ujumbe wa Papa Benedikto XVI, kwa ajili ya tafakari za kipindi cha Kwaresima 2012, umewasilishwa rasmi kwa wanahabari Jumanne hii katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican.

Akiwasilisha ujumbe huo , Kadinali Robert Sarrah , Rais wa Baraza la Kipapa linaloratibu misaada ya Kanisa Katoliki, Cor Unum, ametaja Mada ya ujumbe huo kwamba umevuviwa na aya kutoka Waraka kwa Waeberania 10:24 “Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri".

Ameeleza, Baba Mtakatifu katika mwanga wa mafundisho ya kanisa kwa mwaka huu, anaonyesha mwelekeo wa kina zaidi, katika kazi za Kanisa kama Nabii, katika dunia ya leo, kuutangazia ulimwengu kwa namna ya kipekee, madhara ya utendaji usiomjali Mungu, akitaja hili ni chimbuko halisi la ukosefu wa haki unaoendelea kuitendea dunia

No comments:

Post a Comment