NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, February 1, 2012

CHADEMA:Waonya juu ya Raza

Msimchague Raza si mwadilifu
BAADA ya  Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kutupilia mbali pingamizi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kusimamishwa kwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mohamed Raza, kutokana na kuvunja sheria ya uchaguzi katika kipengele cha uchukuaji fomu, chama hicho kimewataka wananchi kutomchagua mgombea huyo kwa kuwa sio mwadilifu.
Kauli hiyo ilitolewa jana  katika kijiji cha Dagaa na Manzese, visiwani hapa na meneja wa kampeni wa CHADEMA, Saidi Mzee, na kuongeza kuwa
Raza alishindwa kulipa sh 1,500 kwa ajili ya fomu, hivyo ni wazi ameshaiibia nchi na ataendelea kuiibia.
Alisisitiza kuwa wananchi hawapaswi kumchagua Raza kwa kuwa anawania nafasi hiyo kwa ajili ya kupata urahisi wa kupitisha bidhaa zake na si kuwakomboa wananchi.
Naye Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, alisema watakaposhika nchi wataruhusu biashara ya gongo na kwamba kabla ya kukuzwa  itaboreshwa ili iweze kuwaingizia wananchi kipato.
Dk. Slaa alisema nchini  Uganda pombe hiyo imekuwa ikiwanufaisha watengenezaji ambao wanaiuza ndani na nje ya nchi yao, hivyo haoni sababu ya Tanzania kuendelea kuizuia.
Kuhusu upandaji holela wa bei ya sukari, Dk. Slaa alisema hali hiyo inasababishwa na ndoa kati ya CUF na CCM na kuongeza kuwa CUF kwa sasa haiwezi kutetea tena wananchi.
Alisema CHADEMA imeamua kuingia visiwani humo baada ya CUF kushindwa kukemea maovu kwa muda mrefu na kueleza kuwa wanaamini mgombea wao Ali Mbarouk Mshimba atafanya vizuri wakimchagua.
Dk. Slaa aliahidi kampeni zao zitaendelea nyumba kwa nyumba hadi usiku wa manane mpaka kieleweke na kuongeza kwamba  2015 lengo la chama hicho ni kushika baraza la wawakilishi.
Kwa upande wake mgombea Ali Mbarouk Mshimba, aliwataka wakazi hao kumpa kura za ndio kwa kuwa ni mzaliwa wa Uzini na pia anafahamu shida za wananchi.
“Mnajua wazi CCM imeua sera za chama cha Afro Shirazi party, hivyo itumieni hii fimbo ya karibu kuua nyoka badala ya mbali inaoishi Mji Mkongwe,” alisema

No comments:

Post a Comment