NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, November 7, 2012

JE WAJUWA KUWA ASALI NA LIMAU ZINAPUNGUZA UNENE NA UZITO

KUPUNGUZA UNENE KWA KUTUMIA ASALI NA LIMAU/NDIMU

Asali na limau
Diet ya asali na Limau diet inasaidia kupunguza tatizo la uzito mkubwa/unene . Obesity ni hali ya mwili unapokuwa unamafuta mengi kupindukia na mafuta hujitokeza katika tishu za mwili, kwenye moyo, figo, ini na viungo kama vile nyonga, magoti na vifundoni na hivyo, watu wenye uzito mkubwa pia  ni rahisi kukabiliwa na magonjwa kadhaa kama kisukari, shinikizo la damu, arthritis, ini na nyongo ya kibofu cha mkojo kupata matatizo.

Asali ni njia nzuri ya asili ambayo unaweza kutumia kwa ajili ya Obesity na kupunguza kwa viwango vya cholesterol mwilini. 

Kufunga/Fasting kwa asali na lemon-juisi, chakula alkali, ina manufaa katika matibabu ya Obesity bila kupata hamu ya kula.

Kwa ajili ya tiba hii ya asili, changanya kijiko kimoja cha asali mbichi (unheated) na vijiko viwili vya maji ya limau au ndimu katika glasi ya joto au maji vuguvugu (si kuchemsha maji!).

Kunywa mchanganyiko huu wa asali na limau/ndimu kila unapoamka asubuhi tumbo likiwa tupu. Pia unatakiwa kunywa mchanganyiko huu mara baada ya mlo kubwa na vyakula vya mafuta, hii inarahisisha kwenye digestion .

Ukiendelea na tiba asili ya kupunguza uzito unatakiwa kuzingatia kanuni kama vile kutengeneza tabia katika milo unayokula pia kujenga tabia ya kufanya mazoezi ya mwili mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment