NJOMBE

NJOMBE

Monday, January 30, 2012

Madiwani watakiwa kukaribisha wawekezaji makini


MADIWANI wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma, wametakiwa kuhamasisha wawekezaji ili kuwekeza kwenye miradi mbalimbali nchini kwani hali hiyo itawezesha upatikanaji wa ajira kwa vijana wilaya hiyo.
Wito huo ulitolewa jana na diwani wa kata ya Namtumbo mjini Alpihus Mchucha, katika kikao cha baraza la madiwani wakati akichangia hoja iliyosomwa na Kamati ya Uchumi na Mazingira kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo na kuwashirikisha watalamu wa idara mbalimbali.
Diwani Mchucha alisema kuwa ili kuweza kuyalinda mazingira vizuri na kupanua ajira kwa vijana ni vyema wawekezaji hao wakatambuliwa pia na Watanzania hasa katika kulinda mazingira na kupanua ajira ndani ya wilaya hiyo.
Tusipokuwa makini katika kutoa mikataba kwa wawekezaji tutajikuta tumewaacha wawekezaji wenye faida kuwaingiza wawekezaji wasio na faida kwetu jambo ambalo tutakuja kuanza kulaumiana pasipo sababu,” alisema diwani huyo.
Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Namtumbo, Stephen Nana, alisema kuwa ni vyema wataalamu na madiwani kuzingatia yale yote yaliyojadiliwa kwa kuyafanyia kazi ili halmashauri iweze kuinuka kiuchumi na jamii kunufaika nayo.

No comments:

Post a Comment