NJOMBE

NJOMBE

Saturday, January 28, 2012

Makamba ataka mikataba ya wachimba Uranium

KAMATI ya Bunge ya Nishati na Madini, imeitaka Wizara ya Nishati na Madini, kuwasilisha mikataba ya kampuni za Mantra na Urinex, zinazojihusisha na uchimbaji wa madini ya Uraniam, ili kuliwezesha Bunge kujiridhisha juu uhalali wao  katika kufanya shughuli hizo.

Hayo yalisemwa  na Mwenyekiti wa kamati hiyo, January Makamba, ambaye alisema hatua hiyo inatokana na umuhimu wa madini yenyewe katika dunia ya sasa.

Alisema kukaguliwa kwa mikabata hiyo, kutasaidia kubaini uhalali na uwezo wa kampuni hizo katika kufanya shughuli hizo.


“Kuna kampuni mbili za uchimbaji wa madini ya Uranium hapa nchini, lakini hadi sasa mikabata yake hatujaiona, kwa hiyo  tumeitaka wizara kuwasilisha mikataba hiyo kwenye kikao kijacho cha Bunge ili tuweze kuikagua,”alisema Makamba.

Alisema Kampuni ya Urinex  inachimba madini hayo katika maeneo ya Manyoni, mkoani Singida na Bahi huko Dodoma wakati Kampuni ya Mantra,  inachimba Uranium  katika mikoa ya Kusini mwa Tanzania.

Alisema Serikali kupitia kamati hiyo inapaswa kuhakikisha kuwa madini yanawanufaisha wananchi kuiwezesha nchi kujiingizia mapato.

Alisema madini hayo  yanahitajika sana duniani katika shughuli mbalimbali  na kwamba kwa msingi huo kama lazima ijue mikabata yote inayohusu uchimbaji wa Uranium.

Alisema kutowasilishwa kwa mikataba ya kampuni hizo, kumeifanya kama yake, kushindwa kujadili suala lolote kuhusu kampuni hizo.

No comments:

Post a Comment