NJOMBE

NJOMBE

Thursday, October 18, 2012

Papa Benedict kutuma ujumbe Syria

Papa Benedict wa kanisa katoliki
Papa Benedict anatuma ujumbe wa maafisa wa Vatican akiwemo askofu mkuu wa New York, Timothy Dolan -mjini Damascus wiki ijayo katika juhudi za kuitaka serikali na upinzani nchini humo kuheshimu haki za binadamu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea.
Taarifa kutoka Vatican zinasema kuwa Papa anatuma ujumbe wa ngazi za juu nchini humo kuwafariji watu wote wa taifa hilo wanaokabiliwa na wakati mgumu na wala sio kundi ndogo tu la wakristu.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Papa, Kadinali Tarcisio Bertone ambaye ataongoza ujumbe huo amesema kuwa kanisa katoliki haliwezi kushuhudia tu mkasa nchini syria ukiendelea huku wao wakikaa kimya.
Mwakilishi wa papa atakutana na viongozi wa serikali na wale wa waasi.
Mwandishi wa BBC mjini Rome amesema sio jambo la kawaida kwa Vatican kuingilia moja kwa moja katika mzozo kama huo.
Tangazo hili ambalo ni la ghafla lilitolewa wakati wa mkutano wa maaskofu wa kikatoliki mjini Vatican na askofu Tarcisio Bertone, ambaye ni naibu wa Papa.
Ujumbe huo unajumuisha waziri wa mambo ya nje wa Italia pamoja na viongozi wa kanisa hilo kutoka Afrika, Amerika ya Kusini na Bara Asia wote waliohudhuria mkutano wa leo.
Viongozi hao watalenga kukutana na pande zote katika mzozo wa Syria, upande wa upinzani na Serikali ya Assad.
Viongozi wa kikristo nchini Syria walimtumia ujumbe Papa na kumwambia kuwa wakristo nchini humo wanajipata katika hali ngumu sana

No comments:

Post a Comment