NJOMBE

NJOMBE

Monday, January 16, 2012

Wananchi waitaka ‘Katiba mpya rasilimali za nchi ziwe za serikali’

WANANCHI wa Mtama wilayani Lindi mkoani humo wametaka Katiba mpya kuwa na kipengele cha kuhakikisha rasilimali za nchi zinamilikiwa na Serikali, ili kuondoa ukoloni mambo leo uliopo sasa.

Mwalimu wa Shule ya Sekondari Namupa, Kaspal Mtotomwema, alisema hayo jana wakati
alipokuwa akizungumza kwenye mdahalo ulioandaliwa na Mtandao Lingonet.

Alisema ikiwa rasilimali zitamilikiwa na Serikali, itasaidia wananchi kumiliki ipasavyo rasilimali hizo kuliko ilivyo sasa ambapo watu wachache wanamiliki maeneo ya ardhi, migodi na kusababisha jamii kuwa watumwa ndani ya nchi yao.

Alitoa mfano kuwa hivi sasa kuna mfumo wa soko huria ambao wale wenye uwezo watakuwa
nanafasi nzuri ya kufanya kila kitu na jamii wenye kipato cha chini watabakia kunyonywa ndani ya nchi yao daima.

Mtotomwema alisema watu wachache wanamiliki migodi, ardhi na viwanda kutokana kufuatwa
mfumo huo ni hatari kiuchumi katika nchi.

Aliongeza nchi haiwezi kuwa na maendeleo ikiwa haina vyanzo vya mapato na kubakia kutegemea wahisani au kundi la matajiri wanaomiliki uchumi wa nchi.

Mkazi wa Kijiji cha Mtama, Dustan Millanzi alitaka Katiba liwe somo lianzie elimu ya msingi
na kuendelea.

Alisema yeye ana umri wa miaka 30, lakini katiba aliiona kwa macho jana na miaka yote hiyo 29 alikuwa haifahamu wala umuhimu wake, kwa biandamu.

Naye Mwanasheria Khalfan Omary aliwataka wananachi kuanza kujadili na kuilewa Katiba
na kuhakikisha wanatoa michango yao wakati Tume ya Kukusanya Maoni ikifika kwao.

Alisema Katiba ni muhimu kwa maisha ya Mtanzania kwa kuwa inamgusa kwenye vipengele
vya kiuchumi, utawala na siasa.

No comments:

Post a Comment