NJOMBE

NJOMBE

Sunday, January 22, 2012

MKUU WA MKOA WA RUVUMA ATEMBELEA PROJECT YA NISHATI MPYA YA MTO MKUJU

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh.Said Mwambungu jana jumamosi alitembelea project ya nishati mpya ya mto Mkuju.Project hiyo inaendelea mkoani humo wilayani Namtumbo kijijini Likuyu Seka ndani ya Hifadhi ya mbuga ya wanyama ya Selous.Mkuu wa mkoa huyo Mh.Said Mwambungu aliweza kujionea shughuli mbalimbali zinazo endelea katika Project hiyo yenye matarajio baadae ya kuwa mgodi.Project hiyo iliyopo inajishughulisha na utafiti wa madini ya uranium (urani).Utafiti unafanywa na kampuni ya Mantra Tanzania Limited chini ya Uranium1 kampuni inayotokea nchini Urusi.Mpaka sasa utafiti huo unaendelea maeneo mbalimbali chini ya kampuni hizo.Utafiti huo umeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana hadi kuweza kusababisha mradi huo kuwa mgodi wa madini hayo ambayo ni muhimu sana dunia kote.
Licha ya mkuu huyo wa mkoa kujionea shughuli za mradi,mkuu huyo nae pia aliongea machache juu ya mtazamo wake katika shughuli izo katika mkoa wake,mkuu wa mkoa Mh.Said Mwambungu alisema namna shughuli za project hiyo inayotarajiwa kuwa mgodi ni nzuri kwani zimeweza sana kusaidia uchumi wa watu wake katika mkoa huo kwa kuweza kutoa ajira kwa vijana katika mkoa wake nakusema anatarajia mkoa kuwa ni mkoa wenye maendelea makubwa sana kutokana na mradi huo na kusema yeye kwa upande wake amelipokea hilo kwa mikono yote kuwa mradi huo uendelea kwasababu unamafanikia makubwa siku za usoni.
                                                         Matukio ya Picha
      Mh.Said Mwambungu kiweka sahihi katika kitabu cha wageni katika camp ya project ya nishati mpya
Hawa ni baadhi ya mameneja katika mradi huo kuanzia kushoto ni Colline Grammar meneja wa site,Benard Mihayo meneja mausiano,Emmanuel Nyamusika meneja wa utafiti,John Ntukula meneja mazingira,Peter Kaluwa administration officer.
Mh.Emmanuel Nyamusika meneja utafiti akielezea juu ya shughuli za mradi nini maana na nini kanachofanyika na nini kinachotafutwa.
Mh.John Ntukula meneja mazingira akielezea juu ya mazingira namna wanavyofanya katika swala la utunzaji wa mazingira ikiwemo uwoto wa asili.
Mh.Said Mwambungu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi katika mradi wa mto Mkuju
Imeandikwa na Makali Machechi picha na Clever Perfect









No comments:

Post a Comment