NJOMBE

NJOMBE

Monday, January 16, 2012

Twiga Stars yaikandamiza Namibia 2-0

                                                              kikosi cha Twiga Stars
TIMU ya soka ya Taifa ya Wanawake, Twiga Stars jana ilijiweka kwenye mazingira mazuri ya michuano ya Afrika baada ya kuifunga Namibia mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa mjini Windhoek, Namibia.

Habari zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni jana, zilisema mabao ya Twiga yalifungwa
kipindi cha pili na wachezaji Asha Radid 'Mwalala' na Mwanahamisi Shaluwa.

Twiga sasa inajiandaa kucheza mechi ya marudiano jijini Dar es Salaam wiki mbili zijazo.


No comments:

Post a Comment