NJOMBE

NJOMBE

Saturday, January 28, 2012

Mwakyembe aweka wazi yanayomsibu

•  Achoshwa na maswali ya afya yake

 


   AFYA ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, ni tete baada ya kuugua ugonjwa uliomsababisha kuvimba mwili wote.Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na yeye mwenyewe zinaeleza kuwa, alianza kuwashwa ngozi miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye kuvimba sehemu kubwa ya mwili wake.

HATIMAYE Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ameamua kuzungumzia ugonjwa unaomsumbua kwa muda mrefu sasa.
Akizungumza  jana kwa njia ya simu, Dk. Mwakyembe alisema wiki ijayo anatarajia kuzungumzia ugonjwa huo ambao baadhi ya watu wamekuwa wakiuhusisha na kulishwa sumu.
Miongoni mwa watu wanaodai kuwa Dk. Mwakyembe kalishwa sumu ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye mara kwa mara amekuwa akiwatuhumu watu anaowaita mafisadi kushiriki katika uovu huo.
Sitta amenukuliwa akisema pamoja na kutoa madai hayo jeshi la polisi halijayatilia uzito zaidi ya kumhoji yeye na Dk. Mwakyembe.
Katika mazungumzo yake jana na gazeti hili, Dk. Mwakyembe ambaye alirejea nchini mwishoni mwaka jana akitokea India kwa matibabu, alisema kwa siku mbili hizi hawezi kuzungumzia hali yake na kilichomsibu.
“Kwa sasa waulize madaktari kuhusu hali ya ugonjwa wangu, mimi nitafute wiki ijayo tuzungumze,” alisema Mwakyembe bila kubainisha ni siku gani hasa.
Juzi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipozungumza na waandishi wa habari alisema kuwa serikali haiko tayari kuzungumzia ugonjwa unaomsumbua Dk. Mwakyembe, kwani ni kinyume cha maadili ya utabibu.
Pinda alisema hata kama anafahamu ugonjwa unaomsumbua hawezi kuuzungumzia na badala yake mwenye wajibu wa kufanya hivyo ni Dk. Mwakyembe mwenyewe.
Wakati Pinda akitoa kauli hiyo, serikali ilishawahi kutoa taarifa ya magonjwa yaliyowasumbua baadhi ya viongozi waliopata kutibiwa nje ya nchi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.
Kwa muda mrefu Dk. Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa ambao hadi sasa haujawekwa wazi jambo linalowafanya baadhi ya wananchi wapate wasiwasi kuhusu usalama wa viongozi wa serikali.
Tanzania Daima lilidokezwa kuwa madaktari waliomtibu katika Hospitali ya Apollo nchini India waliandika ripoti inayohusu ugonjwa wake ambayo inasemekana imekabidhiwa serikalini.
Kwa mujibu wa taarifa zilizowahi kuandikwa na gazeti hili kutoka kwa baadhi ya watu walio karibu na kiongozi huyo ni kuwa hali yake si nzuri na hatoweza kurejea katika shughuli zake za kawaida katika kipindi kifupi kijacho.
Watu hao walidokeza kuwa Naibu Waziri huyo amenyonyoka nywele, kope na vinyweleo huku ngozi ikiwa imeharibika.
Kabla ya Dk. Mwakyembe kuanza kuugua na hatimaye kupelekwa India alitoa taarifa kwa jeshi la polisi juu ya njama za baadhi ya watu kutaka kumuua.
Baada ya madai hayo Dk. Mwakyembe aliitwa polisi kutoa maelezo juu ya tuhuma hizo lakini mpaka sasa jeshi hilo halijaeleza hatua ilizozichukua dhidi ya watu waliotajwa kuhusika na njama hizo

                                                  

No comments:

Post a Comment