NJOMBE

NJOMBE

Saturday, January 21, 2012

Wanakijiji Mbeya waenda hospitali na taa zao

WANANCHI wa Kijiji cha Mbebe Wilaya ya Ileje mkoani Mbeya wamelazimika kutoka na taa zao nyumbani mpaka Kituo cha Afya cha kijiji hicho ili kupatiwa huduma baada ya kituo hicho kukosa umeme kwa muda mrefu.

Watumishi wa kituo hicho waliojitambulisha kwa jina moja moja la Pagale na Kaponda walisema tatizo la umeme limekuwa kero hasa kwa wanawake wajawazito wanaojifungua usiku.

Wahudumu hao walisema wagonjwa wanaopatiwa huduma katika kituo hicho ni kutoka vijiji saba vinavyoizunguka zahanati hiyo na wengi wao wakiwa wanatoka umbali wa kilometa saba na wengine tano.

Aidha, walisema tatizo hilo linawalazimu mara nyingine kutumia mafuta yao ya taa huku nishati hiyo ikiwa imepanda bei kwa kiasi kikubwa na hivyo kuwa kero kwao.

Kwa Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC), baadhi ya wananchi walihoji pesa wanazotoa katika kituo hicho kuwa zinafanya kazi gani mpaka kituo hicho kinakosa umeme.

“Hapo nyuma umeme ulikuwepo lakini kutokana na wananchi kusuasua kulipia bili za umeme, umeme ukakatwa,” alisema mmoja wa wauguzi ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Aidha alisema kitendo hicho kimewasababishia wachukiwe na wananchi kwa kuwa wagonjwa wafikapo kituoni hapo hukuta kukiwa giza na ndugu wa mgonjwa hulazimika kutafuta mafuta ya taa.
Imeandikwa na Neema Kidumba, Mbeya;

No comments:

Post a Comment