NJOMBE

NJOMBE

Thursday, March 29, 2012

DUNIANI KUNA MAMBO: MATATANI KWA KULEWESHA MBWA

Bwana mmoja nchini Marekani amekamatwa na polisi baada ya kumpa pombe mbwa wake na kumlewesha kiasi cha mbwa huyo kushindwa hata kutembea.

Bwana huyo Todd Harold Schreiner, anashtakiwa kwa kosa la kutesa wanyama. Polisi wa mji wa East Helena walikuta mbwa huyo akiwa amelewa chakari, mara nne zaidi ya kipimo cha wanadamu kinachoruhusu kuendesha gari.

Taarifa zinasema mbwa huyo aitwaye Arly II wakuweza kusimama au kutembea vyema wakati alipokutwa na polisi ndani ya baa moja saa tano na nusu usiku.

Mbwa huyo alichukuliwa na kupelekwa katika zahanati ya wanyama ambapo vipimo vilionesha ana ulevi wa asilimia sifuri nukta tatu nne nane katika damu yake.

Kisheria kipimo cha mwisho cha ulevi wanaadamu wanaruhusiwa kuwa nacho na kuendesha gari ni asilimia sifuri nukta sifuri nane. Muuzaji katka baa aliyokutwa mbwa huyo amesema mwenye mbwa alimpa mbwa wake kilevi aina ya vodka.

No comments:

Post a Comment