NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, March 14, 2012

JAMANI AFRIKA, MATUNDA NA VIUNGO!!NI JAMBO LA KAWAIDA


Nadhani wote mnajua hapa ni mti wa malimao angalia jinsi yalivyo yaani nashindwa hata kuelezea hapa ni mwaka jana  Matema beach mkoani Mbeya Tanzania.

....na hapa bila kiungo hiki kachumbali hainogi ni pilipili kichaa ...swali la kizushi hivi ukila hizi unakuwa kichaa kweli? na kwanini zinaitwa pilipili kicha?..


Bado tupo Matema Beach bonge la mkungu wa ndizi mpaka nikatamani niupate na unajua nini? niliupata:-)
..Hapa ni Mdunduwalo mti wa machungwa ...naipenda Afrika yangu kwa kweli matunda na chakula ni kutoka tu nje na kuchukua.Jamani nimepakumbuka nyumbani

No comments:

Post a Comment