NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, March 20, 2012

Dar kukosa maji siku mbili

Baadhi ya vitongoji vya jiji la Dar es Salaam vinatarajia kukosa huduma ya maji kwa siku mbili kutokana na kupasuka kwa bomba kubwa linalosambaza huduma hiyo katika eneo la gereji Wilaya ya Bagamoyo.

Afisa Uhusiano wa Mamalaka ya Maji safi na Maji taka (Dawasco), Teddy Mlengu, alisema baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam yanatarajiwa kutopata huduma ya maji kutokana na kupasuka kwa bomba kubwa linalosambaza huduma hiyo katikati ya jiji
Maeneo yatakayoathirika na huduma hiyo, kuwa ni Mbezi Beach, Kawe, Tegeta, Sinza, Mwenge, Ilala, Mwananyamala na Bunju.
Alisema mafundi wanashughulikia tatizo hilo kwa juhudi kubwa na wanatarajia kulifunga kesho na kuwataka wakazi wa maeneo hayo kutumia maji kwa uangalifu kwa kujiwekea akiba ya kutosha.
Mlengu alisema Jumamosi walilazimika kuzima mtambo unaosambaza huduma ya maji katika maeneo hayo kutokana na hitilafu ya umeme. 


Chanzo:Nipashe

No comments:

Post a Comment