NJOMBE

NJOMBE

Sunday, October 14, 2012

Nchi zinazotumia Kifaransa zakutana

Viongozi 20 wa mataifa yanayozungumza Kifaransa wanakutana katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo huku machafuko mashariki mwa nchi hiyo yanaendelea na kuna mzozo nchini Mali.
Rais Franois Hollande wa Ufaransa
Rais Francois Hollande wa Ufaransa aliuambia mkutano huo kwamba Ufaransa inaunga mkono pendekezo la kutuma jeshi la kimataifa Mali.
Piya alisema maswala muhimu kwa jumuia hiyo ni demokrasi na haki za kibinaadamu.
Hapo awali aliwakera wenyeji wake kwa kuwalaumu kwa rikodi yao katika maswala hayo.
Lakini alipigiwa makofi kwa kulaani mapigano ya mashariki mwa Congo.

No comments:

Post a Comment