NJOMBE

NJOMBE

Thursday, September 6, 2012

Watu 34 wafariki kiwandani nchini India

Kiwanda cha fataki nchini India
Watu 34 wameuawa na wengine 30 kujeruhiwa katika moto mkubwa uliotokea katika kiwanda cha fataki kusini mwa jimbo la Tamil Nadu, nchini India.
Moto huo katika kiwanda cha Om Shakti ulisababisha milipuko kadhaa ya fataki na moshi mkubwa kwenye kiwanda hicho kilichoko mjini Sivakasi, kitovu cha viwanda vya fataki nchini India.
Mji huo una mamia ya viwanda na hutengeza asilimia tisini ya fataki nchini humo.
Kwa mujibu wa afisaa mkuu wa polisi wilayani Virudhunagar, ambako mji wa Sivakasi uko, idadi ya waliofariki ilipanda hadi watu 34.
Aliongeza kuwa baadhi ya waathiriwa walikuwa wafanyakazi wa viwanda ingawa wengi walikuwa wenyeji wa vitongoji vya eneo hilo.
"baada ya mlipuko, watu walienda kiwandani kujionea na kwa bahati mbaya waliofika kushuhudia tukio hilo nao pia wakateketea'' alisema afisaa huyo.
Bwana Hoda alisema kuwa leseni ya kampuni hiyo ilikuwa imefutiliwa mbali kwa muda kwa sababu ya kukiuka sheria za usalama wa wafanyakazi na kwamba hakuna kazi ilipaswa kuwa inafanyika kiwandani humo hii leo. Aliongeza kuwa polisi wanamsaka mwenye kiwanda hicho.
Awali bwana Hoda aliambia BBC kuwa wazima moto walishindwa kuingia kiwandani kwa sababu milipuko ilikuwa bado inasikika.
"kuna joto jingi sana na hali ni ngumu kwa watu kuweza kuingia ndani ya jengo hilo. Kiwanda kina akiba kubwa ya fataki na milipuko bado inasikika'' alisema bwana Hoda.
Bado haijajulikana kilichosababisha moto huo.

No comments:

Post a Comment