NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, September 12, 2012

Marekani yaadhimisha mashambulizi ya 9/11


Nchini Marekani,maadhimisho ya miaka kumi na moja tangu kutokea kwa mashambulio ya 9/11 mjini New York na katika makao makuu ya idara ya ulinzi ya Pentagon mwaka wa elfu mbili na moja yanafanyika.
Kwa mara ya kwanza hakutakuwepo na hotuba yoyote wakati wa sherehe hizo kutoka kwa wanasiasa.
Familia za zaidi ya watu elfu mbili mia saba waliouawa zitaruhisiwa kufika katika eneo la tukio la mashambulizi hayo maarufu kama Ground Zero mjini New York,.
Awali idara ya afya nchini Marekani ilitangaza kuwa manusura wa mashambulio hayo na wale waliowasaidia watapewa uchunguzi na matibabu ya takriban aina hamsini za saratani bila malipo, kwa sababu walivuta hewa iliyokuwa na sumu baada ya mashambulio hayo.

No comments:

Post a Comment