NJOMBE

NJOMBE

Saturday, September 8, 2012

Kanisa la Anglikana lataka kuwa na rais

Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana, Rowan Williams, amefichua kuwa kanisa hilo linaandaa mpango wa kumteua rais wa kanisa, ambaye atabeba sehemu ya jukumu la kuongoza kanisa duniani.
Askofu Rowan Williams

Alisema mtu atayechukua nafasi hiyo ataweza kusafiri kwa urahisi, na hivo kumuacha Askofu Mkuu kushughulika zaidi na kuongoza kanisa.
Doctor Williams, ambaye anastaafu mwezi wa Disemba baada ya uongozi wa miaka 10, alikiri kuwa hakuweza kufanya mengi kuzuwia mgawanyiko kanisani juu ya swala la uhusiano wa jinsia moja.

No comments:

Post a Comment