NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, September 5, 2012

Jeshi la Kenya lashambulia Kismayo

Mwanajeshi wa Kenya
Jeshi la wanamaji la Kenya limekiri kuwa lilishambulia mji wa Kismayo siku ya Jumatatu
Msemaji wa jeshi la Kenya kanali, Cyrus Oguna, aliambia BBC kuwa shambulizi hilo la hapo jana ni sehemu ya harakati za Muungano wa Afrika, dhidi ya wanamgambo wa Al Shabaab.
Wakaazi wa mji huo ambao unadhibitiwa na kundi la wapiganaji wa al-Shabaab, waliambia BBC kuwa walisikia milipuko katika meli zilizoko baharini.
Awali wanajeshi wa Kenya wakishirikiana na wale wa Ulaya na vikosi maalum vya Marekani walikana kuhusika na mashambulizi hayo.
Hata hivyo Duru zinasema kuwa sasa wameanza kupambana na wanamgambo wa Al Shabaab wanaodhibiti mji huo.
Wakati huohuo,duru zinaarifu kuwa kundi la Al shabaab nalo linajiandaa kwa mapambano hayo.
Al Shabaab hutumia mji huo kuingiza silaha zao kutoka nje na pia huwatoza kodi wafanyabiashara wanaotumia bandari hiyo kujikimu kimaisha.
Kismayo ndio mji mkubwa pekee uliosalia kudhibitiwa na Al Shabaab .
Wanajeshi wa Somalia wanaoshirikiana na wale wa Kenya wanaripotiwa kuukaribia mji huo wakiwa tu umbali wa kilomita hamsini kutoka mjini humo wakati wanajeshi wa Kenya wakisema kuwa wao wangali mbali sana na mji huo.
Inaarifiwa wasiwasi umekumba mji huo wakaazi wakisubiri mapambano ya kuudhubiti mji huo ambao ndio ngome kuu ya Al Shabaab.

No comments:

Post a Comment