NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, September 5, 2012

Ajali mbaya ya barabarani Morocco

Majeruhi waliookolewa kutoka kwa basi hiyo
Takriban watu 42 wamefariki baada ya basi walimokuwa wakisafiria kuanguka katika Korongo kusini mwa Morocco.
Zaidi ya abiria wengine ishirini walipata majeraha mabaya.
Basi hilo lililokuwa linasafiri kati ya miji ya Marrakesh na Zagora, lilianguka umbali wa mita 150 kutoka barabarani
Wengi wa abiria waliokuwa wanasafiri kwenye basi hilo wanaaminika kuwa raia wa Morocco. Haijulikani ikiwa kuna majeruhi wowote wa kigeni walikuwa kwenye basi hilo.
Duru zinaarifu kuwa ajali hiyo ilitokea katika eneo lenye milima mapema leo asubuhi.
Bado haijulikani kilichosababisha ajali yenyewe ingawa afisaa mmoja mkuu anasema kuwa uchunguzi umeanzishwa.
Takriban watu 24 walijeruhiwa , ishirini na moja kati yao wakikimbizwa hospitalini mjini Marrakesh na waliosalia wakipelekwa hospitalini mjini Ouarzazate.
Katika taarifa yake, mfalme wa nchi hiyo Mohammed wa sita, alitoa rambi rambi zake kwa familia za waathiriwa na kuahidi kulipia usafiri na gharama za mazishi.
Mwezi Julai mwaka jana, ajali mbili tofauti za basi nchini humo zilisababisha vifo vya watu 26.
Zaidi ya watu 4,000 walifariki katika ajali tofauti za barabarani nchini Morocco mwaka jana kulingana na takwimu za wizara ya usafiri nchini humo.

No comments:

Post a Comment