NJOMBE

NJOMBE

Friday, September 7, 2012

TANZANIA NCHI YANGU INAYOPOTEZA UHALISIA WAKE

Namshukuru Mungu kuzaliwa Tanzania, Nchi iliyobariliwa kila aina ya utajiri duniani, mwenyezi Mungu yupo pamoja nasi kwa kila kitu ndiomana nchi kama za mashariki ya mbali ulaya na amerika zimetajirika kupitia maliasili za watanzania tuliolala usingizi bila kujua wapi tunaelekea na hii baiskeli yetu ya miti, kwanza napenda kutoa pole kwa ndugu zetu wote waliopoteza maisha kwenye matukio tofauti kama mabomu ya Mbagala na Gongo la mboto,kuzama kwa meli ya MV BUKOBA,MV SPICE, MV SKAGIT, tumepoteza nguvu kazi kubwa ya taifa, lakini yote tisa sijui ni tatizo nini ukiuliza tumeunda tume tuwaachie tume wafanye kazi yao, yakitokea tena oooh nimakosa yakimaumbile sisi ni ngumu kuyazuia, wenzetu
wanazidi kuteketea, nchi inaingia gizani wawakilishi wetu wanakula rushwa wanaanza kurushia vijembe bungeni mambo yanapita hakuna hatua zilizochukuliwa, dah inaumiza sana, hivi napenda kuuliza tunaangalia maisha ya mjini tu au na watu wa kijijini tumewasahau, kwa sababu inasikitisha kuniambia uchumi umekuwa wakati watu zaidi ya milioni kumi hawajui watakula nini pale wanapofika muda husika kwa sababu hata shilingi mia moja hawana mfukoni. Mnamo mwaka 2010 nilibahatika kufanya utafiti katika mkoa wa Rukwa wilaya ya sumbawanga vijijini jimbo la kwela kuhusu kushuka kwa elimu katika mkoa wa Rukwa, ni masikitiko makubwa sana pale ukiipata hiyo taarifa nafikiri serikali ifike pahala iseme kuna maeneo tumeshindwa kufikia              malengo na watoe taarifa kwa nini wameshindwa hili hata wananchi watafute namna nyingine ya msaada hili wajikomboe na tatizo hili la uchumi.
Madini ya Tanzanite
Tatizo lingine vijana wakitanzania tuliowengi tunapenda mijadala ambayo haijengi nchi ni kubomoa nchi kwa sababu ya itikadi ya chama, na pili tumeshajiwekea katabia kakutofanya kazi sijui tunategemea nini, jamani hii nchi hawa jamaa wanaipeleka sehemu ambapo palipo tufanya tuwaone wakoloni wabaya, na watu wa kurekebisha hayo maswala ni sisi si wao, sasa tufike pahala jamani watanzania wenzangu tuangalie maisha haya na nchi yetu inapokwenda. ni mtazamo wangu
 
 Vijana wakiwa kijiweni na baada ya hapo ni kwenye pombe tu na mambo mengine sasa je tutaweza kujikwamuwa hapa tulipo na kwenda mbele licha tu ya kukosa ajira hata wenyewe kujishughulisha hatuwezi jamani.Hebu jamani tujufunze kutoka china,Watu wa China wanafanya kazi sana ndiomana hata nchi yao inakuwa kiuchumi si watu wakukaa tu kama hapa kwetu

No comments:

Post a Comment