NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, September 4, 2012

Ustaarabu na Ushenzi ni vitu vinavyofanana

Ustaarabu...

Ustaarabu na ushenzi ni vitu vinavyo fanana sana. Na wala sio rahisi kupambanua upi ni ustaarabu hasa na upi ni ushenzi. Kwa maana kile kinachoitwa ustaarabu kwa mtu mmoja kinaweza kuwa ushenzi kwa mtu mwingine na ushenzi kwa huyu unaweza kuwa ustaarabu kwa yule.
Mdada asilia

Si ajabu wakoloni walipokuja waliuita utamaduni wetu eti ni wa kishenzi. Tunapoishi katika jamii tunaupima ustaarabu kutokana na kawaida (norms) ya watu wanao tuzunguka. Tatizo ni kwamba mara nyingine huo tunaouita ustaarabu kumbe ndio ushenzi hasa kuliko ule tunaodhania kuwa ndio ushenzi.

Halle Berry
Inanishitua sana ninaposikia kampeni za kuhimiza kukubalika kwa ndoa za jinsia moja. Inanishangaza ninapoona viongozi wa dini na watu wanaoheshimika sana wakisisitiza wanaume wanaojifanya wanawake na wanawake wanaojifanya wanaume wapewe haki ya kufunga ndoa na kuheshimiwa kama wanandoa wengine kwa sababu eti huo ndio ustaarabu.  Inanisumbua ninapoona wanawake na wanaume wakijitembeza mitaani kuuza uroda kana kwamba ni njugu kwa madai kwamba huo ni ustaarabu...

Jeniffer Lopez

Inaniuma sana ninapoona wezi wa mali ya umma wakitukuzwa, kushangiliwa, kulindwa na kupewa nafasi zajuu zaidi za uongozi kwa sababu eti huo ndio ustaarabu...Inanikera ninapoona viongozi wanazidi kujilimbikizia mali, kujenga himaya za kifalme, kutumia mabilioni ya shilingi za wavuja jasho kwa matumizi yasiyo ya lazima huku wakiwaacha wananchi wakiteseka kwa kukosa huduma muhimu kama afya (matibabu) umeme, maji, na usafiri wa kuaminika mijini. Inanitia kichefuchefu kwamba madaktari wetu wanafikia kugoma kwa madai ya fedha huku wanasiasa wakilimbikiziwa posho kiasi cha kuogopa kuzipokea kwa aibu...huu nao ni ustaarabu. 

Lady Gaga

Zaidi ya yote inaniuma sana ninapoona watoto wetu wakifundishwa ubinafsi, kutothamini utu, kutomuogopa Mungu kwa imani kwamba hayupo (ha exist) na kupewa uhuru mkubwa kuliko mtoto anaostahili kuwa nao kwa kisingizio cha haki za watoto, eti  nao ni ustaarabu...Wallah kama huu ndio ustaarabu ni bora turudi kwenye kutembea uchi maana naamini watu walikuwa wastaarabu zaidi kuliko sasa...
 

No comments:

Post a Comment