NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, September 4, 2012

Televisheni ya Misri yaruhusu hijabu

Wanawake wa Misri waliovaa hijabu, wakipiga kura mwezi May
Serikali ya Misri imeondoa amri iliyopiga marufuku wasomaji habari kwenye televisheni kuvaa hijabu.
Jumapili taarifa ya habari ya mchana kwenye televisheni ya taifa ilisomwa na mwanamke, Fatma Nabil, ambaye alifunika kichwa na kitambaa cha rangi ya maziwa.
Afisa wa televisheni ya Misri alisema wanawake sasa wataambiwa nao wafuate, na kwamba hawatahatarisha kazi zao wakivaa hijabu.
Amri ya marufuku iliwekwa na serikali zilizopita za Misri.
Baadhi ya wasomaji wa habari waliishtaki televisheni ya taifa na walishinda, lakini baada ya hapo hawakuruhusiwa kuonekana mbele ya kamera.

No comments:

Post a Comment