NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, September 4, 2012

Mshirika wa Aboud Rogo ajikabidhi kwa polisi

Mtu anayesemekana kuwa mshirika wa karibu wa mhubiri aliyeuawa wiki jana mjini Mombasa, Kenya, Sheikh Aboud Rogo, amefikishwa mahakamani kwa kosa la uchochezi wa ghasia na kufanya mauaji.
Abubaker Sharif anayejulikana kwa jina lengine kama Makaburi, awali alikuwa amedai kuwa maisha yake yamo hatarini na hata kudai kuwa maafisa wa serikali walikuwa na njama ya kumuua.
Polisi wanasema walikuwa wametoa kibali cha kumkamata ingawa Abubakar aliweza kujikabidhi mwenyewe kwa polisi.
Hata hivyo amekana madai hayo dhidi yake.

No comments:

Post a Comment