NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, September 12, 2012

Malema aitisha mgomo wa kitaifa wa wachimba migodi

Mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini Julius Malema ametoa wito wa maandamano makubwa ya kitaifa nchini humo kwa wafanyakazi wa migodini.
"wamekuwa wakiiba madini haya ya dhahabu kutoka kwenu." bwana Malema aliambia wachimba migodi waliokuwa wanamshangilia katika mgodi mmoja wa dhahabu mashariki mwa Johannesburg.
"sasa ni wakati wenu." aliongeza Malema.
Migomo migodi ya wachimba migodi imekumba Afrika Kusini na kuathri shughuli za kuchimba madini ya Platinum na dhahabu katika nchi hiyo yenye rasilimali nyingi.
Lakini baadhi wanamtuhumu Malema kwa kuwa na njama na kujinufaisha kisiasa huku wengi wakiwa bado wanaomboleza vifo vya wachimba migodi 34 wa Marikana mwezi jana nchini humo.
Watu 44 walifariki katika mgodi huo katikati ya mwezi Agosti. 34 wakipigwa risasi na kuuawa na polisi kwa siku moja.
Tume ilibuniwa na serikali kuchunguza matukio katika mgodi huo.
Wadadisi wanasema kuwa kuangazia baadhi ya mambo yanayohusu chama cha ANC kama uhusiano wake na biashara kubwa kubwa pamoja na kupuuza wananchi wafanyakazi ambao wamekuwa daima wakiunga mkono chama hicho bila shaka ni mwiba kwa chama tawala.
"lazima mgomo wa kitaifa ufanyike," Malema aliwaambia wafanyakazi wanaogoma katika machimbo ya dahahabu ya KDC.
''Yametosha! Tumesubiri miaka mingi kunufaika na madini haya. Lazima sasa mfaidike na nyiyi kutokana na dhahabu hii.'' alisema Malema.
Wakati akitoa hotuba yake, Malema alishangiliwa sana watu wakipiga firimbi na mbinja pamoja na kupuliza vuvuzela.
Malema alifurushwa kutoka chama tawala ANC na angali anachunguzwa kwa madai ya ufisadi . Lakini anaendelea kuzua hisia miongoni mwa umma hasa kufuatia mauaji ya wachimba migodi mwezi jana.

No comments:

Post a Comment