NJOMBE

NJOMBE

Sunday, July 15, 2012

Clinton amzuru Mursi Misri

Waziri wa mashauri ya Nchi za Nje wa Marekani, Hillary Clinton, yuko nchini Misri kukutana na kiongozi mpya, rais kutoka chama cha muslim brotherhood, Mohamed Morsi.
Hillary Clinton katika ziara yake ya karibuni barani Asia

Miaka iliyopita, waziri mmoja wa mashauri ya nchi za nje wa Marekani, alitangaza Marekani haizungumzi na muslim brotherhood, na daima haitafanya hivo.
Sasa, serikali ya Rais Obama, imefanya haraka kuwasiliana na rais mpya wa Misri wa muslim brotherhood, Mohamed Morsi.
Marekani imekubali kuwa ukweli hauepukiki, na inajaribu iwezavyo.
Bila ya shaka Hillary Clinton atataka kupata ahadi ya Rais Morsi, juu ya siasa za Misri kuhusu mambo ya nje na ya ndani ya nchi.
Serikali ya Marekani inataka kuona demokrasi na haki za kibinaadamu zinalindwa nchini Misri.
Kwa upande wao, muslim brotherhood wamesisitiza mara kadha kwamba hawataki kutengwa na ulimwengu, hasa kwa sababu nchi hiyo inategemea sana biashara za kimataifa na utalii.

No comments:

Post a Comment