NJOMBE

NJOMBE

Monday, July 9, 2012

Morsi akaidi amri ya jeshi

 
Katika hatua ya kulikaidi jeshi lenye nguvu nchini Misri, rais mpya Mohammed Morsi, ametoa amri kuwa bunge likutane.
Rais Mohammed Morsi wa Misri

Amri yake inakwenda kinyume na hukumu iliyotolewa mwezi uliopita na mahakama ya katiba, kwamba bunge la sasa siyo halali.
Bunge hilo lina wajumbe wengi wa vyama vya Kiislamu.
Hukumu ya mahakama ilitekelezwa na jeshi, ambalo lilifuta bunge na kujipa madaraka ya kutunga sheria.
Televisheni ya taifa inasema halmashauri ya jeshi itafanya kikao cha dharura kujadili amri ya Rais Morsi.

No comments:

Post a Comment