NJOMBE

NJOMBE

Thursday, July 19, 2012

Waziri wa serikali wauawa Syria

Daoud Rajiha aliyekuwa shameji ya rais Bashar Al Asaad pamoja na naibu wake Assef Shawkat
Waziri wa ulinzi wa Syria pamoja na naibu wake wameuawa katika shambulizi la kujitoa mhanga lililofanywa dhidi ya makao makuu ya ulinzi mjini Damascus.
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa runinga ya kitaifa nchini Syria.
Daoud Rajiha aliyekuwa shameji ya rais Bashar Al Asaad pamoja na naibu wake Assef Shawkat walikuwa wanahudhuria mkutano wa maafisa wakuu wa serikali wakati wa shambulizi.
Afisaa mkuu wa ujasusi pamoja na waziri wa mambo ya ndani wanasemekana kuwa katika hali mahututi.
Shambulizi hili linajiri wakati taarifa zinasema kuwa waasi wanakaribia kuuzingira mji mkuu Damascus.
Shambulizi lenyewe limetafsiriwa kama hatua kubwa katika mapambano dhidi ya utawala wa rais Assad ambao wapinzani wanataka kuuangusha.
Hatua ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga kuweza kupenya na kufanya shambulizi kama hili, dhidi ya makao ya ulinzi ya serikali ya Assad ambayo ulinzi wake unakuwa umedhibitiwa sana.
Eneo la shambulizi la kujitoa mhanga
Shambulizi la leo linazua maswali mengi kuhusu uwezo wa serikali kulinda maafisa wake na pia kuhusu hali ya usalama wa serikali ya Syria.
Huku idadi ya maafisa wakuu wanaojiuzulu kutoka kwa serikali ya Syria ikiongezeka, wadadisi wengi wanaamini kuwa kwa sasa hakuna nafasi kwa swali la ikiwa serikali ya Syria itaporomoka kuanzania ndani bali ni lini tu itakapoporomoka.
Wakati jeshi pamoja na zana zake nzito mfano vifaru na ndege za kivita, likiwa bado lina uwezo mkubwa wa nguvu dhidi ya upinzani, kuna dalili kuwa linakabiliwa na changamoto kubwa katika mashambulizi ya ardhini.
Hata hivyo wafuasi wa rais Assad wa madhhebu ya Alawite hawana pa kwenda. Hali hii inazua hofu ya kuchochea aapigano ya kikabila yanayoendelea nchini humo ikiwa rais Assad atangolewa madarakani.

No comments:

Post a Comment