NJOMBE

NJOMBE

Monday, July 9, 2012

Wanavijiji Wakristo Nigeria wauwawa

Jeshi la Nigeria linasema kuwa watu 37 wameuwawa kwenye mashambulio katika vijiji vya Wakristo karibu na mji wa Jos, katikati mwa nchi.
Mashambulio kadha yameshawahi kufanywa Nigeria


Msemaji wa jeshi, Mustapha Salisu, alisema askari wa usalama walipigana vikali kwa saa kadha, na wale aliosema walikuwa washambuliaji wajuzi.
Alisema zaidi ya washambuliaji 20 waliuwawa.
Msemaji wa kikundi cha Wakristo alisema vijiji 13 vilishambuliwa.

No comments:

Post a Comment