NJOMBE

NJOMBE

Saturday, July 14, 2012

Kamanda wa Afghanistan auliwa harusini

 
Mwanasiasa mmoja maarufu nchini Afghanistan ameuliwa na mtu aliyejitolea mhanga, kwenye harusi ya mtoto wake wa kike.
Ahmed Khan Samangani
Watu zaidi ya ishirini waliuwawa kwenye mripuko wa bomu na wengine wengi kujeruhiwa.
Mwanasiasa huyo, Ahmad Khan Samangani, alikuwa akiamkia wageni kwenye harusi, pale mtu aliyekuwa na bomu alipomkumbatia, na kuripua bomu.
Bwana Samangani kutoka kabila la WaUzbek, aliwahi kuwa kamanda wa wapiganaji.
Baadae akachaguliwa kuwa mbunge, lakini aliendelea kuongoza kundi kubwa la askari waliokuwa na silaha.
Msemaji wa Taliban, alikanusha kuwa wao walihusika na shambulio hilo.

No comments:

Post a Comment