NJOMBE

NJOMBE

Friday, July 20, 2012

Umoja wa mataifa kushtaki Habre

Hissen Habre
Hissen Habre
Majaji katika Mahakama ya Juu zaidi ya Umoja wa Mataifa wana njia mbili wanazoweza kufuata kumsthaki aliyekuwa kiongozi wa Chad Hissen Habre, aliye uhamishoni nchini Senegal.
Wanaweza kulazimisha Senegal kumshtaki Hissene Habre kienyeji au wamhamishe hadi Ubeligiji ashtakiwe huko.
Dikteta huyo wa zamani aliyejulikana kama "Pinoche wa Afrika" amekuwa akiishi uhamishoni tangu apinduliwe mamlakani mwaka 1990.
Analaumiwa kwa kuwaua makumi ya maelfu ya watu alipokuwa akitawala Chadi kati ya mwaka 1982 hadi 1990. Amekanusha mashtaka hayo.
Habre alifikishwa katika mahakama mara ya kwanza nchini Senegal mwaka 2000 lakini mahakama za nchi hiyo zikaamua kuwa hazina mamlaka ya kusikiliza kesi yo yote dhidi yake.
Walioathirika na utawala wake waliwasilisha mashtaka dhidi ya Habre nchini Ubelgiji.
Baada ya uchunguzi wa miaka minne, Jaji mmoja wa Ubelgiji aliomba Senegal imhamishie nchini mwake.
Baada ya uamuzi huo Senegal ilikubali kuwa itamshtaki Habré katika mahakama zake lakini hatua hiyo imecheleweshwa kwa miaka sasa. Hii ni mara ya nne Ubelgiji kuomba Habre ahamishwe hadi nchini Ubelgiji. Uamuzi wa ICJ utakuwa wa mwisho.

No comments:

Post a Comment