NJOMBE

NJOMBE

Sunday, July 22, 2012

Wapinzani walalama Kilimo kupewa fedha kiduchu

KAMBI ya Upinzani Bungeni imelalamikia fedha kidogo zilizotolewa kwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika katika mwaka wa fedha 2011/12.
Kambi hiyo ilisema kati ya Sh258.35 bilioni zilizoidhinishwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida,  fedha za matumizi zilizopelekwa wizarani kutoka hazina kufikia Mei 31, mwaka huu ni Sh103.06 bilioni, sawa na asimilia 67.62.
Msemaji wa kambi hiyo kwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Rose Kamili alisema kwa upande wa fedha za maendeleo hadi kufikia Mei 31, zilizokuwa zimepelekwa wizarani kutoka hazina ni Sh72.63 bilioni ambazo ni sawa na asilimia 68.56 ya fedha zilizoidhinishwa.

“Huu ni uthibitisho kamili kwamba malengo yaliyopangwa kufikiwa mwaka wa fedha 2011/12 hayakufikiwa,” alisema Kamili alipokuwa akiwasilisha maoni ya kambi yake kuhusu makadirio ya matumizi ya wizara hiyo.
Aliongeza kuwa: “Serikali itoe maelezo mbele ya Bunge hili kwa nini tuipatie fedha inazoomba kwa wizara hii, wakati mwaka jana haikutekeleza bajeti iliyoidhinishwa na Bunge, hivyo kuzorotesha malengo yake.”
Alisema taarifa ya utekelezaji ya Wizara ya Kilimo, inaonyesha bajeti imepungua kutoka Sh258.35 bilioni  mwaka 2011/12 hadi Sh237.624 bilioni sawa na punguzo la asimilia 8.7.
 “Pamoja na kupungua kwa bajeti, matumizi  ya kawaida yameongezeka  kutoka Sh152.41 bilioni mwaka uliopita hadi Sh170.364 bilioni, sawa na  ongezeko la asilimia 11.78,”alisema Kamili ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) na kuongeza:
“Wakati matumizi ya kawaida yameongezeka kwa takriban asilimia 12, bajeti ya maendeleo katika wizara hii imepungua kutoka Sh105.94 bilioni mwaka 2011/12 hadi Sh67.260 bilioni ikiwa ni anguko la asilimia 57.5.”
Alisema kwa takwimu hizo ni dhahiri kwamba hakuna mkakati wa dhati wa kutekeleza kauli ya Kilimo Kwanza, kwani licha ya bajeti ya maendeleo kupungua, imeendelea kuwa tegemezi kwa fedha za nje kwa asilimia 77.7.
“Tafsiri ya utegemezi huu ni kwamba sasa Serikali imeamua kukiweka kilimo chetu rehani,” alisema

No comments:

Post a Comment