NJOMBE

NJOMBE

Monday, July 23, 2012

Mvua na dhoruba yaleta mafuriko Beijing

Mji Mkuu wa Uchina, Beijing, umepata mvua kubwa kabisa kuwahi kutokea kwa zaidi ya miaka 60.
Mafuriko mjini Baijing

Watu kama 10 wamekufa, na maelfu wamehamishwa makwao.
Mvua kubwa ya jana ilifurika mabara-barani, kupeperusha mapaa, na kuporomosha miti na milingoti ya taa.
Maji mjini yalikuwa yanafika kiunoni.
Safari za ndege zaidi ya mia mbili zilivunjwa, na hivo kuwaacha maelfu ya watu wamenasa kwenye viwanja vya ndege.
Mvua sasa imeanuka mjini Beijing, lakini mvua kubwa inatarajiwa kaskazini-mashariki na kusini-magharibi mwa Uchina.

No comments:

Post a Comment