NJOMBE

NJOMBE

Thursday, August 16, 2012

Assange apewa hifadhi na Ecuador


 
Wafuasi wa Bwana Assange
Wafuasi wa Bwana Assange waliokusanyika nje ya Ubalozi wa Ecuador mjini London
Ecuador imeamua kumpatia hati ya ukimbizi muasisi wa mtandao wenye utata wa Wikileaks, Julian Assange.
Ubalozi wa Ecuador mjini London umesema kuna wasi wasi kuwa haki za kibinadam za Bwana Assange huenda huenda zikakiukwa.
Assange amekuwa akiishi kwenye ubalozi wa Equador mjini London kwa miezi miwili iliyopita kuepuka kupelekwa nchini Sweden ambako anakabiliwa na mashtaka ya ubakaji.
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imesema uamuzi wa Bwana Asange wa kuomba hifadhi ya ukimbizi hautahujumu azma na nia yake ya kutaka asafirishwe hadi nchini Sweden, kufunguliwa mashtaka.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Equador, Ricardo Patino, amesema kuna hatari kuwa Bwana Assange akasafirishwa kutoka Swesen kwa lazima hadi Marekani, kukabiliana na mashtaka ya kufichuliwa kwa mtandao wake wa kidiplomasia.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ecuadorean, Ricardo Patiño, aliwaambia waandishi wa habari kuwa nchi yake itachukua hatua ziwezekanazo kukwepa kile akilichokitaja kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.
Serikali ya Uingereza imesema, haitamruhusu Bwana Assange, kuondoka nje ya ubalozi huo na kuwa atakamatwa atakapotoka nje.
Akitangaza uamuzi wa serikali yake Bwana Platino amesema, Ecuador inaamini madai yaliyotolewa na Bwana Assange kuwa ananyanyaswa kisiasa ni ya kweli.
Tangazo hilo lilitolewa moja kwa moja njia ya video kutoka mji mkuu wa Ecuador, Quito.
Nje ya ubalozi wa Ecuador, mjini London, wafuasi wa Bwana Assange ambao walikuwa wamekusanyika walifurahiswa na tangazo hilo.
Mwandishi wa masuala ya kisheria wa BBC, Clive Coleman amesema uhusiano kati ya Uingereza na Ecuador umehujumiwa pakubwa na uamuzi huo wa kuumpa hifadhi bwana Assange na hatma ya ubalozi huo mjini London haijulikani.

No comments:

Post a Comment