NJOMBE

NJOMBE

Friday, May 11, 2012

Waasi washambulia gereza nchini Nigeria

  Watu wenye silaha wamevamia gereza nchini Nigeria, katika jimbo la Kaskazini Mashariki la Borno, na kuua walinzi wawili wa gereza hilo na kuwafungulia wafungwa.

Polisi wamesema wapiganaji kutoka kikundi la Kiislam la Boko Haram, kwanza walikishambulia kituo cha polisi katika mji wa Banki, kabla ya kwenda kuvamia gereza karibu na kijiji cha Kunshi.
Msemaji wa polisi amesema wamewakamata watu 23.
Hakuna kikundi kilichodai kuhusika na shambulio hilo lakini kikundi cha Boko Haram kimelaumiwa kwa kuhusika na matukio ya aina hii kaskazini mwa Nigeria.

No comments:

Post a Comment