NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, May 22, 2012

Mhemko kwa vijana

TUMEKUTANA tena kwenye kona yetu tuipendayo ya mahaba ili kujuzana machache kuhusiana na maisha ya kila siku.
Leo nataka kuzungumzia kichaa cha mapenzi kwa wanafunzi, hii imetokea baada ya kupokea simu nyingi za wanafunzi waliojiingiza kwenye mapenzi na kusahau kuwa wapo katika masomo.

Najua kila mmoja amepitia hatua hii ambayo mwanadamu huanza kujengeka kimuhemko ambayo humuandaa kwa ajili ya kufanya tendo la ngono. Kila mwanaume anapopevuka huanza kuwa na tamaa ya kufanya ngono hasa anapoziona sehemu zinazomshawishi kufanya ngono kwa mwanamke.
Mwanaume akiishapevuka akiziona sehemu za mwanamke kama matiti mapaja mgongo ukiwa wazi makalio yaliyovimba. Na baadhi ya sehemu za mwili wa mwanamke ambazo zina kishawishi cha ngono kwa asilimia 90, pia humshawishi kutamani ngono.

Kwa msichana naye akishavunja ungo huanza kupata mihemko hata mwenyewe akijishika baadhi ya sehemu uhisi kuitaji kitu fulani ambacho si kingine, ni kufanya ngono. Msichana anapojisugua sehemu za siri au kwenye matiti ambayo huwa na maumivu ya mbali ukiyakanda hupunguza muwasho.

Vitu hivi vimekuwa vikiwafanya wasichana wengi wasio na uvumilivu kuanza kutafuta mtu wa kumpunguzia vitu vinavyomsumbua au mwanaume kutafuta msichana kwa ajili ya kufanya naye mapenzi.
Katika kufanya uchunguzi wangu wa kina nimegundua pamoja na hali hiyo vipi vitu vinavyo waingiza vijana kwenye ngono kabla ya wakati wake, kimoja ni tamaa ya kutaka akiwa shuleni naye awe na baadhi ya vitu vilivyopo nje ya uwezo wake ambavyo humfanya ajirahisi kwa kuutoa mwili wake.

Hata wanaume ambao kwa sasa wamekuwa wakisakwa na Mama Sukari kwa kuwahonga na kufanya nao ngono kwa kugeuzwa chombo cha starehe.
Pia wapo wanaoingia katika mtandao huu kwa kufuata mkumbo kwa kupenda kusikiliza simulizi za ngono kwa watu wenye tabia hizo naye kujaribu kutokana na kusikia sifa ya kitu kile bila kujua muda wake bado. Wengine kuangalia picha za ngono ambazo humfanya apate muhemko na kujikuta akimtafuta wa kumtuliza muhemko wake.

Lakini vitu hivi vinawezekana kabisa kuvishinda, kwanza lazima ujijue una umri gani, nini madhara ya kufanya mapenzi katika umri mdogo. Pia kujua nini malengo yako katika maisha ngono na elimu, nini kitakacho kubeba hata kama wazazi wako wamekufa.

Tatu, kuijua thamani ya usichana wako au uvulana wako kwa kujitunza ili siku moja ufikie malengo yako. Kwa mwanamke ambaye ndiye aliye katika kundi baya la kuathirika kama ataendekeza ngono, jivunie kukutwa bado msichana japo kwa sasa ni jambo gumu kama kuliona jua saa mbili usiku. Kumbuka kosa lako moja linaweza kukuharibia mfumo mzima wa maisha.
Jiepusheni na vitendo ambavyo mnaamini ndivyo vitakavyo kufanyeni muonekane mnakwenda na wakati. Kufanya ngono katika umri mdogo kuna hasara nyingi mojawapo kuunguza mayai ambayo huungua na kukufanya uwe tasa.

Pia kuvuruga ndoto zako ambazo zinatakiwa uvumilivu na kujiepusha na chochote ambacho unakiona kitakupotosha na kukuvurugia malengo yako. Kama utayafuata haya machache, hakika utashinda na kufikia ulichopanga.

No comments:

Post a Comment