NJOMBE

NJOMBE

Sunday, May 13, 2012

Honi kali zitatumiwa kwenye Olimpiki


Wizara ya Ulinzi ya Uingereza imethibitisha kuwa chombo kama honi, kitatumiwa kama silaha mjini London wakati wa michezo ya Olimpiki.
Mazoezi ya ulinzi kwenye Mto Thames, London

Kelele za chombo hicho zinaweza kuvuma kwa masafa marefu na kuumiza masikio.
Chombo hicho kimetumiwa sehemu kadha za dunia kutawanya mkusanyiko wa watu; na kinatengenezwa Marekani ambako kimearifiwa kuharibu masikio daima.
Lakini Wizara ya Ulinzi inasema kitatumiwa tu kwenye vipaza sauti kuzuwia misafara kwenye Mto Thames; na ni sehemu ya zana kadha zitazotumiwa kuhakikisha usalama wa Olimpiki.
Chombo hicho kinatumiwa kupambana na maharamia wa Somalia.

No comments:

Post a Comment