NJOMBE

NJOMBE

Sunday, May 27, 2012

Mtumishi wa Papa Benedict akamatwa

 Polisi wa Vatikani wamemshtaki rasmi mtumishi wa Papa Benedict, katika kesi inayohusu wizi wa nyaraka za siri.

Paolo Gabriele na Papa Benedict
Paolo Gabriele - ambaye akitumika kwenye fleti ya papa - amezuwiliwa Vatikani, na ameruhusiwa kuonana na mawakili wawili.
Wakuu wanachunguza vipi, katika miezi ya karibuni, magazeti ya Utaliana yalipata nyaraka ambazo zinaeleza mashindano kati ya wakuu wa kanisa - kisa ambacho kimeanza kuitwa 'Vatileaks'.
Inaarifiwa kuwa Papa Benedict ameshangazwa na kusikitishwa kuwa mtumishi wake mmoja amekamatwa.
Mkuu wa Benki ya Vatikani alitolewa kazini Alkhamisi, kutokana na kashfa hiyo.

No comments:

Post a Comment