NJOMBE

NJOMBE

Friday, May 25, 2012

Marekani ya kata misaada kwa Pakistan

Kamati ya baraza la senate nchini Marekani, imekata misaada ya kwa serikali ya Pakistan kwa dola milioni thelathini na tatu kila mwaka.
shakil afridi
Marekani inasema hakutendewa haki
Hatua hiyo imechukuliwa kujibu uamuzi wa mahakama moja nchini humo wa kumfunga daktari ambaye alisaida Idara ya Ujasusi CIA, kumnasa Osama Bin Laden.
Shakil Afridi alihukumiwa kifungo cha miaka thelathini na tatu baada ya kupatikana na hatia ya uhaini.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton, amesema dakatari huyo kamwe hakufanyiwa haki na haikubaliki.
Mwaka jana, kikosi maalum cha jeshi la Marekani kilimuua Osama bin Laden, mjini Abbottabad Pakistan, alipokuwa amejificha.
Mauaji ya Osama, yalizua tofauti kati Marekani na Pakistan, nchi ambazo zimekuwa na ushirikiano wa karibu hasaa katika juhudi za kukabiliana na ugaidi.
Pakistan ilichukulia operesheni hiyo ya kumsaka Osama bila idhini yake kama kuishushia hadhi yake ya kitaifa.

No comments:

Post a Comment